Skip to main content

Ving'amuzi vyawatesa wakazi Dar

 
Kuzimwa kwa mitambo ya kurushia matangazo ya televisheni kwa mfumo wa analojia, kumezua utata baada ya wakazi wengi wa Mkoa wa Dar es Salaam kushindwa kupata matangazo. Mitambo hiyo ilizimwa juzi usiku kwa maelekezo ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).Baadhi ya wakazi wa jijini Dar es Salaam, wamesema hawapati matangazo ya televisheni licha ya kununua ving’amuzi.


Aidha, wamesema chaneli tano zilizopewa leseni na serikali kuendelea kurusha matangazo yao, nazo zinaonyesha chenga chenga.


Baadhi ya watu waliozungumza na gazeti hili jana, walidai kuwa mfumo huo umeleta usumbufu mkubwa kwao.


“Mimi mwenyewe nimekumbwa na tatizo hili tangu jana baada ya mitambo hiyo kuzimwa, sipati tena zile chaneli tano ambazo serikali ilisema ni lazima zionyeshwe ili Watanzania waendelee kuona hata kama vocha zao zitakuwa zimekwisha,” alisema mkazi mmoja wa jijini Dar es Salaam, ambaye hata hivyo, hakutaka jina lake liandikwe gazetini.


Alidai kwamba kituo cha TBC tu ndiyo kilikuwa kinaonyesha na kusema kuwa kama ndiyo hivyo, wananchi wengi watakosa matangazo.


Wakati wananchi hao wakitoa malalamiko yao, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa TCRA, Innocent Mungy, aliliambia NIPASHE kwa njia ya simu jana kuwa, kinachowafanya wananchi washindwe kupata matangazo ni wao wenyewe kushindwa kuunganisha ving’amuzi.


Mungy aliwataka wananchi kubadilika na kutumia mafundi wa kampuni zinazouza ving’amuzi badala ya wao wenyewe kujigeuza mafundi.


Mungy alisema huduma ya kufungiwa king’amuzi inatolewa bure na hakuna haja ya mtu kupanda juu ya nyumba yake na kuanza kufunga bila kujua anachokifunga.


“Kila kitu kinaenda vizuri na jana tulizunguka maeneo mbalimbali kuangalia zoezi hili na tumebaini tatizo kuwa ni watu hawajui kufunga hivi ving’amuzi,’’ alisema Mungy.


Juzi, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Profesa John Nkoma, wakati akizungumza na waandishi wa habari, alisema hata kama mitambo hiyo itazimwa, lakini chaneli tano za hapa nchini zitaendelea kurusha matangazo yake kama kawaida.


DAR WAGOMBEA VING'AMUZI
Wakati zoezi la kuhamia dijitali likiendelea, jana mamia ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam walifurika katika maduka mbalimbali ya mawakala wa kampuni ya Star Times kuendelea kununua ving’amuzi kwa ajili ya televisheni zao.
Hata hivyo, baadhi ya wakazi hao walikosoa huduma zilizokuwa zikitolewa na mawakala hao kwa madai kwamba hazikidhi kiwango kinachotakiwa.


Wakizungumza na NIPASHE kwa nyakati tofauti, walieleza kwamba baada ya kuweka ving'amuzi kwenye televisheni zao, pamekuwa pakijitokeza tatizo la picha na sauti hasa kwa wale waliolipia chaneli chache.


Mmoja wa wananchi hao, Esther Msigwa, alisema kuwa tangu amenunua king’amuzi chake, hajakitumia kutokana na matatizo kama hayo.


“King'amuzi kinasumbua, sipati picha wala sauti, vile vile tuliambiwa bei yake ni Sh. 39,000, lakini tunauziwa Sh. 48,000," alisema.


Akijibu tuhuma hizo, Afisa Masoko wa kampuni ya Star Times, Erick Cyprian, alisema watu walinukuu vibaya kuhusiana na suala la punguzo la manunuzi kwa kipindi cha kuelekea sikukuu.


“Punguzo la manunuzi ya king'amuzi halihusiani na muda wa hewani, hivyo wengi wao wanadhani wakishanunua king'amuzi kwa bei ya Sh. 39,0000, watapata muda wa maongezi moja kwa moja,” alisema Cyprian.


Hata hivyo, jitihada za NIPASHE za kuwatafuta viongozi wa DSTV kueleza namna walivyojipanga kuonyesha matangazo ya chaneli za ndani zilishindikana.


Simu ya Ofisa Mawasiliano, wake, Barbara Kambogi, ilikuwa inaita bila kupokelewa.

HABARI NA RICHARD MAKORE
CHANZO: NIPASHE

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

Coastal ipo tayari kuanza ligi kuu, yashinda 3-0 ikiwa kambini Moshi.

Wachezaji wa Coastal Union wakifanya mazoezi mepesi muda mfupi kabla ya kukabiliana na Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini Moshi, anayeonekana pichani mwenye jezi namba 17 ni haruna Moshi 'Boban'. Mtokeo ya mechi hiyo ni ushindi wa 3-0 kwa Wagosi. Mazoezi yamekolea, uwanja wa Ushirika Moshi. Uhuru Suleiman amesifiwa na kocha kuwa ni kiungo mwenye kasi nyingi na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira. Mshambuliaji anayetumia mguu wa kushoto kutoka Uganda, Yayo Lutimba Kato amefunga bao lake la kwanza tangu kujiunga na Coastal Union ambayo imeweka kambi mjini Moshi tangu jana. Kato ambaye ametoka URA inayoshiriki ligi kuu nchini Uganda, alipatia timu yake bao la kuongoza dhidi ya Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini humo, bao hilo alilifunga kwa ufundi mkubwa katika kipindi cha pili baada ya kupokea pasi murua na kupiga shuti kali akiwa nje ya 18. Akitoa taarifa kutoka Moshi, mwenyekiti wa Wagosi Hemed Hilal ‘Aurora’ amesema “Katika dakika za lal...

Tuhuma nzito : Magufuli, Mwakyembe, Lukuvi kufikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge

Dk John Magufuli   Dar es Salaam.   Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imesema itawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akiwatuhumu kwa kulidanganya Bunge. Hatua hiyo ilitangazwa jana na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe baada ya kumhoji Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert Mrango kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka wa fedha 2011/2012. Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo kiasi cha Sh348,075,000,000 fedha za ndani zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililotajwa kuwa ni la mradi maalumu (Special Road Construction Project) hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni. “Ni vizuri leo uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. T...