Skip to main content

KADA WA CCM ATIMKIA CHADEMA SONGEA


Na Giden Mwakanosya, Songea ALIYEKUWA Katibu Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Mjimwema iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoa wa Ruvuma Magdalena Zuru Gama amejivua uwanachama wa chama hicho na amejiunga katika Chama cha Democrasia na Maendeleo (CHADEMA) na amedai kuwa amefanya uamuzi huo akiwa na akili timamu ambapo ameeleza kuwa ameona chama hicho kinaendelea kukosa maendeleo na baadhi ya viongozi wa mejaa ubinafsi. Magdalena Gama alitoa kauli hiyo jana kwenye ofisi ya chadema kata ya Mjimwema wakati alipokuwa akikabidhiwa kadi mpya ya CHADEMA baada yakuomba na chama hicho kwa mwenyekiti wa CHADEMA wa tawi la Pachanne lililopo Mjimwema Swedi Milanzi ambako kulihudhuliwa na wanachama wa chama hicho. Alisema kuwa ameamua kukihama chama cha CCM baada ya kuona baadhi ya viongozi wa CCM wamekuwa na tabia ya ubinafsi na kuonekana kuwa CCM ni ya kwao wao wenyewe na kwamba kila nafasi inayotangazwa kugombea wanafanya kila njia wagombee wao wenyewe na kuwakatisha tamaa wanachama wengine wanaotaka kugombea nafsi hizo. Alifafanua zaidi kuwa alijiunga na uwananchama wa CCM tangu mwaka 1981 baada ya kupata mafunzo ya elimu ya siasa kwa muda wa miezi 3 hivyo alikuwa mwanachama wa muda mrefu na amewahi kushika nyadhifa mbalimbali za chama hicho licha ya kuwepo mizengwe ya hapa na pale iliyokuwapo ikifanywa na baadhi ya viongozi ambao walioifanya chama cha CCM ni mali yao,hivyo ameamua kujiunga na chama cha Chadema ambacho ndio chama pekee chenye sera nzuri zenye tija kwa watanzania. Kwa upande wake mjumbe wa Halmashauri kuu ya Taifa ya chama hicho Samweli Chale alisema kuwa kitendo alichokifanya Magdalena Gama kukihama chama cha Ccm na kukimbilia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ni cha kiungwana kwani Ccm imejaa fitina hasa kwa wale Viongozi wanaoonekana kwa jamii kuwa makini. Chale ambaye pia ni mwenyekiti wa chama cha Democrasia na Maendeleo (Chadema) kata ya Bombambili alisema kuwa msimamo wa Chadema ni kuboresha zaidi maendeleo mbalimbali ya wananchi na kila malengo makini ya kuhakikisha kuwa chama kinashika dola kuanzia ngazi ya uongozi wa Serikali za mitaa,vitongoji na vijiji na kwamba hakuna chama kingine chenye kipaombele ni Chadema peke. Naye Mwenyekiti wa Baraza la vijana Chadema(Bavicha) wa Kata ya Mjimwema John Mkina alieleza kuwa nguvu ya chama inazidi kuongezeka na alidai kuwa baadhi ya viongozi wa Chama cha Mapinduzi wameonesha nia ya kutaka kujiunga na chama hicho hivyo Magdalena Gama ni sehemu ya wananchama wengi waliomba kutaka kujiunga na Chadema ambao wanataraijwa kukaribishwa kwa mikono miwili kujiunga na chama hicho

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

MAJINA YA WASHIRIKI NA WA WEZESHAJI WA FILM YA HOUSE GIRL!

CAST SELEMANI MOHAMED / BUNTO ANDREW / C-O YORAM MWETA / MGANGA MWANTUMU / MKE WA C-O JOHN / MCHUNGAJI BI FURURATU / JINI WAOMBOLEZAJI SAUMU HUSENI HASHIMU BABA RASTA MAN YOHANNA TAMILWAI SAIDI MWALUBADU SEMY STIR SELEMANI MOHAMEDI  AND ANDREW C-O LOCATION ATHUMANI HAMADI MAKE UP MWASHAMBA RAMADHANI BEDUI DEREVA DAUDI SPOONSER SAIDI SHABANI AND THE FRESH2012 GLOB SOUND PRODUCER J-B LIGHT YOHANNA TAMILWAI THENK YOU THE FRESH ENERTAINMENT AND THE FRESH2012 BLOG CONTACTS 0653785027 +255714091786 ZAIDI TEMBELEA www.the-fresh.blogspot.com ADRESS Thefresh@ymail.com AU Saidshabani60@gmai.com

Video: Blackchild – Put Inside

David Abdulichel, also known as BlackChild is a Ghanaian from Asanti origin, born and raised in Lagos Nigeria. BlackChild, who is a recording artist, song writer and performer started his music career back in 2000 and since then has released four singles. He has also worked with top producers in Nigeria such as Fliptyce, Spanky, Meca E & BrainMix to mention but few. BlackChild Abdul rose to prominence with his hit songs “Treasure”, “Ele” featuring Rock Steady, “Could It Be Love” featuring Cartiar, “All I Need” featuring Solid Star. This time around he comes out with “Put Inside” which sees him delivering lines in french and his native language and is steadily generating buzz and enjoying airplay on radio stations within and outside Lagos. Listen up!