Skip to main content

Macho yote Qunu: Buriani Tata Madiba

Qunu. Huzuni na simanzi viliyateka maeneo ya Mthatha na Qunu katika Jimbo la Eastern Cape, Afrika Kusini baada ya kuwasili kwa mwili wa rais wa kwanza mzalendo wa nchi, Nelson Mandela.
Mwili wa Mandela uliwasili jana katika Uwanja wa Ndege wa Mthatha saa 7:40 mchana (kwa saa za huku) dakika 20 kabla ya muda uliotarajiwa, ukiwa umesafirishwa kutoka Uwanja wa Ndege wa Jeshi wa Waterkloof, Pretoria.
Ulisindikizwa na maofisa waandamizi wa Jeshi la Afrika Kusini (SANDF), maofisa kutoka Serikali, wawakilishi wa familia yake na viongozi wa mila kutoka kabila la abaThembu.
Mandela anazikwa leo katika makaburi ya familia yaliyopo katika Kijiji cha Qunu ambako alikulia, katika mazishi ambayo yatakuwa mchanganyiko wa mila na desturi, dini yake ya Kikristo ikifuata taratibu za kimethodisti na kijeshi kwa maana ya Serikali,
 Alizaliwa katika Kijiji cha Mvezo, Julai 18, 1918 na alifariki dunia Desemba 5, mwaka huu nyumbani kwake, Houghton, Johannesburg akiwa na umri wa miaka 95 baada ya kuugua magonjwa ya figo kwa zaidi ya mwaka mmoja.
Maziko yake yanamaanisha kuhitimishwa kwa siku 10 za maombolezo ya kitaifa, ambayo yalishuhudia mamia ya viongozi kutoka pande zote za dunia, waliofika Afrika Kusini kushiriki Ibada ya Kitaifa iliyofanyika katika Uwanja wa FNB, Soweto   Jumanne iliyopita.
Jeneza lililobeba mwili wa aliyekuwa Rais wa Kwanza Mzalendo wa Afrika Kusini, Nelson Mandela lilipofikishwa Uwanja wa Ndege wa Mthatha jana. Maziko yanafanyika leo kijijini kwao, Qunu kwa taratibu za kimila. PICHA | AFP   
Kadhalika mwili wa kiongozi huyo kwa siku tatu mfululizo; Jumatano hadi Ijumaa wiki hii ulikuwa ukiwekwa katika Ikulu ya Pretoria iliyopo Majengo ya Umoja (Union Buildings) ambako waombolezaji zaidi ya 100,000 walipata nafasi ya kutoa heshima zao za mwisho.
Serikali ya Afrika Kusini imetaganza kuwa leo ni siku ya mapumziko huku wamiliki wa maduka makubwa nao wakitangaza kwamba hawatafungua biashara zao kama hatua ya kuienzi siku ya mwisho ya Mandela.
 Rais Jakaya  Kikwete na Rais wa Malawi, Joyce Banda ni wakuu wa nchi pekee ambao watahudhuria mazishi ya Mandela na wote wamepangiwa kutoa salaamu za rambirambi wakati wa mazishi. Watawaongoza viongozi wengine kadhaa wakiwamo wale wanaowakilisha mashirika ya kimataifa.
Simanzi uwanjani
Uwanja wa Ndege wa Mthatha ulikuwa kimya hasa baada ya ndugu wa karibu wa Mandela, wakiongoza na mjane Graca Machel kuwasili saa 6:44 mchana na kulakiwa na viogozi mbalimbali wakiongozwa na Waziri wa Ulinzi, Nosiviwe Mapisa Nqakula.
Mara baada ya jeneza kushushwa kutoka kwenye ndege ya jeshi Namba C-130, wimbo wa taifa ulipigwa, pia kupokea heshima kutoka kwa askari wa SANDF ambao walikuwa uwanjani hapo mapema.

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

MAJINA YA WASHIRIKI NA WA WEZESHAJI WA FILM YA HOUSE GIRL!

CAST SELEMANI MOHAMED / BUNTO ANDREW / C-O YORAM MWETA / MGANGA MWANTUMU / MKE WA C-O JOHN / MCHUNGAJI BI FURURATU / JINI WAOMBOLEZAJI SAUMU HUSENI HASHIMU BABA RASTA MAN YOHANNA TAMILWAI SAIDI MWALUBADU SEMY STIR SELEMANI MOHAMEDI  AND ANDREW C-O LOCATION ATHUMANI HAMADI MAKE UP MWASHAMBA RAMADHANI BEDUI DEREVA DAUDI SPOONSER SAIDI SHABANI AND THE FRESH2012 GLOB SOUND PRODUCER J-B LIGHT YOHANNA TAMILWAI THENK YOU THE FRESH ENERTAINMENT AND THE FRESH2012 BLOG CONTACTS 0653785027 +255714091786 ZAIDI TEMBELEA www.the-fresh.blogspot.com ADRESS Thefresh@ymail.com AU Saidshabani60@gmai.com

Video: Blackchild – Put Inside

David Abdulichel, also known as BlackChild is a Ghanaian from Asanti origin, born and raised in Lagos Nigeria. BlackChild, who is a recording artist, song writer and performer started his music career back in 2000 and since then has released four singles. He has also worked with top producers in Nigeria such as Fliptyce, Spanky, Meca E & BrainMix to mention but few. BlackChild Abdul rose to prominence with his hit songs “Treasure”, “Ele” featuring Rock Steady, “Could It Be Love” featuring Cartiar, “All I Need” featuring Solid Star. This time around he comes out with “Put Inside” which sees him delivering lines in french and his native language and is steadily generating buzz and enjoying airplay on radio stations within and outside Lagos. Listen up!