Kampuni ya facebook ambao ndio mtandao unaoongoza kuwa na wanachama duniani ikiwa chini ya mmiliki wake Mark Zuckerberg inatarajiwa kupandishwa mahakamni nchini Marekani na wawekezaji walionunua hisa za kampuni hiyo baada ya kufanya udanganyifu kwenye mauzo ya hisa zao. Wawekezaji hao ambao walinunua hisa hizo wanaituhumu kampuni hiyo kwa kuficha na kutoa takwimu za uongo juu y thamani halisi ya bei ya
hisa hizo, Kwani ikiwa chini ya uuzaji wa benki ya Morgan Stanley walificha kuporomoka kwa thamani ya hisa hizo kwa zaidi ya asilimia 18 kitendo ambacho kimepelekea wawekezaji hao kupata hasara, Kesi hiyo itasikilizwa nchini Marekani.
