Skip to main content

BURIANI SHARO MILIONEA!!!!!!!!!!!!!!!!

Gari alilokuwa akiendesha Sharomilionea linavyoonekana katika eneo la ajali.
Baadhi ya wananchi wakilitazama gari alilokuwa akiendesha Sharomilionea na kuharibika vibaya baada ya kupinduka na kumsababaishia umauti.

Wananachi wakiendelea kutazama mabaki ya gari aina ya Toyota Harrier lenye namba za usajili T 478 BVR alilokuwa akiliendesha Sharomilionea kabla halijapinduka na kumsababaishia umauti. (Picha zote: Kwa hisani ya blog ya Libeneke la Kaskazini) 
.
Hapa linavyoonekana gari alilokuwa akiendesha marehemu Sharomilionea linavyoonekana kwa nyuma.


Mbunge wa Jimbo la Muheza, Herbet Mtangi (kushoto) akiwa katika Hospitali Teule ya Muheza ulikohifadhiwa mwili wa marehmu Sharomilionea.

Hatuamini... tunataka kuhakikisha! Baadhi ya wananchi wakiwa nje ya chumba cha maiti cha Hospitali Teule ya Wilaya ya Muheza kushuhudia mwili wa marehemu Sharomilionea aliyefariki kwa ajali ya gari. 
Mbunge wa Jimbo la Muheza, Herbet Mtangi ni miongoni mwa maelfu ya watu waliomiminika katika Hospitali Teule ya Wilaya ya Muheza kushuhudia mwili wa msanii wa vichekesho na muimbaji wa muziki wa kizazi kipya, Hussein Mkietty a.k.a Sharomilionea ambaye alifariki kwenye ajali mbaya ya gari juzi usiku huku taarifa zaidi kuhusianan na kifo chake zikidai kuwa mijitu yenye roho mbaya kama ya shetani ilimkomba marehemu kila kitu alichokuwa nacho na kuuacha mwili wake ukiwa na pensi ya ndani tu maarufu kama 'boxer'.

Mbunge Mtangi aliyekuwa mmoja wa watu walioguswa sana na taarifa hizo, aliibukia kwenye viunga vya Hospitali ya Muheza na kuungana na wananchi kibao ambao nao walifika hapo kuthibitisha kama kweli msanii huyo kipenzi cha wengi ameaga dunia kwa kujeruhiwa kichwani kufuatia ajali mbaya ya kupinduka zaidi ya mara tatu kwa gari alilokuwa akiendesha na kuharibika vibaya aina ya Toyota Harrier.

Baadaye, umati wa watu ulipozidi, mhudumu wa chumba cha maiti hospitalini hapo aliyetambulika kwa jina la Mhusa na pia daktari mmoja aitwaye Kibaja walilazimika kuomba msaada wa walinzi hospitalini hapo ii kuzuia umati huo usiingie kwa wakati mmoja na kuathiri shughuli za utoaji huduma na masomo kwa wanafunzi wanaosomea udaktari.

Sharomilionea alipata ajali hiyo wakati akiwa katika Kijiji cha Mguzoni wilayani Muheza, mkoani Tanga kuelekea kwao katika Kijiji cha Lusanga, wilayani humo humo (Muheza) kwa nia ya kuwajulia hali wazazi wake.

Baada ya kupata ajali mbaya na kufariki, mijitu yenye roho ya shetani haikujishughulisha na hatua yoyote ya kuukimbizia mwili wake hospitali bali walianza kumkomba kila kitu na mwishowe kumsaula viwalo vyake na kutokomea navyo, wakimuacha na nguo ya ndani tu.

KAMPUNI YA AIRTEL
Kampuni ya huduma za simu ya Airtel ambayo hivi karibuni imkuwa ikipata mafanikio makubwa katika kutoa matangazo yake kupitia Sharomilionea, imeguswa na kifo cha msanii huyo na kutoa ujumbe maalum wa kumkumbuka.

Katika kuelezea hisia zao, Airtel wameandaa bango maalum la kumkumbuka, likiwa na picha yake yenye pozi 'tamu' na kuandika juu yake ujumbe wenye maandishi makubwa yasemayo: "Daima utakumbukwa kjwa ucheshi na upendo wako, hakuna atakayeziba pengo lako."

Katika tangazo mojawapo lililokimbiza sana la Airtel, Sharomilionea anaonekana akimtamkia kwa mbwembwe msanii mwingine, King Majuto kwa kumwambia 'Umebuugi meeen...!" , ambapo sasa msemo huo ni miongoni mwa matamshi yasiyokauka midomoni mwa vijana wengi wa mjini.

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

Coastal ipo tayari kuanza ligi kuu, yashinda 3-0 ikiwa kambini Moshi.

Wachezaji wa Coastal Union wakifanya mazoezi mepesi muda mfupi kabla ya kukabiliana na Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini Moshi, anayeonekana pichani mwenye jezi namba 17 ni haruna Moshi 'Boban'. Mtokeo ya mechi hiyo ni ushindi wa 3-0 kwa Wagosi. Mazoezi yamekolea, uwanja wa Ushirika Moshi. Uhuru Suleiman amesifiwa na kocha kuwa ni kiungo mwenye kasi nyingi na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira. Mshambuliaji anayetumia mguu wa kushoto kutoka Uganda, Yayo Lutimba Kato amefunga bao lake la kwanza tangu kujiunga na Coastal Union ambayo imeweka kambi mjini Moshi tangu jana. Kato ambaye ametoka URA inayoshiriki ligi kuu nchini Uganda, alipatia timu yake bao la kuongoza dhidi ya Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini humo, bao hilo alilifunga kwa ufundi mkubwa katika kipindi cha pili baada ya kupokea pasi murua na kupiga shuti kali akiwa nje ya 18. Akitoa taarifa kutoka Moshi, mwenyekiti wa Wagosi Hemed Hilal ‘Aurora’ amesema “Katika dakika za lal...

Tuhuma nzito : Magufuli, Mwakyembe, Lukuvi kufikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge

Dk John Magufuli   Dar es Salaam.   Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imesema itawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akiwatuhumu kwa kulidanganya Bunge. Hatua hiyo ilitangazwa jana na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe baada ya kumhoji Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert Mrango kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka wa fedha 2011/2012. Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo kiasi cha Sh348,075,000,000 fedha za ndani zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililotajwa kuwa ni la mradi maalumu (Special Road Construction Project) hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni. “Ni vizuri leo uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. T...