Skip to main content

HII NDO BARUA YA MGOMO WA WATANGAZAJI WA SUNRISE RADIO ARUSHA


Watangazaji wa kituo cha radio cha Sunrise cha jijini Arusha wamegoma kufanya kazi kutokana na uongozi wa kituo hicho kushindwa kuwatimizia matakwa yao ikiwa pamoja na kulipwa ujira mdogo na wengine kufanya kazi bila kupewa mikataba.

Hii ni barua waliyoiandika:

Ndugu wanahabari sisi baadhi ya wafanyakazi wa Sunrise Radio Arusha kuanzia tarehe 22/8/2012 tumeamua kugoma kuendelea kufanya kazi na Aspire Media Company Limited ambao ndio wamiliki wa Sunrise Radio 94.8 FM Arusha baada ya kushindwa kutimiziwa mambo kadha wa kadha tuliyokuwa tunayahitaji.

Mgomo huu ulianza kama mgomo baridi mnamo tarehe 10/8/2012 baada ya sherehe za wakulima nane nane na hii ni baada ya kutokea tofauti kati ya mkurugenzi wa ufundi wa Sunrise Radio ndugu Dionis Idowa Sikutegemea Moyo na kamati ya sherehe za wakulima nane nane mwaka 2012 ambao ndiyo waliokuwa na jukumu ya kurusha matangazo ya moja kwa moja yaani live kutoka katika viwanja vya taso nane nane Njiro.

Ndugu wanahabari mgomo huu umesababishwa pia na kutofanyiwa kazi kwa madai ya wafanyakazi, wafanyakazi tumekua tukifanya kazi katika mazingira magumu kwani:-

a) Tunalipwa mishahara midogo isiyokidhi mahitaji (mshahara wa 100,000 na wengine 170,000)

b) Kufanyishwa kazi bila kuwa na mikataba, tukidai mikataba tunapigwa tarehe

c) Kutokatwa makato kwenye mishahara kwaajili ya pensheni

d) Baadhi ya wafanyakazi kufanyishwa kazi bila kulipwa
e) Hakuna overtime payment

f) Wafanyakazi kutishiwa kufukuzwa mara kwa mara pale wanapodai haki zao

g) Hakuna likizo

h) Waandishi wa habari walioripoti live ya uchaguzi wa Arumeru Mashariki tarehe 1/4/2012 kutolipwa posho zao hadi leo na wengine walidai na hatimaye wakafukuzwa kazi

i) Mishahara wa wafanyakazi kucheleweshwa kulipwa kwani utakuta mshahara wa mwezi huu tunaweza kulipwa mwezi ujao katikati au mwishoni
j) Mkurugenzi wa ufundi kutishia kumfukuza kazi mhasibu kwa maslahi yake binafsi

k) Wafanyakazi wanaofanya vipindi vya usiku kutopewa usafiri wakati wa kwenda na kurudi kitu ambacho kinamlazimisha mtangazaji kulala studio kwa lazima

l) Gari la ofisi kutotumika kwa mahitaji ya ofisi bali kwa maslahi ya mkurugenzi wa ufundi

m) Mishahara ya mwezi July ya baadhi ya wafanyakazi kuzuiliwa kuanzia tarehe 1/8/2012 hadi leo hii tarehe 22/8/2012 kwa sababu zisizo za msingi
Ndugu wanahabari, kwa madai hayo hapo juu sisi wafanyakazi wa sunrise radio hatupo tayari kurudi kazini mpaka pale mkurugenzi wa ufundi ndugu Dionis Idowa Sikutegemea Moyo atakapojiuzulu nafasi yake na madai ya wafanyakazi yatakapokua yametatuliwa.

Dionis Idowa
Tunaipenda sana Sunrise Radio bila kuwasahau wasikilizaji wetu pia tunawapenda sana ila tumeona ni vyema kuyaweka bayana haya yote ili mtuelewe na pia ni majibu ya baadhi ya maswali mliyokuwa mnatuuliza wasikilizaji wetu wapendwa.

NDUGU WANAHABARI WAFANYAKAZI WA SUNRISE RADIO WALIOGOMA KUFANYA KAZI IDADI YAO NI KUMI NA WAWILI (12) WAKIWEMO

a) WATANGAZAJI 4
b) MARIPOTA 2
c) WATU WA MASOKO 3
d) WAZALISHAJI WA VIPINDI 2 NA
e) MHASIBU 1
WAFANYAKAZI HAO WAMEGOMA KUTOKANA NA MADAI YAO HAPO JUU PAMOJA NA MADAI MENGINE MENGI AMBAYO HAYAJAORODHESHWA
MAJINA YA WAFANYAKAZI WALIOGOMA NI HAYA YAFUATAYO

1. SEVERINUS MWIJAGE Jr – MTANGAZAJI
2. BEATRICE GERALD NANGAWE – MTANGAZAJI
3. EMMANUE MWAKALUKWA – MTANGAZAJI
4. JALACK ALLY – MTANGAZAJI
5. HAMIS ABTWAY (DJ HAAZU) – MTANGAZAJI, MZALISHA VIPINDI NA DJ
6. BERTHA ISMAIL – RIPOTA
7. ONESMO LOY – RIPOTA
8. JOSEPH AMANI – MZALISHAJI WA VIPINDI
9. ALLY CHARO – MENEJA WA MASOKO
10. RODGERS I. NELSON – MHASIBU
11. WITNESS RAYMOND – MASOKO
12. HAPPYNESS ALPHONCE – MASOKO

ASANTENI SANA KWA KUTUSIKILIZA

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

MAJINA YA WASHIRIKI NA WA WEZESHAJI WA FILM YA HOUSE GIRL!

CAST SELEMANI MOHAMED / BUNTO ANDREW / C-O YORAM MWETA / MGANGA MWANTUMU / MKE WA C-O JOHN / MCHUNGAJI BI FURURATU / JINI WAOMBOLEZAJI SAUMU HUSENI HASHIMU BABA RASTA MAN YOHANNA TAMILWAI SAIDI MWALUBADU SEMY STIR SELEMANI MOHAMEDI  AND ANDREW C-O LOCATION ATHUMANI HAMADI MAKE UP MWASHAMBA RAMADHANI BEDUI DEREVA DAUDI SPOONSER SAIDI SHABANI AND THE FRESH2012 GLOB SOUND PRODUCER J-B LIGHT YOHANNA TAMILWAI THENK YOU THE FRESH ENERTAINMENT AND THE FRESH2012 BLOG CONTACTS 0653785027 +255714091786 ZAIDI TEMBELEA www.the-fresh.blogspot.com ADRESS Thefresh@ymail.com AU Saidshabani60@gmai.com

Video: Blackchild – Put Inside

David Abdulichel, also known as BlackChild is a Ghanaian from Asanti origin, born and raised in Lagos Nigeria. BlackChild, who is a recording artist, song writer and performer started his music career back in 2000 and since then has released four singles. He has also worked with top producers in Nigeria such as Fliptyce, Spanky, Meca E & BrainMix to mention but few. BlackChild Abdul rose to prominence with his hit songs “Treasure”, “Ele” featuring Rock Steady, “Could It Be Love” featuring Cartiar, “All I Need” featuring Solid Star. This time around he comes out with “Put Inside” which sees him delivering lines in french and his native language and is steadily generating buzz and enjoying airplay on radio stations within and outside Lagos. Listen up!