Skip to main content

Coastal ipo tayari kuanza ligi kuu, yashinda 3-0 ikiwa kambini Moshi.

Wachezaji wa Coastal Union wakifanya mazoezi mepesi muda mfupi kabla ya kukabiliana na Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini Moshi, anayeonekana pichani mwenye jezi namba 17 ni haruna Moshi 'Boban'. Mtokeo ya mechi hiyo ni ushindi wa 3-0 kwa Wagosi.
Mazoezi yamekolea, uwanja wa Ushirika Moshi.
Uhuru Suleiman amesifiwa na kocha kuwa ni kiungo mwenye kasi nyingi na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira.


Mshambuliaji anayetumia mguu wa kushoto kutoka Uganda, Yayo Lutimba Kato amefunga bao lake la kwanza tangu kujiunga na Coastal Union ambayo imeweka kambi mjini Moshi tangu jana.
Kato ambaye ametoka URA inayoshiriki ligi kuu nchini Uganda, alipatia timu yake bao la kuongoza dhidi ya Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini humo, bao hilo alilifunga kwa ufundi mkubwa katika kipindi cha pili baada ya kupokea pasi murua na kupiga shuti kali akiwa nje ya 18.
Akitoa taarifa kutoka Moshi, mwenyekiti wa Wagosi Hemed Hilal ‘Aurora’ amesema “Katika dakika za lala salama mchezaji Atupele Green, ambaye ameonyesha kiwango cha hali ya juu katika kipindi cha hivi karibuni aliipatia Coastal Union bao la pili kabla ya Danny Lyanga kumalizia la tatu na kukifanya kikosi cha Wagosi wa Kaya kuondokana na uhaba wa mabao ambapo tangu mechi ya kwanza ya kirafiki mpaka sasa haijawahi kupata ushindi wa bao zaidi ya moja.”
Kabla mpira kuisha mwamuzi wa mechi ya leo aliwapatia penati Wagosi baada ya mchezaji wao kuchezewa madhambi ndani ya eneo la hatari, lakini Yayo Kato alikosa penati hiyo na kuwanyima wenzake ushindi mnono wa 4-0.
Itakumbukwa mechi ya kwanza ya kirafiki walicheza na URA ya Uganda wakatoka na ushindi wa bao 1-0, mechi ya pili walishuka dimbani dhidi ya wekundu wa msimbazi Simba na kuibuka na ushindi wa bao 1-0, wakati mechi ya tatu walitoka suluhu ya 1-1 dhidi ya 3 Pillars ya Nigeria.
Aidha mechi ya nne ya kirafiki waliyocheza mjini Mombasa Kenya, walimaliza kwa suluhu ya 1-1, wakati mechi ya leo ni ya tano ya kirafiki kabla ya kuanza msimu wa ligi kuu ya soka Vodacom keshokutwa Agosti 24 jumamosi, ambapo Wagosi watafungua ligi mjii Arusha dhidi ya JKT Oljoro katika uwanja wa kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid.
Tukiweka kumbukumbu sawa tangu Coastal Union irudi kwenye ligi kuu ya soka Tanzania bara huu utakuwa ni msimu wa tatu ambapo msimu wa kwanza ilimaliza ikiwa imeshika nafasi ya tano, msimu wa pili ikashika nafasi ya sita wakati msimu huu wamedhamiria kufanya makubwa kutokana na aina ya kikosi walichonacho.
COASTAL UNION
AGOSTI 22, 2013
DAR ES SALAAM, TANZANIA

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

MAJINA YA WASHIRIKI NA WA WEZESHAJI WA FILM YA HOUSE GIRL!

CAST SELEMANI MOHAMED / BUNTO ANDREW / C-O YORAM MWETA / MGANGA MWANTUMU / MKE WA C-O JOHN / MCHUNGAJI BI FURURATU / JINI WAOMBOLEZAJI SAUMU HUSENI HASHIMU BABA RASTA MAN YOHANNA TAMILWAI SAIDI MWALUBADU SEMY STIR SELEMANI MOHAMEDI  AND ANDREW C-O LOCATION ATHUMANI HAMADI MAKE UP MWASHAMBA RAMADHANI BEDUI DEREVA DAUDI SPOONSER SAIDI SHABANI AND THE FRESH2012 GLOB SOUND PRODUCER J-B LIGHT YOHANNA TAMILWAI THENK YOU THE FRESH ENERTAINMENT AND THE FRESH2012 BLOG CONTACTS 0653785027 +255714091786 ZAIDI TEMBELEA www.the-fresh.blogspot.com ADRESS Thefresh@ymail.com AU Saidshabani60@gmai.com

Video: Blackchild – Put Inside

David Abdulichel, also known as BlackChild is a Ghanaian from Asanti origin, born and raised in Lagos Nigeria. BlackChild, who is a recording artist, song writer and performer started his music career back in 2000 and since then has released four singles. He has also worked with top producers in Nigeria such as Fliptyce, Spanky, Meca E & BrainMix to mention but few. BlackChild Abdul rose to prominence with his hit songs “Treasure”, “Ele” featuring Rock Steady, “Could It Be Love” featuring Cartiar, “All I Need” featuring Solid Star. This time around he comes out with “Put Inside” which sees him delivering lines in french and his native language and is steadily generating buzz and enjoying airplay on radio stations within and outside Lagos. Listen up!