Skip to main content

Posts

Showing posts from August, 2012

MAMBO MANNE YANAYOWAVUTIA WATALII MAPANGO YA AMBONI TANGA

Hussein Semdoe, Tanga KUMBE mapango maarufu ya Amboni yaliyopo katika Kata ya Kiomoni, Tarafa ya Chumbageni wilayani Tanga, Mkoa wa Tanga, ni sehumu muhimu ya kujivunia na ya kihistoria ya nchi yetu, kutokana na miamba ya mapango hayo kituo cha hija kwa watu mbalimbali wa ndani na nje ya Tanzania .   Kutokana na umuhimu wa mapango hayo watu 42, wamekuwa wakitembelea kila siku kwa ajili ya kufanya matambiko na kutoa sadaka kwa kizimu. Mambo yanayovutia Mapango ya Amboni Mambo manne yanayowavutia wataliii katika mapango hayo ni: mawe yakua kama mimea, sanamu ya Bikira Maria, maandiko ya Quran takatifu, miamba inayofanana na kochi na meli, na barabara zinazopita ndani ya mapango hayo.  Kwa mujibu wa utafiti, miamba hiyo inakua kwa kasi zaidi katika kipindi cha mvua, ukilinganisha na msimu wa kiangazi. Katika kipindi cha miaka 10 iliyopita ukuaji wa miamba hiyo ulikuwa kwa  milimeta 0.5 na iliwahi kuongezeka kwa kasi ya milimeta saba katika kila baada ya miaka 100.  

Sitta: Tishio Chadema ni Dk Slaa tu

Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, akiwa ameshikilia silaha za jadi baada ya kusimikwa kuwa mzee wa kimila wa kabila la Wanyambo, katika hafla iliyofanyika juzi kwenye ofisi ya CCM ya Wilaya ya Karagwe, mkoani Kagera. Picha na Edwin Mjwahuzi ADAI WENGINE NI WAZOEFU WA KUONGOZA KUMBI ZA MUZIKI, ATAMBA CCM KINA ZAIDI YA WATU 20 WENYE SIFA ZA URAIS, ZITTO AMJIBU  MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya CCM, Samuel Sitta amekiponda Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), akidai kuwa muda wake wa kutawala nchi bado, kwa kuwa hakina viongozi wa kutosha wa kufanya kazi za Serikali ukimwondoa Katibu Mkuu wake, Dk Willibrod Slaa. Sitta ambaye pia ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, alisema hayo jana alipokuwa akizungumza na baadhi ya viongozi wa CCM wa Wilaya ya Karagwe, Kagera, alikokuwa katika ziara ya kutembelea ofisi za CCM. Alisema kuna upungufu mwingi katika safu ya uongozi wa chama hicho, kutokana na kutokuwa na watu wenye uzoefu w

Kutana na watoto wahubiri. Je ni sawa?

Mamake Ezekiel na babake wa kambo ni wachungaji wa kanisa la 'Fullness of time' huko Maryland kanisa ambalo walilianza miaka mbili iliyopita.Ni katika kanisa hili ambapo hezekaiah alitawazwa kuwa mchungaji na ndugu yake shemasi mapema mwaka huu. 'Ulikuwa wakati wa ajabu kwangu' alisema Hezekiah nduguye Ezekiel mwenye umri wa miaka 13.'Kila mtu kanisani alitupigia makofi kwa furaha na kutupongeza' Micah, nduguye Hezekiah ana mumri wa miaka saba na tayari anataka kufuata nyayo zake hezekaih 'Tayari nimetayarisha mahubiri lakini nitayahubiri nitakapo hitimu miaka 10' alisema Micah kwa sauti ya unyenyekevu. Sio nchi ya marekani tu ambayo ina watoto wanaohubiri, bali Brazil pia imeboboea katika jambo hili.Indonesia pia haijawachwa nyuma kwani ina kipindi cha runi

