Skip to main content

Madaktari 50 toka India kutua nchini kesho




JOPO la madaktari 50 kutoka nchini India, wanatarajia kufanya maonesho ya matibabu katika ukumbi wa Diamond Jubilee Agosti 30 hadi 31, mwaka huu, kuanzia saa nne asubuhi hadi 11 jioni.


Taarifa iliyotolewa kwa waandishi wa habari Dar es Salaam jana na Balozi wa India nchini, Bw. Debnath Shaw, ilisema maonesho hayo yameandaliwa na Taasisi ya Shirikisho la Biashara nchini India la Medical Tourism Destination (IMTD).

Aliwaomba watu wenye matatizo mbalimbali ya kiafya wajitokeze katika maonesho hayo ili waweze kupata huduma ya matibabu ambayo itatolewa katika ukumbi huo kwa gharama za chini.

“Gharama zao zitakuwa za chini na zitamwezesha kila mwananchi mwenye matatizo ya kiafya kuzimudu na kupata huduma, India inaongoza duniani kwa kutoa huduma bora za tiba.

“Nchi yetu pia ina madaktari bingwa wanaoaminika katika utoaji huduma, mwaka huu IMTD inawaleta watoa huduma kutoka hospitali kubwa za India ambazo ni Fortis na Medanta,” alisema.

Alizitaja hospitali nyingine kuwa ni Asian Heart, Seven Hills, SRM Hospital, Vasan Eye Care na Idara ya Aayush ili kuja kuwasaidia wagonjwa waliopo nchini.

Alisema maonesho hayo pia yamelenga kutoa fursa ya wataalamu wa sekta hiyo kufahamiana wakiwemo wasomi na wadau ili kuweka jukwaa kwa mashirika na taasisi kati ya India na Tanzania waweze kushirikiana kuimarisha huduma ya afya.

Alisema watakuwepo wawakilishi kutoka hospitali na vituo vya afya vilivyopo nchini humo kikiwemo kitengo cha upasuaji, hospitali za macho, ortho care, bidhaa za afya, huduma za kiasili, utalii wa kiafya, kampuni za dawa na vituo vya physiotherapy.

“Zaidi ya nchi 30 duniani ikiwemo Marekani, Canada, Uingereza, Urusi, Uarabuni, Uganda, Tanzania, Sri Lanka na nchi za Bara la Asia, huwa wanakwenda India kupata matibabu,” alisema.

Bw. Shaw aliongeza kuwa, nchi hiyo pia inaongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya watalii wanaokwenda kufuata matibabu.


Habari na Salim Nyomolelo

Popular posts from this blog

Goog music from tng jojo yatakwisha hii apa

DownLoad Na Sikiliza Joint Mpya Ya Squizer Ft Belle 9 - Mtemi Pesa

MAJINA YA WASHIRIKI NA WA WEZESHAJI WA FILM YA HOUSE GIRL!

CAST SELEMANI MOHAMED / BUNTO ANDREW / C-O YORAM MWETA / MGANGA MWANTUMU / MKE WA C-O JOHN / MCHUNGAJI BI FURURATU / JINI WAOMBOLEZAJI SAUMU HUSENI HASHIMU BABA RASTA MAN YOHANNA TAMILWAI SAIDI MWALUBADU SEMY STIR SELEMANI MOHAMEDI  AND ANDREW C-O LOCATION ATHUMANI HAMADI MAKE UP MWASHAMBA RAMADHANI BEDUI DEREVA DAUDI SPOONSER SAIDI SHABANI AND THE FRESH2012 GLOB SOUND PRODUCER J-B LIGHT YOHANNA TAMILWAI THENK YOU THE FRESH ENERTAINMENT AND THE FRESH2012 BLOG CONTACTS 0653785027 +255714091786 ZAIDI TEMBELEA www.the-fresh.blogspot.com ADRESS Thefresh@ymail.com AU Saidshabani60@gmai.com