Skip to main content

Waasi wa M23 wakutana na Kabila

The M23 rebels spokesperson Vianney Kazarama (L) speaks to the crowd who have gathered at a stadium in Goma November 21, 2012. Rebel forces in eastern Congo said on Wednesday they planned to take control of the whole of the vast central African country after they captured the eastern town of Goma while United Nations peacekeepers looked on. REUTERS/James Akena (DEMOCRATIC REPUBLIC OF CONGO - Tags: CIVIL UNREST POLITICS)
                                                          Waasi wa M23 wametangaza  
kuanzisha mazungumzo na rais wa jamhuri ya kidemokrasi ya Congo Joseph Kabila,saa chache baada ya mkutano wa kimkoa kulitaka kundi hilo kusitisha mashambulizi yake mashariki mwa nchi hiyo.
Wakipata ushindi mdogo kwa viongozi hao wa kimkoa, kiongozi wa kisiasa wa kundi hilo la waasi wa mashariki ya jamhuri ya Congo Jean -Marie Runiga Lugerero , amesema kuwa alikuwa na mazungumzo ya awali na Kabila baada ya mkutano huo uliofanyika mjini Kampala kumalizika.
Wakati hakualikwa binafsi katika mkutano huo , Runiga Lugerero aliliambia shirika la habari la AFP kuwa alifanikiwa kukutana na Kabila kwa kupitia upatanishi wa rais wa Uganda Yoweri Museveni, ambae alitarajiwa kufanya nae mazungumzo hii leo Jumapili(25.11.2012).
In this Wednesday Nov. 21, 2012 photo released by Uganda's Presidential Press Services, Uganda's President Yoweri Museveni, center, sits with his counterparts Paul Kagame of Rwanda, left, and Joseph Kabila of Congo during a meeting in Kampala, Uganda. The three heads of the states want the M23 rebels out of Goma, a town they captured from Congo army. (Foto:Presidential Press Services/AP/dapd)
  Viongozi wa Afrika wakikutanamjini 
 Kampala, rais Kabila (kulia) na Museveni (katikati)
"Hali ilikuwa tete lakini baadaye , kila upande ulipunguza jazba katika majadiliano kwasababu haya si matatizo ya kibinafsi , lakini ni matatizo ya nchi" ambayo inapaswa kupatiwa ufumbuzi, ameliambia shirika la habari la AFP kwa simu.
"Nafikiri mkutano huo ulikwenda vizuri sana".
Runiga Lugerero na Kabila watakutana tena leo Jumapili(25.11.2012) kujadiliana juu ya vipi mazungumzo yao yatakavyoendelea, ameongeza.
"Ndio walikutana," Waziri wa mambo ya kigeni wa jamhuri ya kidemokrasi ya Congo Raymond Tshibanda ameliambia shirika hilo la habari. Lakini amekanusha kuwa mazungumzo zaidi ya ana kwa ana kati ya Kabila na kundi la M23 yanatarajiwa.
Ugandan President, Yoweri Museveni speaks during the London Summit on Family Planning organized by the UK Government and the Bill & Melinda Gates Foundation with the United Nations Population Fund, UNFPA, in central London Wednesday July 11, 2012. (Foto:Carl Court, Pool/AP/dapd)
  Rais Yoweri Museveni wa Uganda
Tangazo la Runiga Lugerero limekuja siku chache baada ya Kabila kuonekana kuondoa uwezekano wa mazungumzo na majeshi hayo ya waasi.
Na saa chache hapo kabla , katika tamko lao la kufunga kikao , viongozi wa kimkoa wametoa wito kwa wapiganaji wa kundi la M23 kusitisha mapigano na kuondoa majeshi yao katika mji muhimu wa mashariki wa Goma katika muda wa saa 48.
Runiga Lugerero , hata hivyo , ameweka wazi kuwa hatua yoyote ya kuondoa majeshi itakuja pale tu baada ya mazungumzo kati ya kundi hilo la waasi na Kabila. Wapiganaji wa M23 watalinda maeneo yao iwapo majeshi ya Congo yatashambulia, ameonya.
Kagame hakuhudhuria
Mkutano huo hata hivyo haukuhudhuriwa na rais wa Rwanda Paul Kagame. Maafisa wa Uganda wametangaza hapo mapema Jumamosi kuwa Rwanda badala yake itawakilishwa na waziri wa mambo ya kigeni Louise Mushikwabo.
Rwanda's President Paul Kagame listens to deliberations during the International Conference on the Great Lakes Region (ICGLR) at the Commonwealth Resort Hotel Munyonyo in the Ugandan capital of Kampala August 8, 2012. African leaders of the Great Lakes region say they will impose sanctions on any party obstructing peace in the volatile Democratic Republic of Congo on Wednesday. The decision was reached at the end of a two-day leaders summit on the conflict in Uganda. REUTERS/Edward Echwalu (UGANDA - Tags: POLITICS CIVIL UNREST)
  Rais Paul Kagame wa Rwanda
Kagame amekuwa akikana shutuma , sio tu kutoka jamhuri ya kidemokrasi ya Congo lakini pia kutoka kwa wachunguzi wa umoja wa mataifa , kuwa Rwanda inawaunga mkono , na kuliendesha jeshi la waasi la M23 ambalo wengi wao ni kutoka kabila la Watutsi.
Waasi watakiwa kusitishamapigano
Katika taarifa yao ya pamoja mwishoni mwa kikao chao , viongozi wa kimkoa wamelitaka kundi la waasi la M23 , "kusitisha shughuli zote za kivita", na "kuacha kusema kuwa wanataka kuiangusha serikali iliyochaguliwa ya Congo." Siku ya Jumatano, (21.11.2012), Vianney Kazarama, mmoja kati ya viongozi wa waasi, amesema kuwa Kabila ni lazima aondoke madarakani.
Waziri wa mambo ya kigeni wa Uganda Sam Kutesa amesema kuwa mkutano huo umetoa wito kwa waasi kuondoka kutoka mjini Goma na kurejea katika eneo karibu kilometa 20 kaskazini mwa mji huo.

