Skip to main content

Wafungwa wawatoa kwa nguvu FFU kwenye nyumba

BAADHI ya wafungwa mjini Moshi mkoani Kilimanjaro wanadaiwa kutumiwa na kigogo mmoja wa Polisi kuwatoa kwa nguvu askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) kwenye nyumba walizokuwa wakiishi katika Kambi Kuu ya mjini Moshi.

Tofauti na ilivyozoeleka ambapo hushuhudiwa FFU wakitumika kusambaratisha mikusanyiko ya watu wenye lengo la kuhatarisha amani, askari hao walitolewa kwa nguvu kwenye nyumba hizo na wafungwa hao ambao wanadaiwa kutoa vyombo vyao nje.

Tukio hilo lililowaacha vinywa wazi watu wengi mkoani Kilimanjaro, limewapata FFU waliokuwa wakiishi kwenye nyumba tatu zilizopo katika kambi kuu ya polisi mjini Moshi.

Taarifa zinadai FFU hao ilibainika kuwa   hawakupaswa kuishi katika nyumba hizo, badala yake polisi wa kawaida ndio waliopaswa kuishi, hivyo waliondolewa ili polisi hao waingie.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz alipoulizwa na gazeti hili alikiri kutokea kwa tukio hilo, lakini akasema: “Hayo ni masuala ya ndani ya polisi, siyo ya kuyaandika.”

Habari zaidi zinapasha kuwa tukio hilo lilitokea Alhamisi iliyopita zikieleza kuwa kigogo mmoja wa polisi (jina tunalo), ndiye aliyewatumia wafungwa hao kuvamia na kuvunja milango ya nyumba za FFU hao ili kuwaondoa kwa nguvu, akidai kuwa alitumia njia za busara kuwataka watoke lakini walionekana  kuleta kiburi na kwamba hakuona sababu ya kuwatumia polisi.
“Ilikuwa saa 5:00 asubuhi ndipo alikuja bosi wetu (jina tunalihifadhi) akiwa na wafungwa, wakavunja milango ya nyumba za hao jamaa (FFU) na kutupa vyombo vyao nje,” kilieleza chanzo chetu.
Habari zaidi zimedai kuwa kigogo huyo mwenye cheo kikubwa alitumia mbinu hiyo kuwadhalilisha askari hao jambo linaloelezwa kuwasononesha FFU hao, huku polisi wengine wakipoteza morali wa kufanya kazi.
“Tuna mahakama zetu za kijeshi, kwa nini asitumie utaratibu huo kama hawakuingia kihalali waamriwe kutoa vitu vyao nje kwa njia ya kistaarabu badala ya kuwadhalilisha hivyo?” alihoji askari mmoja aliyeomba asiandikwe jina lake  kwa sababu za usalama.
Askari mwingine alisema kuwa kitendo cha kutupa vitu nje ya nyumba kwa kuwatumia wafungwa ni kuwadhalilisha polisi.
Alisema kuwa utaratibu uliozoeleka kambini hapo ni kwamba, polisi akitaka kuhama, aliye na shida ya nyumba ndiye anazungumza naye, ili kuangalia kama anaweza kumwachia nyumba husika au la.

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

Coastal ipo tayari kuanza ligi kuu, yashinda 3-0 ikiwa kambini Moshi.

Wachezaji wa Coastal Union wakifanya mazoezi mepesi muda mfupi kabla ya kukabiliana na Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini Moshi, anayeonekana pichani mwenye jezi namba 17 ni haruna Moshi 'Boban'. Mtokeo ya mechi hiyo ni ushindi wa 3-0 kwa Wagosi. Mazoezi yamekolea, uwanja wa Ushirika Moshi. Uhuru Suleiman amesifiwa na kocha kuwa ni kiungo mwenye kasi nyingi na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira. Mshambuliaji anayetumia mguu wa kushoto kutoka Uganda, Yayo Lutimba Kato amefunga bao lake la kwanza tangu kujiunga na Coastal Union ambayo imeweka kambi mjini Moshi tangu jana. Kato ambaye ametoka URA inayoshiriki ligi kuu nchini Uganda, alipatia timu yake bao la kuongoza dhidi ya Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini humo, bao hilo alilifunga kwa ufundi mkubwa katika kipindi cha pili baada ya kupokea pasi murua na kupiga shuti kali akiwa nje ya 18. Akitoa taarifa kutoka Moshi, mwenyekiti wa Wagosi Hemed Hilal ‘Aurora’ amesema “Katika dakika za lal...

Tuhuma nzito : Magufuli, Mwakyembe, Lukuvi kufikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge

Dk John Magufuli   Dar es Salaam.   Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imesema itawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akiwatuhumu kwa kulidanganya Bunge. Hatua hiyo ilitangazwa jana na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe baada ya kumhoji Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert Mrango kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka wa fedha 2011/2012. Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo kiasi cha Sh348,075,000,000 fedha za ndani zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililotajwa kuwa ni la mradi maalumu (Special Road Construction Project) hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni. “Ni vizuri leo uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. T...