Skip to main content

Posts

Showing posts from January, 2013

NGOMA YANDUGU YANGU MKONGWE RUWA

Mkongwe Ruwa ft misosi & Top C Urembo wako

Check Show ya T.I.D na Top Band Ndani ya New Maisha Club

Dully na TID wakifanya mambo yao TID na marafiki zake TID na swahiba wake Country Boy akitambulisha wimbo aliomshirikisha TID, Always wadau wa muziki waliokuwepo kwenye show Mwanadada aliyewahi kufanya kazi na TID

LULU MICHAEL AKATAA KUFANYIWA "SHEREHE" YA KUPONGEZWA KUINGIA URAIANI

January 29 2013 ndio msajili a li thibitisha kwamba mwigizaji Lulu ametimiza masharti yote ya dhamana juu ya kesi inayomkabili ya kuua bila kukusudia na hivyo  kumwachia  kwa dhamana.....   Lulu na mama yake mzazi wote kwa pamoja waliangua vilio baada ya dhamana yao kukamilika wakati wakiwa nje ya Mahakama kabla ya kuondoka na Lulu kuingia uraiani. Kabla  ya dhamana  hiyo kulikwa  na  tetesi  kwamba  Lulu a ngefanyiwa  sherehe kubwa  ya  kupongezwa  kuja uraiani. Kwa mujibu wa ndugu yake  wa karibu, L ulu amegoma  kufanyiwa sherehe  na  badala  yake jana a li waomba  watanzania  wamuombee  kwa  mungu  maana  kesi bado inaendelea.....    “Nawashukuru watu wote na nilikua naomba watu waendelee kuniombea sababu hii ni dhamana tu lakini kesi bado ina safari ndefu… nawashukuru wale wote waliokua na mimi kwa hali yeyote ile na zaidi zaidi namshukuru sana Mwenyezi Mungu” .... LULU

SIKILIZA NGOMA MPYA SHIZAN FEAT BAGUJE

  Shizan ft Baguje=Mama jojo

ROMA MKATOLIKI AIACHIA NGOMA YAKE - 2030 MTANDAONI HII HAPA

Roma_-_2030_(Version_2).mp3   Habari mabibi na mabwana!! poleni na mihangaiko ya siku!! naam ijumaa iliyopita nilitoa kibao changu maridhawa kipya kabisa kinaitwa 2030!!! na nilikiachia kwa radio stations zote nchini kadri ya uwezo wangu/wetu, though kutokana na mawasiliano ni ngumu kufikia radio zote kwa wakati, ila nyingi ziliupata!!! lakini niliweka utaratibu fulani kwa watakaohitaji kuupata huo wimbo 2030 mbali na radio basi wataupata kwa kussuport kuununua on line kwa tsh 3000/=!!nilishatangaza sana mnafahamu!!ilikuwa ni trial ya kuona nani ana love ya kussuport na nani hana kupitia njia zilizowekwa na sio njia nyingine. zoezi limeenda kwa challenge nyingi sana asante wote waliossuport katika hili, pia asante kwa wale walioliharibu zoezi hili maana imenifanya nimtambue hu z real na hu z fake!!! imeniuma kuona wapo wasanii wanafanya biashara kama hii wanauza mix tapes, album,tisherts zikiwa zote ni movements za kuleta changes ktk mziki wetu, then hao hao wanakuwa mstari

Ving'amuzi vyawatesa wakazi Dar

  Kuzimwa kwa mitambo ya kurushia matangazo ya televisheni kwa mfumo wa analojia, kumezua utata baada ya wakazi wengi wa Mkoa wa Dar es Salaam kushindwa kupata matangazo. Mitambo hiyo ilizimwa juzi usiku kwa maelekezo ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).Baadhi ya wakazi wa jijini Dar es Salaam, wamesema hawapati matangazo ya televisheni licha ya kununua ving’amuzi. Aidha, wamesema chaneli tano zilizopewa leseni na serikali kuendelea kurusha matangazo yao, nazo zinaonyesha chenga chenga. Baadhi ya watu waliozungumza na gazeti hili jana, walidai kuwa mfumo huo umeleta usumbufu mkubwa kwao. “Mimi mwenyewe nimekumbwa na tatizo hili tangu jana baada ya mitambo hiyo kuzimwa, sipati tena zile chaneli tano ambazo serikali ilisema ni lazima zionyeshwe ili Watanzania waendelee kuona hata kama vocha zao zitakuwa zimekwisha,” alisema mkazi mmoja wa jijini Dar es Salaam, ambaye hata hivyo, hakutaka jina lake liandikwe gazetini. Alidai kwamba kituo cha TBC tu ndiyo kilikuw

RAIS KIKWETE NA MAMA SALMA KIKWETE WAENDA KUTOA POLE NYUMBANI KWA MAREHEMU SAJUKI LEO....

  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa msanii wa filamu Marehemu Juma Kilowoko '  Sajuki' nyumbani kwao wafiwa Tabata Bima jijjini Dar es salaam leo Januari 4, 2013.     Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiweka saini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa msanii wa filamu Marehemu Juma Kilowoko '  Sajuki' nyumbani kwao wafiwa Tabata Bima jijjini Dar es salaam leo Januari 4, 2013.  Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete wakiwa nyumbani kwa msanii wa filamu Marehemu Juma Kilowoko '  Sajuki' Tabata Bima jijjini Dar es salaam leo ambako walienda kutoa pole leo Januari 4, 2013