KADA WA CCM ATIMKIA CHADEMA SONGEA

Na Giden Mwakanosya, Songea ALIYEKUWA Katibu Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Mjimwema iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoa wa Ruvuma Magdalena Zuru Gama amejivua uwanachama wa chama hicho na amejiunga katika Chama cha Democrasia na Maendeleo (CHADEMA) na amedai kuwa amefanya uamuzi huo akiwa na akili timamu ambapo ameeleza kuwa ameona chama hicho kinaendelea kukosa maendeleo na baadhi ya viongozi wa mejaa ubinafsi. Magdalena Gama alitoa kauli hiyo jana kwenye ofisi ya chadema kata ya Mjimwema wakati alipokuwa akikabidhiwa kadi mpya ya CHADEMA baada yakuomba na chama hicho kwa mwenyekiti wa CHADEMA wa tawi la Pachanne lililopo Mjimwema Swedi Milanzi ambako kulihudhuliwa na wanachama wa chama hicho. Alisema kuwa ameamua kukihama chama cha CCM baada ya kuona baadhi ya viongozi wa CCM wamekuwa na tabia ya ubinafsi na kuonekana kuwa CCM ni ya kwao wao wenyewe na kwamba kila nafasi inayotangazwa kugombea wanafanya kila njia wagombee wao wenyewe n

ASAKWA KWA TUHUMA ZA KUFANYA FUJO NA KUCHANA RAMANI YA SENSA

Na Agustino Chindiye, Tunduru MKAZI wa Kijiji cha Nampungu wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma aliyefahamika kwa jina la Said Mkepa anatafutwa na Jeshila Polisi kwa tuhuma za kufanya fujo na kuchana Ramani iliyotakiwa kutumika na karani wa kuandikisha wananchi katika Zoezi la kuhesabu watu katika Sensa ya Watu na makazi inayoendelea nchini kote. Msako huo umefuatia agizo lililotolewa na Mkuu wa Wilaya hiyo Chande Nalicho kwa jeshi hilo na akaongeza kuwa kitendo hicho kilichofanywa na mwanachi huyo pamoja na makundi mengine hakiwezi kuvumiliwa. Akifafanua taarifa hiyo alipotakiwa kuzungumzia maendeleo ya zoezi hilo katika Wilaya yake pamoja na kutaja changamoto mbalimbali zilizojitokeza siku ya kwanza Dc, Nalicho alisema kuwa mbali na kuwepo kwa changamoto hizo Wananchi wengi walijiwekeza kuhesabiwa. Aidha katika taarifa hiyo Nalicho alibainisha kuwa awali kulikuwa na vitendo vya waandikishaji kugomea zoezi hilo kwa nia ya kushinikiza malipo yao tatizo ambalo lilitatuliwa b

TANESCO YAAHIDI KUSAIDIA UPATIKANAJI WA UMEME SOKO LA SAMAKI LA KASANGA

Soko la Samaki la Kasanga.  Mazungumzo yakiendelea Ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa. Kutoka kulia ni Kaimu Meneja wa Shirika la Umeme Tanesco Mkoa wa Rukwa Emmanuel Kachewa, Mkuu wa Wilaya ya Kalambo Moshi Chang'a, Mrs. Katyega, Mkurugenzi Mkuu Msaidizi Uwekezaji wa Shirika la Umeme Nchini TANESCO Maneno Katyega, Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya, Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Alhaj Salum Mohammed Chima na Katibu Tawala Wilaya ya Kalambo Florence Mtepa.   Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akizungumza na Mkurugenzi Mkuu Msaidizi Uwekezaji wa Shirika la Umeme Nchini TANESCO Maneno Katyega Ofsini kwake jana alipotembelea Mkoani Rukwa kwa ajili ya kufuatilia miradi mbalimbali ya maendeleo ambapo alitembelea Soko la Samaki la Kasanga pamoja na kujionea maendeleo ya mradi wa umeme kwenda Wilaya ya Nkasi. Hakika ziara ya Mkurugenzi huyo Msaidizi imekuwa ya mafanikio makubwa kwani baada ya kutembelea Soko kubwa la Samaki la Kasang

Majina ya waliochaguliwa vyuo vya mifugo na kilimo haya hapa!

www.mifugo.go.tz

Assad ahitaji muda zaidi kushinda vita

Rais Bashr Al Assad Rais wa Syria Bashar al-Assad amesema kuwa serikali yake inahitaji muda wa ziada kuweza kushinda vita dhidi ya waasi nchini humo. Kwenye mahojiano na kituo kimoja cha televisheni kinachounga mkono serikali ya Assad, rais huyo pia alipuuza tamko kuwa haiwezekani kutenga maeneo ya kutolea misaada katika maeneo ya mipaka nchini humo, Wanaharakati wa upinzani wanadai kuwa jeshi limefanya mashambulizi katika maeneo mengi ya nchi hiyo kutaka kudhibiti maeneo yaliyotekwa na waasi. Mapambano makali yaliripotiwa kutokea siku ya Jumanne katika mji mkuu Damascus, Aleppo na mkoa wa kaskazini masharibi wa Idlib. Bwana Assad amesema kuwa serikali yake iko kwenye vita ndani na nje ya nchi. "bila shaka tunahitaji muda zaidi kuwe

