Skip to main content

VANESSA MDEE ALIPAKA MATOPE JARIDA LA BAABKUBWA


Mtangazaji wa MTV Base na Choice FM 102.6 ya Tanzania, Vanessa Mdee, jana aligeuka mbogo baada ya kile kinachoonekana kama kukerwa na jarida la burudani la Baabkubwa.

Vanessa analishutumu jarida hilo kwa kuandika habari za uongo, kuchafua majina ya watu, Kiingereza kibovu miongoni mwa mambo mengine.
Alitweet:
Can’t stand BabKubwa – lies,defamation,horrible grammar, tacky production and print, chipped nail polish and busted weaves …
— Vanessa Mdee (@VanessaMdee) August 28, 2012
Vannesa ambaye pia ni mwanaharakati wa masuala ya HIV/AIDS, alimalizia kwa kuweka nukuu isemayo,
A country is only as informed as its media. Surely this can’t be life. #ImDone
— Vanessa Mdee (@VanessaMdee) August 28, 2012
Hatujaweza kufahamu ni habari gani mbaya waliyoiandika watu wa Baabkubwa kuhusu mrembo huyo

Popular posts from this blog

Goog music from tng jojo yatakwisha hii apa

DownLoad Na Sikiliza Joint Mpya Ya Squizer Ft Belle 9 - Mtemi Pesa

Tugumiane tanga flevani 10_00AM-12_00PM 106.1Mhz @mwambaofm_ fm radio tanga