Skip to main content

Rais Morsi aahidi demokrasia

Egypt's President Mohamed Mursi speaks to supporters in front of the presidential palace in Cairo November 23, 2012. Mursi's decision to assume sweeping powers caused fury amongst his opponents and prompted violent clashes in central Cairo and other cities on Friday. REUTERS/Egyptian Presidency/Handout (EGYPT - Tags: POLITICS) FOR EDITORIAL USE ONLY. NOT FOR SALE FOR MARKETING OR ADVERTISING CAMPAIGNS. THIS IMAGE HAS BEEN SUPPLIED BY A THIRD PARTY. IT IS DISTRIBUTED, EXACTLY AS RECEIVED BY REUTERS, AS A SERVICE TO CLIENTS
Rais Mohamed Morsi amesisitiza Ijumaa (22.11.2012)kuwa Misri inaelekea katika "uhuru na demokrasia",baada ya kujilimbikizia madaraka makubwa,hali ambayo imezusha mapambano kati ya wale wanaomuunga mkono na mahasimu.
"Uthabiti wa kisiasa, uthabiti wa kijamii na uthabiti wa kiuchumi ndio kitu ninachokitaka na ndio ninachokifanyia kazi," ameuambia mkusanyiko wa wafuasi wake nje ya Ikulu ya nchi hiyo.
Wapinzani wa Morsi walianza hatua ya kukalia eneo la Tahrir kwa muda wa wiki moja, eneo ambalo linatambulika kuwa ishara ya maandamano ambayo yameuangusha utawala wa rais wa zamani wa nchi hiyo Hosni Mubarak mwaka jana, na wametoa wito wa maandamano makubwa zaidi siku ya Jumanne.
Protesters storm an office of Egyptian President Mohammed Morsi's Muslim Brotherhood Freedom and Justice party and set fires in the Mediterranean port city of Alexandria, Egypt, Friday, Nov. 23, 2012. State TV says Morsi opponents also set fire to his party's offices in the Suez Canal cities of Suez, Port Said and Ismailia. Opponents and supporters of Morsi clashed across Egypt on Friday, the day after the president granted himself sweeping new powers that critics fear can allow him to be a virtual dictator. (Foto:Amira Mortada, El Shorouk Newspaper/AP/dapd) EGYPT OUT
 
Waandamanaji wakivamia ofisi ya chama cha udugu wa Kiislamu na kuchoma moto mali mbali mbali
Magari yachomwa moto
Mapambano yalizuka kati ya polisi na waandamanaji karibu na uwanja huo, huku waandamanaji wakichoma moto gari la polisi, wamesema watu walioshuhudia.
Na mapambano ya ghasia yamezuka kati ya waungaji mkono wa Morsi na mahasimu wao katika mji wa Suez pamoja na mji wa Alexandria , ambapo waandamanaji walivamia ofisi ya chama tawala cha udugu wa Kiislamu.
Flames burn around a police vehicle after protesters threw a molotov cocktail at it during clashes at Tahrir square in Cairo November 23, 2012. Egyptian President Mohamed Mursi's decree that put his decisions above legal challenge until a new parliament was elected caused fury amongst his opponents on Friday who accused him of being the new Hosni Mubarak and hijacking the revolution. Police fired tear gas in a street leading to Cairo's Tahrir Square, heart of the 2011 anti-Mubarak uprising, where thousands demanded Mursi quit and accused him of launching a coup. There were violent protests in Alexandria, Port Said and Suez. REUTERS/Mohamed Abd El Ghany (EGYPT - Tags: CIVIL UNREST POLITICS)  
Waandamanaji mjini Cairo wamechoma moto gari la polisi
Katika tamko ambalo lilisomwa katika televisheni siku ya Alhamis, rais , "anaweza kuchukua uamuzi wowote ama hatua yoyote kulinda mapinduzi. Maamuzi ya kikatiba, maamuzi na sheria zinazotolewa na rais ni za mwisho na haziwezi kukatiwa rufaa."
Hatua hiyo ni pigo kwa vuguvugu la wanaopendelea demokrasia ambao walifanikisha kumuondoa madarakani rais Mubarak , na kuzusha hofu kuwa Waislamu wanaweza kujikita zaidi katika madaraka.
Jumuiya ya kimataifa yaingiwa na wasi wasi
Pia hali hiyo imezusha wasi wasi kimataifa, huku Marekani ikitoa wito wa utulivu na kuzitaka pande zote kufanyakazi kwa pamoja.
"Uamuzi na matamko yaliyotangazwa Novemba 22 yamezusha wasi wasi kwa wengi wa Wamisri na jamii ya kimataifa, amesema msemaji wa wizara ya mambo ya kigeni ya Marekani Victoria Nuland.
"Moja kati ya nia ya mapinduzi ilikuwa kuhakikisha kuwa madaraka hayatakuwa mikononi mwa mtu mmoja ama taasisi," amesema msemaji huyo wa wizara ya mambo ya kigeni katika taarifa.
Mjini Brussels, msemaji wa mkuu wa sera za mambo ya kigeni wa umoja wa Ulaya Catherine Ashton amesema, " Ni muhimu sana kwamba hatua za kidemokrasia zikamilike kwa mujibu wa jukumu linalochukuliwa na uongozi wa Misri."
Shirika linalotetea haki za binadamu la Amnesty International limeshutumu madaraka hayo mapya ya Morsi, ambayo "yanakandamiza utawala wa sheria na kuileta enzi mpya ya ukandamiza."
epa03483598 Egyptian protesters shout against President Mohamed Morsi, during a rally over Morsi decrees,in tahrir square, Cairo, Egypt, 23 November 2012. Opposition planned a mass rally to protest constitutional changes ordered by the Islamist President Morsi. Egyptian President Mohammed Morsi said on 23 November that a decree granting him sweeping powers was not designed to 'settle scores' with the opposition, but to ensure national stability. EPA/KHALED ELFIQI
 