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

Coastal ipo tayari kuanza ligi kuu, yashinda 3-0 ikiwa kambini Moshi.

Wachezaji wa Coastal Union wakifanya mazoezi mepesi muda mfupi kabla ya kukabiliana na Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini Moshi, anayeonekana pichani mwenye jezi namba 17 ni haruna Moshi 'Boban'. Mtokeo ya mechi hiyo ni ushindi wa 3-0 kwa Wagosi. Mazoezi yamekolea, uwanja wa Ushirika Moshi. Uhuru Suleiman amesifiwa na kocha kuwa ni kiungo mwenye kasi nyingi na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira. Mshambuliaji anayetumia mguu wa kushoto kutoka Uganda, Yayo Lutimba Kato amefunga bao lake la kwanza tangu kujiunga na Coastal Union ambayo imeweka kambi mjini Moshi tangu jana. Kato ambaye ametoka URA inayoshiriki ligi kuu nchini Uganda, alipatia timu yake bao la kuongoza dhidi ya Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini humo, bao hilo alilifunga kwa ufundi mkubwa katika kipindi cha pili baada ya kupokea pasi murua na kupiga shuti kali akiwa nje ya 18. Akitoa taarifa kutoka Moshi, mwenyekiti wa Wagosi Hemed Hilal ‘Aurora’ amesema “Katika dakika za lal...

Tuhuma nzito : Magufuli, Mwakyembe, Lukuvi kufikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge

Dk John Magufuli   Dar es Salaam.   Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imesema itawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akiwatuhumu kwa kulidanganya Bunge. Hatua hiyo ilitangazwa jana na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe baada ya kumhoji Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert Mrango kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka wa fedha 2011/2012. Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo kiasi cha Sh348,075,000,000 fedha za ndani zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililotajwa kuwa ni la mradi maalumu (Special Road Construction Project) hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni. “Ni vizuri leo uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. T...