Skip to main content

HUYU NDIE ANASEMA SIASA ZA WAZIRI MEMBE NI ZA KINAFIKI, ANAFANYA MCHEZO WA KIHUNI NA ANAHUSIKA KUMCHAFUA RAIS KIKWETE

Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa Chama cha Mapinduzi CCM, HUSSEIN BASHE
Mjumbe wa mkutano mkuu wa taifa wa CCM Hussein Bashe amefikia hatua hiyo ya kumtaja Benarnd Membe kutokana na vipeperushi vinavyodaiwa kusambazwa Dodoma kwamba Bashe na kundi lake limepanga kuwashawishi wajumbe wa mkutano mkuu kupiga kura za maruhani ili Rais Kikwete asiwe na uongozi wa kofia mbili ikiwemo ile ya Uenyekiti wa Taifa wa CCM.
BASHE amesema kwa mfumo wa kiuongozi ndani ya CCM ni mwendawazimu pekee anayewaza kwamba suala hilo linawezekana na kwamba kauli iliyotolewa na mmoja wa kada wa chama hicho AGUSTINO MATEFU juu ya kumpunguzia kura rais ni mkakati uliopangwa ili kumdhalilisha Mwenyekiti wa CCM Taifa.
Ili kuondoa utata wa juu ya anayehusika kuwatuma vijana wanaoeneza chuki na makundi ndani ya CCM, Bashe amemtaja mmoja wa Mawaziri wa awamu ya hii kwamba anaendesha mchezo mchafu ili kujisafishia njia ya Urais 2015.
Wakati hayo yakitokea tayari maandalizi ya shughuli za ufunguzi wa mkutano mkuu zimekamilika na wajumbe wameshawasili Dodoma tayari kuwachagua viongozi mbalimbali katika Ukumbi wa mikutano wa Kizota.
Namkariri Bashe akisema “anaewatumia hawa vijana ni Benard Membe ndio anaefanya huu mchezo wa kihuni ambao amekua akiufanya kwa muda mrefu ndani ya chama chetu, nilisema aache michezo hii… ameweza kubakia kwenye siasa za CCM kwa muda mrefu kwa kugawa watu, huu ni sehemu ya mpango wake amekua akitumia vijana hawa, kama mlikuepo hapa Dodoma wakati tunafanya uchaguzi wa vijana alikuja mpambe wake mkubwa kabisa ndugu Nyalandu kutuletea vurugu katika ukumbi wa uchaguzi
Kwenye line ya pili Bashe amesema “nataka kutumia fursa hii kumwambia Membe kwamba sina mpango wa kumnyima kura rais Jakaya bali nina mpango wa kumnyima yeye kura, kura yangu hatopata, kura ya wale wote wanaoweza kunielewa hatopata na kama atashinda NEC atashinda kwa kura za watu wengine na sio kura ya Hussein Bashe, kwa muda mrefu Membe amekua akisurvive kwa siasa za unafiki na uongo ndani ya chama chetu na bahati mbaya viongozi wanafamu, ni mwendawazimu tu anaeweza kufikiri ndani ya chama chetu tunaweza kufikiria tumuweke mwenyekiti mwingine na rais mwingine, huyo atakua aidha ana matatizo ya akili ama sio mwanachama wa CCM”
Kuhusu kipeperushi, Bashe amesema “kwanza kipeperushi hicho hata kukiona sijakiona, hakuna mpango huo na sijawahi kufikiri kuendesha hujuma/mkakati dhidi ya rais Jakaya Mrisho Kikwete”

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

Coastal ipo tayari kuanza ligi kuu, yashinda 3-0 ikiwa kambini Moshi.

Wachezaji wa Coastal Union wakifanya mazoezi mepesi muda mfupi kabla ya kukabiliana na Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini Moshi, anayeonekana pichani mwenye jezi namba 17 ni haruna Moshi 'Boban'. Mtokeo ya mechi hiyo ni ushindi wa 3-0 kwa Wagosi. Mazoezi yamekolea, uwanja wa Ushirika Moshi. Uhuru Suleiman amesifiwa na kocha kuwa ni kiungo mwenye kasi nyingi na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira. Mshambuliaji anayetumia mguu wa kushoto kutoka Uganda, Yayo Lutimba Kato amefunga bao lake la kwanza tangu kujiunga na Coastal Union ambayo imeweka kambi mjini Moshi tangu jana. Kato ambaye ametoka URA inayoshiriki ligi kuu nchini Uganda, alipatia timu yake bao la kuongoza dhidi ya Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini humo, bao hilo alilifunga kwa ufundi mkubwa katika kipindi cha pili baada ya kupokea pasi murua na kupiga shuti kali akiwa nje ya 18. Akitoa taarifa kutoka Moshi, mwenyekiti wa Wagosi Hemed Hilal ‘Aurora’ amesema “Katika dakika za lal...

Tuhuma nzito : Magufuli, Mwakyembe, Lukuvi kufikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge

Dk John Magufuli   Dar es Salaam.   Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imesema itawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akiwatuhumu kwa kulidanganya Bunge. Hatua hiyo ilitangazwa jana na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe baada ya kumhoji Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert Mrango kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka wa fedha 2011/2012. Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo kiasi cha Sh348,075,000,000 fedha za ndani zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililotajwa kuwa ni la mradi maalumu (Special Road Construction Project) hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni. “Ni vizuri leo uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. T...