Skip to main content

MUME WA JACK PATRICK AACHIWA HURU NA KUKAMATWA TENA...

BAADA ya Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu jijini Dar kumuachia huru mume wa mwanamitindo maarufu Bongo, Jacqueline Patrick, aitwaye Abdullatif Fundikira kwa kesi ya kusafirisha madawa ya kulevya iliyokuwa inamkabili, jeshi la polisi limemkamata tena na kumrudisha lupango
 
Tukio hilo lililoshuhudiwa na mwandishi wetu lilitokea Jumatano iliyopita katika mahakama hiyo ambapo Hakimu Riyad Shamshama alimfutia mashitaka mtuhumiwa huyo na kumuachia huru kutokana na makosa yaliyofanyika wakati wa kumfungulia kesi hiyo.

Hakimu huyo aliuambia upande wa mashitaka kuwa, kama wanataka kumbadilishia mashitaka mtuhumiwa, wanatakiwa kumsubiri nje ili wamkamate na kumfungulia mashitaka upya.


Kama walivyoshauriwa, baada ya kutoka nje, polisi walimkamata Abdullatif wakati akikumbatiana na ndugu zake waliokuwa wakiamini kuwa kesi hiyo imekwisha.

Polisi walimsweka Abdullatif katika mahabusu ya mahakama hiyo ili kujiandaa kumpeleka kituoni na kisha katika ofisi ya mwendesha mashitaka mkuu kwa ajili kumfungulia kesi upya.

Hali hiyo iliwafanya baadhi ya ndugu waliokuwepo mahakamani hapo kububujikwa na machozi kwani awali walishaanza kuchekelea.

Popular posts from this blog

Goog music from tng jojo yatakwisha hii apa

DownLoad Na Sikiliza Joint Mpya Ya Squizer Ft Belle 9 - Mtemi Pesa

Tugumiane tanga flevani 10_00AM-12_00PM 106.1Mhz @mwambaofm_ fm radio tanga