Skip to main content

Ndege ya Tanapa yaanguka, yajeruhi rubani

  NDEGE ndogo ya abiria mali ya Hifadhi ya Taifa ya Tanapa  yenye uwezo wa kubeba  watu  wanne aina ya C 182, imeanguka katika  eneo la Kasimba  umbali wa kilometa moja  kutoka katika  Uwanja wa Ndege wa Mpanda  uliopo katika Mkoa wa Katavi  na kumjeruhi rubani wa ndege hiyo.
Akizungumza na vyombo vya habari, Meneja wa Uwanja wa Ndege wa Mpanda, Maulid  Mohamed alisema ajali  hiyo  ilitokea jana  majira saa 10 .55 jioni  katika   eneo la Kasimba lililopo ndani ya Kijiji  cha Nsemlwa   wilayani hapo.
Mohamed aliitaja ndege hiyo iliyoanguka na kusababisha majeraha kwa rubani aliyetajwa kwa jina la Adam Athuman Kajwaa kuwa  ni aina ya C182.
Mohamed  alieleza kuwa  ndege  hiyo   ilikuwa imetoka  katika uwanja wa ndege wa Mpanda ikielekea  katika Hifadhi ya Wanyamapori  ya Katavi.   
Hata hiyo alisema kuwa ajali hiyo  ilitokea   umbali wa  kilometa  moja na  nusu  kutoka Uwanja wa Ndege wa Mpanda  mara  baada  ya  kuondoka  katika uwanja huo ambapo imeharibika sana sehemu ya bawa lake na upande wa injini.
Meneja wa uwanja  huo wa ndege  alisema  taarifa za awali   zinaonyesha  chanzo   cha ajali  hiyo  kilitokana na kufeli kwa  injini  ya ndege  na kuwa rubani wa ndege hiyo   alipata msaada  wa kuokolewa na  wananchi  waliokuwa  wakifanya  shughuli  za  kilimo  kwenye  mashamba.
Mmoja wa  wa mashuhuda wa tukio hilo Credo Mwanisenga   alieleza  kuwa wakati   akiwa  anafanya shughuli  zake  za kilimo  ghafla  aliona  ndege  hiyo ikiwa  angani  ikizimika  na baada ya  muda  mfupi   ikaanguka   jirani  na mti wa mwembe.
Hata hivyo alisema kuwa zoezi la kumuokoa rubani huyo lilichukua muda kuanza kutokana na mti wa mwembe  kuwa na nyuki wengi.
Hata hivyo  alisema mara baada ya   kufanikiwa kumtoa  rubani  huyo,   huku akiwa  amepata  majerahi makubwa sehemu ya  uso  na maumivu  sehemu ya kifua   na kumkimbiza katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda kwa matibabu zaidi,
Pia akiwa anakohoa damu,  rubani huyo aliwahishwa  haraka katika Hospitali ya wilaya ya Mpanda baada ya kupata  msaada wa gari la meneja wa uwanja wa ndege aliyefika  eneo   la tukio.

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

MAJINA YA WASHIRIKI NA WA WEZESHAJI WA FILM YA HOUSE GIRL!

CAST SELEMANI MOHAMED / BUNTO ANDREW / C-O YORAM MWETA / MGANGA MWANTUMU / MKE WA C-O JOHN / MCHUNGAJI BI FURURATU / JINI WAOMBOLEZAJI SAUMU HUSENI HASHIMU BABA RASTA MAN YOHANNA TAMILWAI SAIDI MWALUBADU SEMY STIR SELEMANI MOHAMEDI  AND ANDREW C-O LOCATION ATHUMANI HAMADI MAKE UP MWASHAMBA RAMADHANI BEDUI DEREVA DAUDI SPOONSER SAIDI SHABANI AND THE FRESH2012 GLOB SOUND PRODUCER J-B LIGHT YOHANNA TAMILWAI THENK YOU THE FRESH ENERTAINMENT AND THE FRESH2012 BLOG CONTACTS 0653785027 +255714091786 ZAIDI TEMBELEA www.the-fresh.blogspot.com ADRESS Thefresh@ymail.com AU Saidshabani60@gmai.com

Video: Blackchild – Put Inside

David Abdulichel, also known as BlackChild is a Ghanaian from Asanti origin, born and raised in Lagos Nigeria. BlackChild, who is a recording artist, song writer and performer started his music career back in 2000 and since then has released four singles. He has also worked with top producers in Nigeria such as Fliptyce, Spanky, Meca E & BrainMix to mention but few. BlackChild Abdul rose to prominence with his hit songs “Treasure”, “Ele” featuring Rock Steady, “Could It Be Love” featuring Cartiar, “All I Need” featuring Solid Star. This time around he comes out with “Put Inside” which sees him delivering lines in french and his native language and is steadily generating buzz and enjoying airplay on radio stations within and outside Lagos. Listen up!