Skip to main content

20 wauawa kwa shambulio Somalia


Moja ya mashambulio nchini Somalia

Karibu watu ishirini wameuawa katika shambulio la kujitoa mhanga kwenye kituo cha polisi nchini Somalia.
Shambulio hilo limetokea katika mji wa Beledweyne karibu na mpaka na Ethiopia. Mashuhuda wameiambia BBC kuwa gari lilipiga lango kuu la kuingia kwenye jengo la polisi na kulipuka kabla ya watu wenye silaha kushuka na kushambulia jengo hilo kwa risasi. Taarifa zinasema wengi waliofariki katika shambulio hilo ni maafisa wa polisi.

Wapiganaji wa kiislamu wa Al Shabaab wamekiri kuhusika na shambulio hilo. Mwezi uliopita wapiganaji hao wa Al Shabaab pia walikiri kuhusika na shambulio jingine ambapo watu 16 waliuawa katika hoteli moja maarufu mjini Mogadishu.Mwandishi wa habari wa BBC nchini Somalia Mohammed Moalimu amesema kituo hicho cha polisi kipo karibu na ngome ya majeshi ya Umoja wa mataifa yaliyopo nchini Somalia AMISOM.
Maafisa wa polisi nchini Somalia wamesema mlipuko huo ulikuwa ni mkubwa na umesababisha majeruhi kadhaa.
"Mlipuko ulikuwa ni mkubwa na pia wapo majeruhi kadhaa, hata hivyo hali imedhibitiwa," amesema Kanali Abdulkadir Ali, kamanda wa polisi wa mji huo wakati akiongea na shirika la habari la AFP.
Kamanda wa kundi la Al Shabaab Mohamed Abu Suleiman ameliambia shirika la AFP kuwa makomandoo wa Al Shabaab ndio waliofanya shambulio hilo.
Naye Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud amesema shambulilo hilo ni la kujimaliza na linaonyesha kutojali maisha.
"Kipau mbele changu cha kwanza ni kutuma salamu za rambi rambi kwa waathirika na familia zilizoguswa na tukio hilo la kipumbavu", alisema katika taarifa yake
"Nimesema ni shambulio la kipumbavu kwa sababu maadui zetu wanapaswa kuelewa kwamba mashambulizi hayatawasaidia kuendeleza harakati zao zaidi sana yanawapotosha"

Mwezi Septemba, kundi la Al Shabaab lilisema kuwa lilifanya shambulizi la kigaindi katika kituo cha biashara cha Westgate nchini Kenya ambapo watu wapatao 67 waliuawa.

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

DOWNLOAD BERRY BLACK FT. ALI KIBA - ISHARA ZANGU

Msanii Dr Leader afiwa na mke,

Pole sana Dr Leader Kwa msiba mzito wa kuondokewa na mke, mzazi mwenzio na mpendwa  wako. mungu akupe roho ya uvumilivu katika kipindi hiki kigumu. kila nafsi itaonja mauti.  mwenyezi mungu aiweke roho ya marahemu mahali pema peponi, You,  Selle Wamichanno  and  16 others  like this. Ally Mohamed   R.I.P SHEM.WE SASHA ALIKUWA AUMWA KWN AU? 9 hours ago  via  mobile  ·  Like Young Dutch Mahesabu   dah r.i.p shemeji yetu mpendwa ... natanguliza pole hiz kwa ndugu yetu dr.leader msambaa mungu akupe roho ya uvimilivu kwakipndi chote hki cha mpito 9 hours ago  via  mobile  ·  Like Baba Dailysuperstar   R.!.P 8 hours ago  via  mobile  ·  Like Rajab Kidagaa   R.I.P Xhem 8 hours ago  via  mobile  ·  Like Nick Regy   mung amlaze pem pepn 2ngulia n xx 2taft mpndw ri...