Skip to main content

CHADEMA TANGA YAPONGEZA UAMUZI WA KUVULIWA UONGOZI KATIBU MSAIDIZI












Na Oscar Assenga, Tanga

SIKU Chache baada ya Kamati kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo Taifa (Chadema) kuamua kumvua uongozi ndani ya chama hicho aliyekuwa katibu Msaidizi Zitto Kabwe chama hicho mkoani hapa kimeipongeza hatua hiyo kwa kusema italeta umakini mkubwa kwa viongozi waliobaki.

Uamuzi huo ulitolewa kwa mujibu ibara ya 7.7.16 kifungu (V) ambayo inaeleza kuwa kamati hiyo ina mamlaka ya kumwachisha ujumbe wa kamati kuu mjumbe mteule ambaye ataenda kinyume cha katiba, kanuni na maadili au kushindwa kukidhi matakwa ya kuteuliwa kwake.

Akizungumza na Tanga Raha,Katibu wa Chadema Mkoa wa Tanga,Jonathan Bahweje alisema suala hilo lilipaswa kufanywa na kamati hiyo kwa sababu ni sahihi kwa mtu yoyote anayekiuka kanuni na taratibu za uongozi ndani ya chama hicho.

Bahweje alisema hatua ya Zitto kukiri kuwa alikosea na kupewa adhabu ya siku kumi na nne kujitetea kwa kamati kuu ya chama hicho alitumia busara kubwa sana na kuwataka wanachama kuwa na utulivu wakati mchakato huo ukiendelea.

  “Maamuzi ya kamati kuu yaliyofanywa sidhani kama yanaweza kuingiliwa na upande mwengine hivyo napenda kuwaasa viongozi wa ngazi za chini kuacha kuingilia suala hilo kwani tayari limeshapata muafaka “Alisema Bahweje.

Alisema wanaiomba kamati kuu ya chama hicho kumaliza mgogoro uliopo huo mapema ili kuweza kujiandaa na uchaguzi mkuu wa serikali za mitaa mwaka 2014  kwani wamedhamiri kuhakikisha wanashinda katika chaguzi hizo.

Katibu huyo aliitaka kamati hiyo kukemea viongozi ambao wanapiga maamuzi yao kwani wao ndio chombo cha mwisho ambacho kinauwezo wa kufanya jambo lolote ambalo linaweza kuleta mgawanyiko ndani ya chama hicho.


   “Naishauri kamati kutumia nafasi yao kuwaonya viongozi kuanzia ngazi za chini na kuweza kuleta mshikamano wa pamoja ambao utaweza kuleta mafanikio katika chama chetu kwani uongozi imara ndio utakiwezesha kuwatumikia wananchi “Alisema Bahweje

Popular posts from this blog

Goog music from tng jojo yatakwisha hii apa

DownLoad Na Sikiliza Joint Mpya Ya Squizer Ft Belle 9 - Mtemi Pesa

MAJINA YA WASHIRIKI NA WA WEZESHAJI WA FILM YA HOUSE GIRL!

CAST SELEMANI MOHAMED / BUNTO ANDREW / C-O YORAM MWETA / MGANGA MWANTUMU / MKE WA C-O JOHN / MCHUNGAJI BI FURURATU / JINI WAOMBOLEZAJI SAUMU HUSENI HASHIMU BABA RASTA MAN YOHANNA TAMILWAI SAIDI MWALUBADU SEMY STIR SELEMANI MOHAMEDI  AND ANDREW C-O LOCATION ATHUMANI HAMADI MAKE UP MWASHAMBA RAMADHANI BEDUI DEREVA DAUDI SPOONSER SAIDI SHABANI AND THE FRESH2012 GLOB SOUND PRODUCER J-B LIGHT YOHANNA TAMILWAI THENK YOU THE FRESH ENERTAINMENT AND THE FRESH2012 BLOG CONTACTS 0653785027 +255714091786 ZAIDI TEMBELEA www.the-fresh.blogspot.com ADRESS Thefresh@ymail.com AU Saidshabani60@gmai.com