Skip to main content

Wachimba migodi bado wagoma

Wachimba migodi wa Amplats wakigoma mwezi OktobaMaelfu ya wachimba migodi wa Afrika Kusini wamekataa kurejea kazini, katika kampuni ya dhahabu nyeupe kubwa kabisa duniani iitwayo Anglo American, Amplats
Wachimba migodi wanasema hawakubali pendekezo la kampuni hiyo kuhusu malipo.
Mwezi Oktoba Amplats iliwafukuza makazini wachimba migodi 12,000 kwa sababu walishiriki kwenye mgomo katika migodi ya Rustenberg.
Tangu wakati huo uchimbaji wa dhahabu nyeupe umeathirika sana.
Amplats ni kampuni kubwa ya mwisho ya Afrika Kusini ambayo bado inaathirika na migomo - migomo iliyokuwa na ghasia ambapo watu zaidi ya 50 wamekufa.
Wachimba migodi 34 walipigwa risasi na polisi katika mgodi wa kampuni ya Lonmin mwezi wa Agosti.

Popular posts from this blog

NEW JOINT | dayna special nipe nafasi {Audio}

Goog music from tng jojo yatakwisha hii apa

DownLoad Na Sikiliza Joint Mpya Ya Squizer Ft Belle 9 - Mtemi Pesa