Skip to main content

CHADEMA TANGA YAPONGEZA UAMUZI WA KUVULIWA UONGOZI KATIBU MSAIDIZI












Na Oscar Assenga, Tanga

SIKU Chache baada ya Kamati kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo Taifa (Chadema) kuamua kumvua uongozi ndani ya chama hicho aliyekuwa katibu Msaidizi Zitto Kabwe chama hicho mkoani hapa kimeipongeza hatua hiyo kwa kusema italeta umakini mkubwa kwa viongozi waliobaki.

Uamuzi huo ulitolewa kwa mujibu ibara ya 7.7.16 kifungu (V) ambayo inaeleza kuwa kamati hiyo ina mamlaka ya kumwachisha ujumbe wa kamati kuu mjumbe mteule ambaye ataenda kinyume cha katiba, kanuni na maadili au kushindwa kukidhi matakwa ya kuteuliwa kwake.

Akizungumza na Tanga Raha,Katibu wa Chadema Mkoa wa Tanga,Jonathan Bahweje alisema suala hilo lilipaswa kufanywa na kamati hiyo kwa sababu ni sahihi kwa mtu yoyote anayekiuka kanuni na taratibu za uongozi ndani ya chama hicho.

Bahweje alisema hatua ya Zitto kukiri kuwa alikosea na kupewa adhabu ya siku kumi na nne kujitetea kwa kamati kuu ya chama hicho alitumia busara kubwa sana na kuwataka wanachama kuwa na utulivu wakati mchakato huo ukiendelea.

  “Maamuzi ya kamati kuu yaliyofanywa sidhani kama yanaweza kuingiliwa na upande mwengine hivyo napenda kuwaasa viongozi wa ngazi za chini kuacha kuingilia suala hilo kwani tayari limeshapata muafaka “Alisema Bahweje.

Alisema wanaiomba kamati kuu ya chama hicho kumaliza mgogoro uliopo huo mapema ili kuweza kujiandaa na uchaguzi mkuu wa serikali za mitaa mwaka 2014  kwani wamedhamiri kuhakikisha wanashinda katika chaguzi hizo.

Katibu huyo aliitaka kamati hiyo kukemea viongozi ambao wanapiga maamuzi yao kwani wao ndio chombo cha mwisho ambacho kinauwezo wa kufanya jambo lolote ambalo linaweza kuleta mgawanyiko ndani ya chama hicho.


   “Naishauri kamati kutumia nafasi yao kuwaonya viongozi kuanzia ngazi za chini na kuweza kuleta mshikamano wa pamoja ambao utaweza kuleta mafanikio katika chama chetu kwani uongozi imara ndio utakiwezesha kuwatumikia wananchi “Alisema Bahweje

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

MAJINA YA WASHIRIKI NA WA WEZESHAJI WA FILM YA HOUSE GIRL!

CAST SELEMANI MOHAMED / BUNTO ANDREW / C-O YORAM MWETA / MGANGA MWANTUMU / MKE WA C-O JOHN / MCHUNGAJI BI FURURATU / JINI WAOMBOLEZAJI SAUMU HUSENI HASHIMU BABA RASTA MAN YOHANNA TAMILWAI SAIDI MWALUBADU SEMY STIR SELEMANI MOHAMEDI  AND ANDREW C-O LOCATION ATHUMANI HAMADI MAKE UP MWASHAMBA RAMADHANI BEDUI DEREVA DAUDI SPOONSER SAIDI SHABANI AND THE FRESH2012 GLOB SOUND PRODUCER J-B LIGHT YOHANNA TAMILWAI THENK YOU THE FRESH ENERTAINMENT AND THE FRESH2012 BLOG CONTACTS 0653785027 +255714091786 ZAIDI TEMBELEA www.the-fresh.blogspot.com ADRESS Thefresh@ymail.com AU Saidshabani60@gmai.com

Video: Blackchild – Put Inside

David Abdulichel, also known as BlackChild is a Ghanaian from Asanti origin, born and raised in Lagos Nigeria. BlackChild, who is a recording artist, song writer and performer started his music career back in 2000 and since then has released four singles. He has also worked with top producers in Nigeria such as Fliptyce, Spanky, Meca E & BrainMix to mention but few. BlackChild Abdul rose to prominence with his hit songs “Treasure”, “Ele” featuring Rock Steady, “Could It Be Love” featuring Cartiar, “All I Need” featuring Solid Star. This time around he comes out with “Put Inside” which sees him delivering lines in french and his native language and is steadily generating buzz and enjoying airplay on radio stations within and outside Lagos. Listen up!