Skip to main content

ROMA AAMUA KUUZA WIMBO WAKE MPYA KWA SH. 3000 HUKU NIKKI WA PILI NAYE AKITUMIA M-PESA KUIUZA DVD YAKE




                                  
Wasanii wanazidi kuwaza kila siku jinsi ya kukwepa kuibiwa kazi zao ambazo ni jasho lao wanalotoa booth baada ya kusumbua akili zao na kufanyia kazi vyema mtaji wa kipaji walichopewa na Mungu.



Asilimia 90 ya wasanii wa Hip Hop hawapeleki kazi zao kwa wasambazaji bali huuza wenyewe ili kukwepa kuwafaidisha watu wengine kwa jasho lao.



Staili ya uuzaji iliyopewa jina la ‘kuuuza tapes kwenye bag’ inazidi kupatiwa mbadala kama sio kuboreshwa ili kuwafikia watu wengi zaidi.



Roma mkatoliki ambae ametambulisha wimbo wake alioupa jina la ‘2030’, wimbo ambao unasubiriwa kwa huwa hadi sasa na fans wake kibao waweze kuupakua kwenye mtandao, sasa amekuja na staili tofauti ambapo anauuza wimbo huo kwa Tsh. 3000 tu .



Roma kupitia ukurasa wake wa facebook, ameelezea kuwa mteja wake atatuma pesa hiyo kwa njia ya simu pesa na email yake ama atatumiwa kwa njia ya Whasapp, kisha Roma atamtumia wimbo huo, lakini kwa makubaliano pia kuwa hatausambaza wala kuugawa ili kusapoti kazi yake iendane na kipato chake. 
Roma anasema kwa wale ambao hawana uwezo wa kununua basi watausikiliza tu redioni.




Nikki wa pili

Nikki wa Pili ambae ni msemaji wa WEUSI pia alizindua aina mpya ya usambazaji wa kazi za wasanii akianza na kazi yake, na hiyo December 23, katika tamasha la ‘Funga Mwaka la Weusi’ lilifanyika Dar-es-Salaam, Club Maisha, ambapo walizindua rasmi DVD ya Kum Kubam na wimbo mpya wa Lord Eyez “No More Drama”.



Katika aina hii mpya ya usambazaji, Mteja ama shabiki anatakiwa kutuma pesa kwa njia ya M-Pesa kiasi cha Tsh. 4,000 kisha atapewa CODE NUMBER ambayo ataipeleka kwa wakala wa Fichuka Dar na kupewa DVD hiyo ya BUM KUBAM.

Popular posts from this blog

Goog music from tng jojo yatakwisha hii apa

DownLoad Na Sikiliza Joint Mpya Ya Squizer Ft Belle 9 - Mtemi Pesa

MAJINA YA WASHIRIKI NA WA WEZESHAJI WA FILM YA HOUSE GIRL!

CAST SELEMANI MOHAMED / BUNTO ANDREW / C-O YORAM MWETA / MGANGA MWANTUMU / MKE WA C-O JOHN / MCHUNGAJI BI FURURATU / JINI WAOMBOLEZAJI SAUMU HUSENI HASHIMU BABA RASTA MAN YOHANNA TAMILWAI SAIDI MWALUBADU SEMY STIR SELEMANI MOHAMEDI  AND ANDREW C-O LOCATION ATHUMANI HAMADI MAKE UP MWASHAMBA RAMADHANI BEDUI DEREVA DAUDI SPOONSER SAIDI SHABANI AND THE FRESH2012 GLOB SOUND PRODUCER J-B LIGHT YOHANNA TAMILWAI THENK YOU THE FRESH ENERTAINMENT AND THE FRESH2012 BLOG CONTACTS 0653785027 +255714091786 ZAIDI TEMBELEA www.the-fresh.blogspot.com ADRESS Thefresh@ymail.com AU Saidshabani60@gmai.com