Waandamanaji mjini Cairo
"Watu wanaunga mkono uamuzi wa rais," kundi la watu lilikuwa likiimba.
Siku ya Alhamis, (22.11.2012) Morsi aliipunguzia madaraka mahakama ambayo inapingana nae, ambayo imekwishafikiria iwapo kuondoa jopo linalodhibitiwa na kundi hilo la Waislamu ambalo linaunda rasimu ya katiba , na kuwavua madaraka majaji ya haki ya kutoa hukumu juu ya kesi ama kupinga uamuzi wake.

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

Coastal ipo tayari kuanza ligi kuu, yashinda 3-0 ikiwa kambini Moshi.

Wachezaji wa Coastal Union wakifanya mazoezi mepesi muda mfupi kabla ya kukabiliana na Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini Moshi, anayeonekana pichani mwenye jezi namba 17 ni haruna Moshi 'Boban'. Mtokeo ya mechi hiyo ni ushindi wa 3-0 kwa Wagosi. Mazoezi yamekolea, uwanja wa Ushirika Moshi. Uhuru Suleiman amesifiwa na kocha kuwa ni kiungo mwenye kasi nyingi na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira. Mshambuliaji anayetumia mguu wa kushoto kutoka Uganda, Yayo Lutimba Kato amefunga bao lake la kwanza tangu kujiunga na Coastal Union ambayo imeweka kambi mjini Moshi tangu jana. Kato ambaye ametoka URA inayoshiriki ligi kuu nchini Uganda, alipatia timu yake bao la kuongoza dhidi ya Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini humo, bao hilo alilifunga kwa ufundi mkubwa katika kipindi cha pili baada ya kupokea pasi murua na kupiga shuti kali akiwa nje ya 18. Akitoa taarifa kutoka Moshi, mwenyekiti wa Wagosi Hemed Hilal ‘Aurora’ amesema “Katika dakika za lal...

Tuhuma nzito : Magufuli, Mwakyembe, Lukuvi kufikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge

Dk John Magufuli   Dar es Salaam.   Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imesema itawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akiwatuhumu kwa kulidanganya Bunge. Hatua hiyo ilitangazwa jana na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe baada ya kumhoji Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert Mrango kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka wa fedha 2011/2012. Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo kiasi cha Sh348,075,000,000 fedha za ndani zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililotajwa kuwa ni la mradi maalumu (Special Road Construction Project) hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni. “Ni vizuri leo uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. T...