Madaktari 50 toka India kutua nchini kesho

JOPO la madaktari 50 kutoka nchini India, wanatarajia kufanya maonesho ya matibabu katika ukumbi wa Diamond Jubilee Agosti 30 hadi 31, mwaka huu, kuanzia saa nne asubuhi hadi 11 jioni. Taarifa iliyotolewa kwa waandishi wa habari Dar es Salaam jana na Balozi wa India nchini, Bw. Debnath Shaw, ilisema maonesho hayo yameandaliwa na Taasisi ya Shirikisho la Biashara nchini India la Medical Tourism Destination (IMTD). Aliwaomba watu wenye matatizo mbalimbali ya kiafya wajitokeze katika maonesho hayo ili waweze kupata huduma ya matibabu ambayo itatolewa katika ukumbi huo kwa gharama za chini. “Gharama zao zitakuwa za chini na zitamwezesha kila mwananchi mwenye matatizo ya kiafya kuzimudu na kupata huduma, India inaongoza duniani kwa kutoa huduma bora za tiba. “Nchi yetu pia ina madaktari bingwa wanaoaminika katika utoaji huduma, mwaka huu IMTD inawaleta watoa huduma kutoka hospitali kubwa za India ambazo ni Fortis na Medanta,” alisema. Aliz

Lowassa: Siungi mkono Kilimo Kwanza

Aliyewahi kuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa ASEMA HATA CCM INAJUA MSIMAMO WAKE, WAZIRI KABAKA ASISITIZA KILIMO NI LAZIMA, PROFESA LIPUMBA, MBATIA WAMSHANGAA   WAKATI Serikali ikielekeza nguvu nyingi kutekeleza mkakati wa kuendeleza sekta ya kilimo nchini uliopewa jina la Kilimo Kwanza, aliyewahi kuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa ameibuka na kusema haungi mkono mkakati huo.Alisema mkakati huo wa Kilimo Kwanza umekosa mashiko hivyo ili auunge mkono, kuna haja ya kubadili dhana yake na kuwa, elimu kabla ya kilimo kwanza. “Ni vyema nikaeleweka hapa. Ninachomaanisha ni kuongeza elimu katika Kilimo Kwanza ili wananchi wawe na elimu kwanza ndipo waweze kuboresha kilimo,” alisema Lowassa. Akizungumza katika Kipindi cha Dakika 45 kilichorushwa na Kituo cha Televisheni cha ITV juzi usiku, Lowassa alisema pamoja na Serikali kuwa na nia nzuri ya kumkomboa mwananchi kwa kuboresha mazingira ya kilimo, jambo hilo litakuwa si chochote kama hatapatiwa elimu itakayomwongoza

VANESSA MDEE ALIPAKA MATOPE JARIDA LA BAABKUBWA

Mtangazaji wa MTV Base na Choice FM 102.6 ya Tanzania, Vanessa Mdee, jana aligeuka mbogo baada ya kile kinachoonekana kama kukerwa na jarida la burudani la Baabkubwa. Vanessa analishutumu jarida hilo kwa kuandika habari za uongo, kuchafua majina ya watu, Kiingereza kibovu miongoni mwa mambo mengine. Alitweet: Can’t stand BabKubwa – lies,defamation,horrible grammar, tacky production and print, chipped nail polish and busted weaves … — Vanessa Mdee (@VanessaMdee) August 28, 2012 Vannesa ambaye pia ni mwanaharakati wa masuala ya HIV/AIDS, alimalizia kwa kuweka nukuu isemayo, A country is only as informed as its media. Surely this can’t be life. # ImDone — Vanessa Mdee (@VanessaMdee) August 28, 2012 Hatujaweza kufahamu ni habari gani mbaya waliyoiandika watu wa Baabkubwa kuhusu mrembo huyo

