Skip to main content

Kutana na watoto wahubiri. Je ni sawa?


Mamake Ezekiel na babake wa kambo ni wachungaji wa kanisa la 'Fullness of time' huko Maryland kanisa ambalo walilianza miaka mbili iliyopita.Ni katika kanisa hili ambapo hezekaiah alitawazwa kuwa mchungaji na ndugu yake shemasi mapema mwaka huu.
'Ulikuwa wakati wa ajabu kwangu' alisema Hezekiah nduguye Ezekiel mwenye umri wa miaka 13.'Kila mtu kanisani alitupigia makofi kwa furaha na kutupongeza'
Micah, nduguye Hezekiah ana mumri wa miaka saba na tayari anataka kufuata nyayo zake hezekaih 'Tayari nimetayarisha mahubiri lakini nitayahubiri nitakapo hitimu miaka 10' alisema Micah kwa sauti ya unyenyekevu.
Sio nchi ya marekani tu ambayo ina watoto wanaohubiri, bali Brazil pia imeboboea katika jambo hili.Indonesia pia haijawachwa nyuma kwani ina kipindi cha runinga ambacho wahubiri wachanga wa dini ya kiislamu hishindana. ini se
'Jambo hili lina uwezo wa kuchipuka haswa katika dini ambazo husisistiza uwepo ya roho mtakatifu na pia jamii zilizotengwa' asema Edith Blumhofer mtaalam wa historia ya wakristo chuo cha Wheaten mjini Illinois.
Ted Lavigne kasisi aliye staafu na anaandika kitabu kilicho na mada hii ya watoto wahuburi,asema kuwa wahubiri wengi watoto walisikika sana miaka ya 1920 na 1930 wakati ambapo kanisa la pentekoste lilikuwa changa.

Fasihi za awali zinaelezea wakati huu ambapo watoto walisikika wakinena maneno yenye hekima kuliko miaka yao.Jambo hili lilipokelewa kwani lilikuwa thibitisho la uwepo wa Roho Mtakatifu.
Jambo la kushangaza ni kwamba,jinsi makanisa haya yalipoendelea kuwatumia watotohawa ndivyo waliendelea kuonekana wamejitenga.

Lavigne amegundua takriban mifano 500 tangu miaka ya 1500 na 1700 ya watoto hawa,wengi wao wakiwa na asili ya marekani na wengine uingereza.

'Kuna elimu ya nguvu ya kidini inayoendelea hapa nchini.Hapa Amerika kuna watu wanaopeda dini sana' asem Randall Balmer mwenyekiti wa kitengo cha dini chuo cha Dartmouth.
Waumini kanisani

Kanuni zinazosema nani anayeweza kuanzisha kanisa zina posho kubwa kwa hivyo mtu yeyote anaweza kuanzisha kanisa mahali popote.Kanisa la familia ya Ezekiel ni kanisa ambalo halifuati madhehebu yoyote kwa hivyo wana uhuru wa kufanya mambo yao vyovyote.
Hata hiyo si vigumu kupata watu walio na wasiwasi kuhusu watoto wahubiri.Watu kama hawa huwa na dhana kuwa ni wachanga sana kuapishwa kama kasisi na wana ushahidi wa kesi za watoto wahubiri waliopotoka.
Ushahidi mkubwa haswa ni ule wa Marjoe Gortner,mtoto mhubiri aliyetangaza baada ya miaka mingi kuwa hakuamini kuwa kuna Mungu na alikuwa mhubiri kwa shinikizo ya wazazi wake na baadaye kama ajira.
Wazazi wa Ezekiel wanafahamu fika mambo haya na wako tayari kumtetea mtoto wao.Mamake asema kuwa watoto wake wana adabu na tabia nzuri.Maisha ya watoto wao ina uwianao,kwani hata ingawa ni wahubiri wao kufanya vitu ambavyo watoto wa kawaida hufanya kama kwenda shule,kucheza na watoto wengine na kadhalika.
Hata hivyo watoto hawa hukumbwa na changamoto nyingi kwa sababu ya majukumu yao ya kuhubiri.Kwa mfano ,wao hufanya masomo nyumbani kwa vile wakienda shuleni hutaniwa wenzao.
Ezekiel bado hajaamua kazi atakayoifanya maishani. Hajaamua kama atakuwa mhubiri maisha yake yote ama ataifanya kazi ingine.
Siku hizi watoto wanao hubiri ni wachache nchini amerikani na amabao wako,huhubiri kwenye mitaani.

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

Coastal ipo tayari kuanza ligi kuu, yashinda 3-0 ikiwa kambini Moshi.

Wachezaji wa Coastal Union wakifanya mazoezi mepesi muda mfupi kabla ya kukabiliana na Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini Moshi, anayeonekana pichani mwenye jezi namba 17 ni haruna Moshi 'Boban'. Mtokeo ya mechi hiyo ni ushindi wa 3-0 kwa Wagosi. Mazoezi yamekolea, uwanja wa Ushirika Moshi. Uhuru Suleiman amesifiwa na kocha kuwa ni kiungo mwenye kasi nyingi na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira. Mshambuliaji anayetumia mguu wa kushoto kutoka Uganda, Yayo Lutimba Kato amefunga bao lake la kwanza tangu kujiunga na Coastal Union ambayo imeweka kambi mjini Moshi tangu jana. Kato ambaye ametoka URA inayoshiriki ligi kuu nchini Uganda, alipatia timu yake bao la kuongoza dhidi ya Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini humo, bao hilo alilifunga kwa ufundi mkubwa katika kipindi cha pili baada ya kupokea pasi murua na kupiga shuti kali akiwa nje ya 18. Akitoa taarifa kutoka Moshi, mwenyekiti wa Wagosi Hemed Hilal ‘Aurora’ amesema “Katika dakika za lal...

Tuhuma nzito : Magufuli, Mwakyembe, Lukuvi kufikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge

Dk John Magufuli   Dar es Salaam.   Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imesema itawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akiwatuhumu kwa kulidanganya Bunge. Hatua hiyo ilitangazwa jana na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe baada ya kumhoji Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert Mrango kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka wa fedha 2011/2012. Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo kiasi cha Sh348,075,000,000 fedha za ndani zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililotajwa kuwa ni la mradi maalumu (Special Road Construction Project) hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni. “Ni vizuri leo uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. T...