Skip to main content

"Rushwa yazorotesha uchumi duniani"



Greece's PM Antonis Samaras waits for visiting Luxembourg's PM and Eurogroup Chairman Jean-Claude Juncker before their meeting in Athens (Foto: Reuters) / Eingestellt von wa
                                          Waziri Mkuu wa Ugiriki Antonis Samaras
 
Kwa mara nyingine, Dernmark, Finland na New Zealand zimekuwa na rikodi nzuri kwa mujibu wa Transparency International wakati Afghanstan, Korea Kasikazini na Somalia zikisalia mkiani katika kadhia ya rushwa.
Kwa kuzingitia kipimo kinachoanisha sifuri - kama kiwango kibaya zaidi cha rushwa - mpaka 100 - ikiwa ndiyo rikodi nzuri kabisa, Dernmark, Finland na New Zealand zimefungana kwa kupata alama 90. Lakini Afghanstan, Korea Kaskazini na Somalia kila moja imepata alama 8.
Hali ilivyo katika mataifa ya Kiarabu
Pamoja na hayo, ripoti hiyo imeonesha kumekuwa na mafanikio kidogo sana katika mataifa ya Kiarabu yaliyokumbwa na vuguvugu la kisiasa. Mataifa hayo ni pamoja na Misri na maeneo mengine ya Mashariki ya Kati.
Mataifa ambayo ni kiini cha mgogoro wa madeni yameendelea kupata alama duni zaidi, ambapo tatizo hilo la mgogoro wa madeni limeonekana kama chachu ya vitendo vya rushwa. Ugiriki imepata alama 36, Italia 42, Ureno 63 na Uhispania 65.
Mkurugenzi Mkuu wa Transparency International, Cobus de Swardt, ameyataka mataifa yenye nguvu za kiuchumi duniani yanapaswa kuonesha mfano kwa kuhakikisha taasisi zake zinasimamia uwazi na kwamba viongozi wanawajibika katika hilo.
Mataifa ya Magharibi yanayoongoza kiviwanda, kama Uswis, Canada, Australia na Sweden yanashikilia tena ile nafasi yake ya kuwa safi katika kudhibiti tatizo la rushwa. Lakini China, kama taifa namba mbili kwa nguvu za kiuchumi duniani limepata alama 39.
Taifa kubwa kabisa lenye nguvu za kiuchumi duniani Marekani limepata alama 73 na Ujerumani, ambalo ni taifa lenye uchumi mkubwa kuliko yote barani Ulaya, ikiwa na alama 79. Urusi, pamoja na kuwa na utajiri mkubwa wa maliasili yake, inaonekana kufanya jitihada kidogo sana katika kukabiliana na tatizo la rushwa. Taifa hilo limeshika nafasi ya 133 katika nchi 176 katika kudhibiti rushwa kwa mujibu wa utafiti wa mwaka huu wa Transparency International.

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

Coastal ipo tayari kuanza ligi kuu, yashinda 3-0 ikiwa kambini Moshi.

Wachezaji wa Coastal Union wakifanya mazoezi mepesi muda mfupi kabla ya kukabiliana na Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini Moshi, anayeonekana pichani mwenye jezi namba 17 ni haruna Moshi 'Boban'. Mtokeo ya mechi hiyo ni ushindi wa 3-0 kwa Wagosi. Mazoezi yamekolea, uwanja wa Ushirika Moshi. Uhuru Suleiman amesifiwa na kocha kuwa ni kiungo mwenye kasi nyingi na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira. Mshambuliaji anayetumia mguu wa kushoto kutoka Uganda, Yayo Lutimba Kato amefunga bao lake la kwanza tangu kujiunga na Coastal Union ambayo imeweka kambi mjini Moshi tangu jana. Kato ambaye ametoka URA inayoshiriki ligi kuu nchini Uganda, alipatia timu yake bao la kuongoza dhidi ya Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini humo, bao hilo alilifunga kwa ufundi mkubwa katika kipindi cha pili baada ya kupokea pasi murua na kupiga shuti kali akiwa nje ya 18. Akitoa taarifa kutoka Moshi, mwenyekiti wa Wagosi Hemed Hilal ‘Aurora’ amesema “Katika dakika za lal...

Tuhuma nzito : Magufuli, Mwakyembe, Lukuvi kufikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge

Dk John Magufuli   Dar es Salaam.   Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imesema itawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akiwatuhumu kwa kulidanganya Bunge. Hatua hiyo ilitangazwa jana na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe baada ya kumhoji Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert Mrango kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka wa fedha 2011/2012. Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo kiasi cha Sh348,075,000,000 fedha za ndani zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililotajwa kuwa ni la mradi maalumu (Special Road Construction Project) hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni. “Ni vizuri leo uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. T...