MPAKA SASA WATU WAWILI WAMETHIBITISHA KUWA WALITUMWA NA T.I.D ILI WAMUUE ALLY KIBA

TID Jana kumevuma habari kuwa mwanamuziki wa Bongo Flava Khalid Mohamed aka Top In Dar, anashikiliwa na polisi baada ya kushutumiwa kuwa alipanga njama za kumuua msanii mwenzie Ali Kiba. Leo kupitia XXL ya Clouds FM, meneja wa Ali Kiba amezungumza kutoa ufafanuzi kuhusu taarifa hizo. Ali Kiba Anasema ni kweli walipata ujumbe unaosema kuwa kuna watu waliokuwa wametumwa kwenda kumuua  Ali Kiba. "Baada sasa ya taarifa hizo  kuifikia familia, iliamua kulipoti jambo hilo polisi, polisi walifika eneo lile na kulikuwa kuna watu wawili, mwanaume na mwanamke ambao walifika maeneo jirani na pale Ali Kiba anaishi wakawa wameweka kambi pale kwa muda wakijaribu kuchunguza hili na lile.   Sasa baada ya watu wa karibu kuwaona na kutowatambua vizuri waliamua kuwafuatlia na kuwaweka chini baada ya kuwakamata.  Walipowahoji vizuri wakasema kwamba ni kweli wao wametumwa kuja kufanya jambo hlo hapo kwa Ali Kiba na wao sio wenyeji wa Dar es Salaa

HII NDO BARUA YA MGOMO WA WATANGAZAJI WA SUNRISE RADIO ARUSHA

Watangazaji wa kituo cha radio cha Sunrise cha jijini Arusha wamegoma kufanya kazi kutokana na uongozi wa kituo hicho kushindwa kuwatimizia matakwa yao ikiwa pamoja na kulipwa ujira mdogo na wengine kufanya kazi bila kupewa mikataba. Hii ni barua waliyoiandika : Ndugu wanahabari sisi baadhi ya wafanyakazi wa Sunrise Radio Arusha kuanzia tarehe 22/8/2012 tumeamua kugoma kuendelea kufanya kazi na Aspire Media Company Limited ambao ndio wamiliki wa Sunrise Radio 94.8 FM Arusha baada ya kushindwa kutimiziwa mambo kadha wa kadha tuliyokuwa tunayahitaji. Mgomo huu ulianza kama mgomo baridi mnamo tarehe 10/8/2012 baada ya sherehe za wakulima nane nane na hii ni baada ya kutokea tofauti kati ya mkurugenzi wa ufundi wa Sunrise Radio ndugu Dionis Idowa Sikutegemea Moyo na kamati ya sherehe za wakulima nane nane mwaka 2012 ambao ndiyo waliokuwa na jukumu ya kurusha matangazo ya moja kwa moja yaani live kutoka katika viwanja vya taso nane nane Nji

Serikali bado inayo fursa kurekebisha kasoro za Sensa

KATIKA hali isiyotegemewa, zoezi la Sensa ya watu na Makazi iliyoanza juzi nchini kote, imekumbana na kasoro na vikwazo mbalimbali, huku tatizo kubwa likiwa ni uhaba wa vifaa na wenyeviti wa mitaa kugoma kuwaongoza makarani kuendesha zoezi hilo kwa madai ya kutolipwa posho.   Mbali na tatizo la baadhi ya wananchi kugoma kuhesabiwa ambalo tayari linafahamika kwa mamlaka za kiserikali, uchunguzi wa gazeti hili uliofanyika katika mikoa mbalimbali pia umegundua kwamba kasoro nyingine zinazolikabili zoezi hilo hazikutegemewa na  zilijitokeza tu mara baada ya zoezi hilo kuanza juzi.    Tunaweza kusema kwamba kasoro zilizojitokeza ni za aina mbili. Moja ni kasoro zinazoweza kuwekwa katika kundi la kasoro zilizosababishwa na mamlaka za kiserikali. Pili, ni kasoro zilizosababishwa na wananchi wenyewe, wakiwamo viongozi wa mitaa ambao walishindwa kuwahamasisha wananchi katika ngazi hizo kuhusu zoezi hilo la Sensa ya Watu na Makazi.    Pamoja na kusema kwamba mamlaka za kiserikali h

