
Viongozi wa Afrika Magharibi
wanatarajiwa kukutana katika mji mkuu wa Nigeria, Abuja, kukamilisha
mipango ya kuwatuma wanajeshi kaskazini mwa Mali.
Mazungumzo hayo yatashughulika na mapendekezo ya
kutuma wanajeshi elfu kadha kuwaondoa wapiganaji wa Kiislamu, iwapo
juhudi za kufanya majadiliano hazitafanikiwa.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limewasihi viongozi Afrika magharibi kutayarisha mpango huo kufikia mwisho wa mwezi huu.
Mataifa ya Magharibi yamejitolea kutuma vikosi vya kutoa mafunzo kwa majeshi ya Afrika Magharibi.