Skip to main content

Serikali ya Tanganyika yaibuliwa katika Rasimu ya pili

Jambo jingine jipya ni kupunguzwa kwa madaraka ya uteuzi ya Rais kwa kuweka vyombo vya kupendekeza majina ya watu wa kuteuliwa na baadhi ya vyeo kuhitaji kuthibitishwa na Bunge.PICHA|MAKTABA 

Dar es Salaam.Tume ya Mabadiliko ya Katiba imetoa Rasimu ya Pili ya Katiba ikiwa na mambo sita mpya, huku ikiendelea kupendekeza Muungano wa Serikali tatu na kurejea kwa nchi ya Tanganyika.
Rasimu hiyo ya Pili ambayo imetolewa miezi saba baada ya Rasimu ya Kwanza, ilikabidhiwa jana kwa Rais Jakaya Kikwete na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba katika hafla iliyofanyika kwenye Viwanja vya Karimjee, Dar es Salaam. Akizungumza kabla ya kukabidhi rasimu hiyo, Jaji Warioba alisema ina Ibara 271, tofauti na ile ya kwanza iliyokuwa na Ibara 240.
Alisema ripoti ya rasimu hiyo pia ina maoni ya wananchi kuhusu mabadiliko ya Katiba, sera, sheria na utekelezaji maoni ya Mabaraza ya Katiba, takwimu za ukusanyaji wa maoni ya wananchi, makala za utafiti kuhusu mabadiliko ya Katiba na viambatanisho vya ripoti ya mabadiliko ya Katiba.
Mambo mapya
Maeneo yaliyofanyiwa marekebisho baada ya mchakato wa Mabaraza ya Katiba yaliyokutana kuanzia Julai 12 hadi Septemba 2 mwaka huu ni kuongezwa kwa vipengele kuhusu haki za binadamu.
Miongoni mwao ni haki ya kutoa na kupata habari. Pia imetaja haki za makundi maalumu yakiwamo ya watoto, vijana, wazee, walemavu na wanawake.
Kuhusu uraia, Jaji Warioba alisema imependekezwa uraia wa Tanzania kuwa mmoja tu na kutambuliwa kwa uraia wa kuzaliwa na wa kujiandikisha wa nchi moja. Alisema imependekeza pia kutoa fursa kwa uraia wa nchi mbili.
Jambo jingine jipya ni kupunguzwa kwa madaraka ya uteuzi ya Rais kwa kuweka vyombo vya kupendekeza majina ya watu wa kuteuliwa na baadhi ya vyeo kuhitaji kuthibitishwa na Bunge.
Aidha, alisema rasimu hiyo imependekeza Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa iwe taasisi inayojitegemea badala ya kuwa sehemu ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) kama ilivyokuwa katika Rasimu ya Kwanza.
“Rasimu inapendekeza kuwepo na Jeshi moja la polisi na Idara moja ya Usalama kwa taifa zima, siyo kama tulivyokuwa imependekezwa katika rasimu ya kwanza kwamba kila upande unaweza kuanzisha jeshi lake la polisi,” alisema.
Muungano
Akizungumzia Muungano na jinsi Tume ilivyofanya uchambuzi wa pendekezo lake la Serikali tatu alisema: “Katika Rasimu ya Kwanza tulieleza kuwa kuendelea kwa Serikali mbili kulihitaji ukarabati mkubwa ambao tuliona hautawezekana.

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

MAJINA YA WASHIRIKI NA WA WEZESHAJI WA FILM YA HOUSE GIRL!

CAST SELEMANI MOHAMED / BUNTO ANDREW / C-O YORAM MWETA / MGANGA MWANTUMU / MKE WA C-O JOHN / MCHUNGAJI BI FURURATU / JINI WAOMBOLEZAJI SAUMU HUSENI HASHIMU BABA RASTA MAN YOHANNA TAMILWAI SAIDI MWALUBADU SEMY STIR SELEMANI MOHAMEDI  AND ANDREW C-O LOCATION ATHUMANI HAMADI MAKE UP MWASHAMBA RAMADHANI BEDUI DEREVA DAUDI SPOONSER SAIDI SHABANI AND THE FRESH2012 GLOB SOUND PRODUCER J-B LIGHT YOHANNA TAMILWAI THENK YOU THE FRESH ENERTAINMENT AND THE FRESH2012 BLOG CONTACTS 0653785027 +255714091786 ZAIDI TEMBELEA www.the-fresh.blogspot.com ADRESS Thefresh@ymail.com AU Saidshabani60@gmai.com

Video: Blackchild – Put Inside

David Abdulichel, also known as BlackChild is a Ghanaian from Asanti origin, born and raised in Lagos Nigeria. BlackChild, who is a recording artist, song writer and performer started his music career back in 2000 and since then has released four singles. He has also worked with top producers in Nigeria such as Fliptyce, Spanky, Meca E & BrainMix to mention but few. BlackChild Abdul rose to prominence with his hit songs “Treasure”, “Ele” featuring Rock Steady, “Could It Be Love” featuring Cartiar, “All I Need” featuring Solid Star. This time around he comes out with “Put Inside” which sees him delivering lines in french and his native language and is steadily generating buzz and enjoying airplay on radio stations within and outside Lagos. Listen up!