
May ya
mwaka huu kulisikika habari za kuibiwa kwa gari la mwimbaji wa Taarabu
Malkia Khadija Kopa ambalo lilikuwa aina ya Noah lililokuwa limelazwa
sehemu ya kupaki magari kwa kulipia. Gari hilo lililoibiwa maeneo ya
Mwananyamala pamoja na magari mengine liliweza kukamatwa mjini Moshi
likiwa limepakiwa nyumbani kwa mtu huku likiwa limeng'olewa rim zote
huku likiwa limewekwa rehani na mtu ambaye alilinunua gari hilo, taarifa
zaidi
zinadai kuwa jambazi aliekamatwa na kuhusika na wizi
huo anafahamika kwa jina la Ringo na anashikiliwa na polisi pia akiwa
amekamatwa na magari mengine matatu.