Skip to main content

HII NDO BARUA YA MGOMO WA WATANGAZAJI WA SUNRISE RADIO ARUSHA


Watangazaji wa kituo cha radio cha Sunrise cha jijini Arusha wamegoma kufanya kazi kutokana na uongozi wa kituo hicho kushindwa kuwatimizia matakwa yao ikiwa pamoja na kulipwa ujira mdogo na wengine kufanya kazi bila kupewa mikataba.

Hii ni barua waliyoiandika:

Ndugu wanahabari sisi baadhi ya wafanyakazi wa Sunrise Radio Arusha kuanzia tarehe 22/8/2012 tumeamua kugoma kuendelea kufanya kazi na Aspire Media Company Limited ambao ndio wamiliki wa Sunrise Radio 94.8 FM Arusha baada ya kushindwa kutimiziwa mambo kadha wa kadha tuliyokuwa tunayahitaji.

Mgomo huu ulianza kama mgomo baridi mnamo tarehe 10/8/2012 baada ya sherehe za wakulima nane nane na hii ni baada ya kutokea tofauti kati ya mkurugenzi wa ufundi wa Sunrise Radio ndugu Dionis Idowa Sikutegemea Moyo na kamati ya sherehe za wakulima nane nane mwaka 2012 ambao ndiyo waliokuwa na jukumu ya kurusha matangazo ya moja kwa moja yaani live kutoka katika viwanja vya taso nane nane Njiro.

Ndugu wanahabari mgomo huu umesababishwa pia na kutofanyiwa kazi kwa madai ya wafanyakazi, wafanyakazi tumekua tukifanya kazi katika mazingira magumu kwani:-

a) Tunalipwa mishahara midogo isiyokidhi mahitaji (mshahara wa 100,000 na wengine 170,000)

b) Kufanyishwa kazi bila kuwa na mikataba, tukidai mikataba tunapigwa tarehe

c) Kutokatwa makato kwenye mishahara kwaajili ya pensheni

d) Baadhi ya wafanyakazi kufanyishwa kazi bila kulipwa
e) Hakuna overtime payment

f) Wafanyakazi kutishiwa kufukuzwa mara kwa mara pale wanapodai haki zao

g) Hakuna likizo

h) Waandishi wa habari walioripoti live ya uchaguzi wa Arumeru Mashariki tarehe 1/4/2012 kutolipwa posho zao hadi leo na wengine walidai na hatimaye wakafukuzwa kazi

i) Mishahara wa wafanyakazi kucheleweshwa kulipwa kwani utakuta mshahara wa mwezi huu tunaweza kulipwa mwezi ujao katikati au mwishoni
j) Mkurugenzi wa ufundi kutishia kumfukuza kazi mhasibu kwa maslahi yake binafsi

k) Wafanyakazi wanaofanya vipindi vya usiku kutopewa usafiri wakati wa kwenda na kurudi kitu ambacho kinamlazimisha mtangazaji kulala studio kwa lazima

l) Gari la ofisi kutotumika kwa mahitaji ya ofisi bali kwa maslahi ya mkurugenzi wa ufundi

m) Mishahara ya mwezi July ya baadhi ya wafanyakazi kuzuiliwa kuanzia tarehe 1/8/2012 hadi leo hii tarehe 22/8/2012 kwa sababu zisizo za msingi
Ndugu wanahabari, kwa madai hayo hapo juu sisi wafanyakazi wa sunrise radio hatupo tayari kurudi kazini mpaka pale mkurugenzi wa ufundi ndugu Dionis Idowa Sikutegemea Moyo atakapojiuzulu nafasi yake na madai ya wafanyakazi yatakapokua yametatuliwa.

Dionis Idowa
Tunaipenda sana Sunrise Radio bila kuwasahau wasikilizaji wetu pia tunawapenda sana ila tumeona ni vyema kuyaweka bayana haya yote ili mtuelewe na pia ni majibu ya baadhi ya maswali mliyokuwa mnatuuliza wasikilizaji wetu wapendwa.

NDUGU WANAHABARI WAFANYAKAZI WA SUNRISE RADIO WALIOGOMA KUFANYA KAZI IDADI YAO NI KUMI NA WAWILI (12) WAKIWEMO

a) WATANGAZAJI 4
b) MARIPOTA 2
c) WATU WA MASOKO 3
d) WAZALISHAJI WA VIPINDI 2 NA
e) MHASIBU 1
WAFANYAKAZI HAO WAMEGOMA KUTOKANA NA MADAI YAO HAPO JUU PAMOJA NA MADAI MENGINE MENGI AMBAYO HAYAJAORODHESHWA
MAJINA YA WAFANYAKAZI WALIOGOMA NI HAYA YAFUATAYO

1. SEVERINUS MWIJAGE Jr – MTANGAZAJI
2. BEATRICE GERALD NANGAWE – MTANGAZAJI
3. EMMANUE MWAKALUKWA – MTANGAZAJI
4. JALACK ALLY – MTANGAZAJI
5. HAMIS ABTWAY (DJ HAAZU) – MTANGAZAJI, MZALISHA VIPINDI NA DJ
6. BERTHA ISMAIL – RIPOTA
7. ONESMO LOY – RIPOTA
8. JOSEPH AMANI – MZALISHAJI WA VIPINDI
9. ALLY CHARO – MENEJA WA MASOKO
10. RODGERS I. NELSON – MHASIBU
11. WITNESS RAYMOND – MASOKO
12. HAPPYNESS ALPHONCE – MASOKO

ASANTENI SANA KWA KUTUSIKILIZA

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

Coastal ipo tayari kuanza ligi kuu, yashinda 3-0 ikiwa kambini Moshi.

Wachezaji wa Coastal Union wakifanya mazoezi mepesi muda mfupi kabla ya kukabiliana na Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini Moshi, anayeonekana pichani mwenye jezi namba 17 ni haruna Moshi 'Boban'. Mtokeo ya mechi hiyo ni ushindi wa 3-0 kwa Wagosi. Mazoezi yamekolea, uwanja wa Ushirika Moshi. Uhuru Suleiman amesifiwa na kocha kuwa ni kiungo mwenye kasi nyingi na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira. Mshambuliaji anayetumia mguu wa kushoto kutoka Uganda, Yayo Lutimba Kato amefunga bao lake la kwanza tangu kujiunga na Coastal Union ambayo imeweka kambi mjini Moshi tangu jana. Kato ambaye ametoka URA inayoshiriki ligi kuu nchini Uganda, alipatia timu yake bao la kuongoza dhidi ya Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini humo, bao hilo alilifunga kwa ufundi mkubwa katika kipindi cha pili baada ya kupokea pasi murua na kupiga shuti kali akiwa nje ya 18. Akitoa taarifa kutoka Moshi, mwenyekiti wa Wagosi Hemed Hilal ‘Aurora’ amesema “Katika dakika za lal...

Tuhuma nzito : Magufuli, Mwakyembe, Lukuvi kufikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge

Dk John Magufuli   Dar es Salaam.   Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imesema itawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akiwatuhumu kwa kulidanganya Bunge. Hatua hiyo ilitangazwa jana na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe baada ya kumhoji Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert Mrango kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka wa fedha 2011/2012. Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo kiasi cha Sh348,075,000,000 fedha za ndani zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililotajwa kuwa ni la mradi maalumu (Special Road Construction Project) hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni. “Ni vizuri leo uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. T...