Skip to main content

Madaktari 50 toka India kutua nchini kesho




JOPO la madaktari 50 kutoka nchini India, wanatarajia kufanya maonesho ya matibabu katika ukumbi wa Diamond Jubilee Agosti 30 hadi 31, mwaka huu, kuanzia saa nne asubuhi hadi 11 jioni.


Taarifa iliyotolewa kwa waandishi wa habari Dar es Salaam jana na Balozi wa India nchini, Bw. Debnath Shaw, ilisema maonesho hayo yameandaliwa na Taasisi ya Shirikisho la Biashara nchini India la Medical Tourism Destination (IMTD).

Aliwaomba watu wenye matatizo mbalimbali ya kiafya wajitokeze katika maonesho hayo ili waweze kupata huduma ya matibabu ambayo itatolewa katika ukumbi huo kwa gharama za chini.

“Gharama zao zitakuwa za chini na zitamwezesha kila mwananchi mwenye matatizo ya kiafya kuzimudu na kupata huduma, India inaongoza duniani kwa kutoa huduma bora za tiba.

“Nchi yetu pia ina madaktari bingwa wanaoaminika katika utoaji huduma, mwaka huu IMTD inawaleta watoa huduma kutoka hospitali kubwa za India ambazo ni Fortis na Medanta,” alisema.

Alizitaja hospitali nyingine kuwa ni Asian Heart, Seven Hills, SRM Hospital, Vasan Eye Care na Idara ya Aayush ili kuja kuwasaidia wagonjwa waliopo nchini.

Alisema maonesho hayo pia yamelenga kutoa fursa ya wataalamu wa sekta hiyo kufahamiana wakiwemo wasomi na wadau ili kuweka jukwaa kwa mashirika na taasisi kati ya India na Tanzania waweze kushirikiana kuimarisha huduma ya afya.

Alisema watakuwepo wawakilishi kutoka hospitali na vituo vya afya vilivyopo nchini humo kikiwemo kitengo cha upasuaji, hospitali za macho, ortho care, bidhaa za afya, huduma za kiasili, utalii wa kiafya, kampuni za dawa na vituo vya physiotherapy.

“Zaidi ya nchi 30 duniani ikiwemo Marekani, Canada, Uingereza, Urusi, Uarabuni, Uganda, Tanzania, Sri Lanka na nchi za Bara la Asia, huwa wanakwenda India kupata matibabu,” alisema.

Bw. Shaw aliongeza kuwa, nchi hiyo pia inaongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya watalii wanaokwenda kufuata matibabu.


Habari na Salim Nyomolelo

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

Coastal ipo tayari kuanza ligi kuu, yashinda 3-0 ikiwa kambini Moshi.

Wachezaji wa Coastal Union wakifanya mazoezi mepesi muda mfupi kabla ya kukabiliana na Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini Moshi, anayeonekana pichani mwenye jezi namba 17 ni haruna Moshi 'Boban'. Mtokeo ya mechi hiyo ni ushindi wa 3-0 kwa Wagosi. Mazoezi yamekolea, uwanja wa Ushirika Moshi. Uhuru Suleiman amesifiwa na kocha kuwa ni kiungo mwenye kasi nyingi na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira. Mshambuliaji anayetumia mguu wa kushoto kutoka Uganda, Yayo Lutimba Kato amefunga bao lake la kwanza tangu kujiunga na Coastal Union ambayo imeweka kambi mjini Moshi tangu jana. Kato ambaye ametoka URA inayoshiriki ligi kuu nchini Uganda, alipatia timu yake bao la kuongoza dhidi ya Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini humo, bao hilo alilifunga kwa ufundi mkubwa katika kipindi cha pili baada ya kupokea pasi murua na kupiga shuti kali akiwa nje ya 18. Akitoa taarifa kutoka Moshi, mwenyekiti wa Wagosi Hemed Hilal ‘Aurora’ amesema “Katika dakika za lal...

Tuhuma nzito : Magufuli, Mwakyembe, Lukuvi kufikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge

Dk John Magufuli   Dar es Salaam.   Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imesema itawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akiwatuhumu kwa kulidanganya Bunge. Hatua hiyo ilitangazwa jana na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe baada ya kumhoji Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert Mrango kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka wa fedha 2011/2012. Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo kiasi cha Sh348,075,000,000 fedha za ndani zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililotajwa kuwa ni la mradi maalumu (Special Road Construction Project) hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni. “Ni vizuri leo uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. T...