POLISI WATUMIA MABOMU KUWATAWANYA CHADEMA, MMOJA ADAIWA KUUAWA KWA RISASI,WAWILI WAJERUHIWA

Mkuu wa Operesheni Sangara-Vuguvugu la Mabadiliko (M4C) chama cha Chadema, Benson Kigaila akiwa chini ya ulinzi katika gari la polisi mara baada ya kukamatwa kwa viongozi na wanachama wa chama hicho katika eneo la Msamvu Morogoro wakati wakiwasiri msafara wa Katibu Mkuu Taifa wa Chadema na viongozi wengine kwa ajili ya mkutano wa chama hicho katika Kiwanja cha Ndege Manispaa ya Morogoro. Picha na Juma Mtanda. VURUGU kubwa zimezuka mjini Morogoro baina ya wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Polisi na kusababisha kifo cha mtu mmoja anayedaiwa kuwa mfuasi wa chama hicho cha upinzani.Tukio hilo lilisababisha taharuki kubwa katika eneo kubwa la Manispaa ya Morogoro, huku wanachama na baadhi ya viongozi wa chama hicho wakionekana kuzagaa katika maeneo mbalimbali  yakiwamo ya mjini na Hospitali ya Mkoa alikopelekwa maiti huyo na polisi kwa lengo la kupata taarifa zaidi. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Faustine Shillogile alithibitisha kutokea kwa

Binadamu wa kwanza kufika mwezini afariki kwa ugonjwa wa moyo

NAIL Armstrong linaweza lisiwe jina maarufu enzi hizi, lakini hilo ndilo jina lililoshika chati mwishoni mwa miaka ya 1960 kwani alikuwa binadamu wa kwanza kukanyaga mwezini.Hata hivyo gwiji huyo wa mambo ya anga , amefariki akiwa na umri wa miaka 82 akiacha rekodi yake hiyo iliyotikisa dunia. Neil Armstrong alitua mwezini Julai  20, 1969 akiwa katika chombo kilichoitwa Apollo na kusema ''hiyo ilikuwa hatua ndogo ya binadamu, lakini mapinduzi makubwa kwa ubinadamu''. Armstrong na mwanaanga mwenzake Buzz Aldrin walitumia saa mbili na nusu wakitembea juu ya mwezi .  Neil Armstrong na wanaanga wenzake watatu Novemba mwaka 2011, walitunukiwa tuzo ya Congressional Gold Medal ambayo ndiyo ya juu zaidi inayotolewa kwa raia nchini Marekani.  Armstrong amefariki  dunia jana katika hospitali ya Columbus jimboni Ohio ambako alifanyiwa upasuaji wa moyo mapema mwezi huu. Kulingana na wasifu wa Armstrong ambao umechapishwa na Shirika la Anga la Marekani, NASA, mwanaa

Wengi wajitokeza Sensa ya Watu na Makazi

SENSA ya Watu na Makazi imeanza jana nchi nzima, huku kukiripotiwa matukio kadhaa ambayo yamesababisha baadhi ya watu kushindwa kuhesabiwa ikiwamo ukosefu wa vifaa katika baadhi ya mikoa, makarani kukosa ushirikiano kutoka kwa mabalozi ambao wamegoma kwa madai ya kuwa hawakushirikishwa tangu awali. Habari kutoka sehemu mbalimbali nchini zinaeleza kuwa baadhi ya wananchi waligoma kuhesabiwa na kutokana na matukio hayo, watu wanne wanashikiliwa na polisi Dar es Salaam kwa madai ya kusambaza vipeperushi kuzuia watu wagome kuhesabiwa. Dar es Salaam Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadick alimweleza Rais Jakaya Kikwete jana kuwa waliwakamata watu wanne wakiwatuhumu kusambaza vipeperushi vya kuzuia watu wasihesabiwe. Alisema mmoja wao ni mwanafunzi wa chuo kikuu. “Katika eneo la Mbagala, Mbande kulikuwa na msikiti mmoja ambao baadhi ya waumini wa dini ya Kiislamu walikuwa wamejifungia ili wasihesabiwe. Nimewaagiza polisi wawaache ili tuone mwisho wao, naamini nao wat

BURUNDI KUSHIRIKI MAISHA PLUS 2012.

Masoud Kipanya   Habari kutoka Bujumbura zinasema nchi hiyo inatarajiwa kutuma wawakilishi wake wawili kuingia katika shindano la Maisha Plus 2012. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mtangazaji wa Radio Puplique Africaine, Aisha Amuri Ndimubandi ambaye ndiye mratibu wa zoezi hilo alisema "Maandalizi yote yako ta yari, tunachosubiri ni fomu tu kutoka Tanzania ili tuanze zoezi la usaili". Akifafanua zaidi alisema anaamini hiyo itakuwa ni moja kati ya nafasi adimu sana kwa nchi yao ambayo ina makabila makubwa mawili yaliyowahi kuwa hasimu kujifunza namna ambavyo watanzania wameweza kuishi kama ndugu licha ya uwepo wa makabila zaidi ya 120. Burundi inakuwa nchi ya kwanza kufungua mwelekeo wa Maisha Plus kuingia katika ukanda wa Afrika ya mashariki ambapo mwakani, nchi karibu zote nne zinatarajiwa kuleta washiriki wake na kulifanya kuwa ni shindano la kwanza kutoka Tanzania lenye hadhi ya kimataifa. Mshindi wa Maisha Plus 2012 anatarajiwa kuondoka

USAILI WA MAISHA PLUS UNAANZA LEO!

