Skip to main content

Wafungwa wawatoa kwa nguvu FFU kwenye nyumba

BAADHI ya wafungwa mjini Moshi mkoani Kilimanjaro wanadaiwa kutumiwa na kigogo mmoja wa Polisi kuwatoa kwa nguvu askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) kwenye nyumba walizokuwa wakiishi katika Kambi Kuu ya mjini Moshi.

Tofauti na ilivyozoeleka ambapo hushuhudiwa FFU wakitumika kusambaratisha mikusanyiko ya watu wenye lengo la kuhatarisha amani, askari hao walitolewa kwa nguvu kwenye nyumba hizo na wafungwa hao ambao wanadaiwa kutoa vyombo vyao nje.

Tukio hilo lililowaacha vinywa wazi watu wengi mkoani Kilimanjaro, limewapata FFU waliokuwa wakiishi kwenye nyumba tatu zilizopo katika kambi kuu ya polisi mjini Moshi.

Taarifa zinadai FFU hao ilibainika kuwa   hawakupaswa kuishi katika nyumba hizo, badala yake polisi wa kawaida ndio waliopaswa kuishi, hivyo waliondolewa ili polisi hao waingie.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz alipoulizwa na gazeti hili alikiri kutokea kwa tukio hilo, lakini akasema: “Hayo ni masuala ya ndani ya polisi, siyo ya kuyaandika.”

Habari zaidi zinapasha kuwa tukio hilo lilitokea Alhamisi iliyopita zikieleza kuwa kigogo mmoja wa polisi (jina tunalo), ndiye aliyewatumia wafungwa hao kuvamia na kuvunja milango ya nyumba za FFU hao ili kuwaondoa kwa nguvu, akidai kuwa alitumia njia za busara kuwataka watoke lakini walionekana  kuleta kiburi na kwamba hakuona sababu ya kuwatumia polisi.
“Ilikuwa saa 5:00 asubuhi ndipo alikuja bosi wetu (jina tunalihifadhi) akiwa na wafungwa, wakavunja milango ya nyumba za hao jamaa (FFU) na kutupa vyombo vyao nje,” kilieleza chanzo chetu.
Habari zaidi zimedai kuwa kigogo huyo mwenye cheo kikubwa alitumia mbinu hiyo kuwadhalilisha askari hao jambo linaloelezwa kuwasononesha FFU hao, huku polisi wengine wakipoteza morali wa kufanya kazi.
“Tuna mahakama zetu za kijeshi, kwa nini asitumie utaratibu huo kama hawakuingia kihalali waamriwe kutoa vitu vyao nje kwa njia ya kistaarabu badala ya kuwadhalilisha hivyo?” alihoji askari mmoja aliyeomba asiandikwe jina lake  kwa sababu za usalama.
Askari mwingine alisema kuwa kitendo cha kutupa vitu nje ya nyumba kwa kuwatumia wafungwa ni kuwadhalilisha polisi.
Alisema kuwa utaratibu uliozoeleka kambini hapo ni kwamba, polisi akitaka kuhama, aliye na shida ya nyumba ndiye anazungumza naye, ili kuangalia kama anaweza kumwachia nyumba husika au la.

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

MAJINA YA WASHIRIKI NA WA WEZESHAJI WA FILM YA HOUSE GIRL!

CAST SELEMANI MOHAMED / BUNTO ANDREW / C-O YORAM MWETA / MGANGA MWANTUMU / MKE WA C-O JOHN / MCHUNGAJI BI FURURATU / JINI WAOMBOLEZAJI SAUMU HUSENI HASHIMU BABA RASTA MAN YOHANNA TAMILWAI SAIDI MWALUBADU SEMY STIR SELEMANI MOHAMEDI  AND ANDREW C-O LOCATION ATHUMANI HAMADI MAKE UP MWASHAMBA RAMADHANI BEDUI DEREVA DAUDI SPOONSER SAIDI SHABANI AND THE FRESH2012 GLOB SOUND PRODUCER J-B LIGHT YOHANNA TAMILWAI THENK YOU THE FRESH ENERTAINMENT AND THE FRESH2012 BLOG CONTACTS 0653785027 +255714091786 ZAIDI TEMBELEA www.the-fresh.blogspot.com ADRESS Thefresh@ymail.com AU Saidshabani60@gmai.com

Video: Blackchild – Put Inside

David Abdulichel, also known as BlackChild is a Ghanaian from Asanti origin, born and raised in Lagos Nigeria. BlackChild, who is a recording artist, song writer and performer started his music career back in 2000 and since then has released four singles. He has also worked with top producers in Nigeria such as Fliptyce, Spanky, Meca E & BrainMix to mention but few. BlackChild Abdul rose to prominence with his hit songs “Treasure”, “Ele” featuring Rock Steady, “Could It Be Love” featuring Cartiar, “All I Need” featuring Solid Star. This time around he comes out with “Put Inside” which sees him delivering lines in french and his native language and is steadily generating buzz and enjoying airplay on radio stations within and outside Lagos. Listen up!