USAILI WA MAISHA PLUS UNAANZA LEO! Masoud Kipanya   Kama uko eneo la bagamoyo na vitongoji vyake, nafasi ndo hii. Katika misimu iliyopita tuliruhusu washiriki wa bagamoyo kuja Dar kwa usaili, na safari hii, walio dar wanaweza kuruka bagamoyo ingawa usaili wa Dar utakuwepo muda wake utakapofika. Ukifika unapewa fomu, safari hii usaili ni 'FREE STYLE' kwa maana ya kwamba tukifika sokoni tunapiga kazi, tukifika uwanjani tunapiga kazi na hata mtaani tunapiga kazi. Njoo sokoni karibu na kituo cha mabasi. Lushoto, kesho tunakuja kesho 28/08/2012

ANGALIA NA DOWNLOAD VIDIO MPYA YA ERICK IVYOIVYO ft PICO

Akipiga stor na blog hii leo asubuhi Msanii uyo wa vichekesho alifunguka kua mimi naweza ndiomaana nimeamua kufanya na muziki na wimbo huu nimemshilikisha msanii maarufu wa muda mrefu kwenye muziki wa kizazi kipya hapa nchini PICO ailie wahi kutamba na wimbo wa Kikongwe kaka ni Bonge la ngoma nimeifanyia hapa jijijni TANGA kwa producer J.B pale Elyz, rec, na video nimefanya na production ya YOSSO PICTURES kule jijini dar,eslamu

HAPPY BIRTHDAY! Ahmed Khatib Wawoooooooooo!!

  Happy birthday jembe Mwezi.mungu akupe umri   na afya njema!   Happy Birthday Wawoooooooooo!!

BONDIA MANENO OSWARD AMTWANGA RASHIDI MATUMLA KWA POINT

MANENO OSWARD AKIJARIBU KUTUPIANA NGUMI ZA MABISHANO NA RASHIDI MATUMLA YANI NIPE NIKUPE MPAKA MWISHO WA MCHEZO MANENO ALIBUKA MSHINDI KWA POINT Bondia Rashidi Matumla kushoto akioneshana umwamba wa kutupa masumbwi na Maneno Osward wakati wa mpambano wao uliofanyika jana katika ukumbi wa Dar live Maneno alishinda kwa point Bondia Rashidi Matumla kushoto akioneshana umwamba wa kutupa masumbwi na Maneno Osward wakati wa mpambano wao uliofanyika jana katika ukumbi wa Dar live Maneno alishinda kwa point.

WAISLAM WATAKIWA KUSHIKA MAFUNDISHO YA DINI

Na Stephano Mango, Songea WAISLAM nchini wametakiwa kuhakikisha kuwa wanauendeleza uadilifu na mafundisho ya dini hiyo ili kudumisha amani na usalama wa watanzania na majirani zao hapa duniani ili kuweza kujenga jamii iliyo bora kiroho na kimwili. Maombi hayo yalikuwa ni sehemu ya Ibada ya swala ya Idd el fitr iliyofanyika katika Msikiti wa mkoa wa Ruvuma uliopo mjini Songea iliyohudhuriwa na maelfu ya waumini wa Dini hiyo wakiongozwa na mufti wa Tanzania Sheikh Issa Shaaban bin Simba na Mgeni Rasmi kitaifa Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwambungu. Immam wa Msikiti huo, Sheikh Shaaban Mbaya katika maombi maalum ya kuliombea taifa na viongozi wake wapate afya njema na uwezo wa kuwatumikia watanzania ili wawe na amani, alisema kuwa waumini wa kiislamu hawatakiwi hata kidogo kumbagua muislam au asiye kuwa muislam katika maisha yao ya kila siku. Alisema, mafundisho ya dini hiyo yana sisitiza upendo na amani ili kuenzi uumbaji wa mwenyezi Mungu, ambaye ni mwingi