Skip to main content

CINDY RULZ:- WASANII WA KIKE WANAOIMBA RNB WAMEANZA KUELEWEKA LAKINI NA HIPHOP HAITOCHUKUA MUDA KUELEWEKA BONGO



Rapper toka Bongo CORRINE MARY a.k.a CINDY RULZ ametoa pongezi na shukurani zake za dhati kwa wasanii wenzake wa kike ambao humpa ushirikiano kwa kuzisambaza nyimbo zake mpya mara kwa mara katika mitandao ya kijamii na media mbalimbali.




Akipiga Stori na kipengele cha Chumba Cha Sindano kupitia kipindi cha Kali za Bomba hapa Bomba FM Mbeya, hitmaker huyo wa Unstoppable, Party ya Cindy na Lets wait CINDY RULZ amesema licha ya muziki wa hiphop bongo kuwa na wadau wachache wanaousapoti lakini anatambua fika haitochukua muda muziki huo kuteka mashabiki wengi kutokana na kufuata misingi.




“Sasa hivi nachoshukuru Mungu ni kwamba wako more supportive wote female rappers ambao nawafahamu kawa wapo CHIKU K kuna DIVAwote tumekuwa response, maana nakumbuka hata nilipotoa hii Cover, isitoshe ali-post kwenye mitandao yake ya kijamii, CHIKU K alikuwa anaandika Status yaani ndo iko hivyo. Kwa sasa hivi tupo pamoja zaidi tunaandaa kitu kwa pamoja wote sisi sote wanne kwa hiyo siwezi kusema ni competition zaidi tunajitahidi kujisukuma sisi wenyewe ka wenyewe, lakini ukiangalia hao wengine sijui wanaoimba RNB  nini naweza nikasema kwamba it nice wameanza kueleweka zaidi kuliko sisi na sisi ndiko tunakoelekea” alisema CINDY RULZ




Kwa hatua nyingine Rapper CINDY RULZ ameweza kuelezea mikakati na ahadi alizopewa baada ya ngoma ya Lets Wait aliyomshirikisha DUNGAkuwekwa kwenye tovuti ya kimataifa www.hotnewhiphop.com na blogs mbili za Dearth Chambers na Grime Culture na kueleza furaha yake “(Anaanza kwa kucheka) kwanza sikutegemea kabisa kwa sababu unajua na-rap kwa Kiswahili  kwa hiyo ni tofauti kwa huko kuweza kuelewa hiyo lugha, lakini nacho shukuru Mungu  ndo hivyo walinitumia email wakasema wamependa quality ya nyimbo hata kama wao walikuwa wao walikuwa hawaelewi naongea nini, lakini delivery yangu iliwafurahisha niweze kusema kwa hiyo wakasema watakuwa wananisapoti  niendelee kutuma nyimbo zangu huko”.
BOFYA HAPA CHINI KUSIKILIZA MAHOJIANO ZAIDI. 

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

Coastal ipo tayari kuanza ligi kuu, yashinda 3-0 ikiwa kambini Moshi.

Wachezaji wa Coastal Union wakifanya mazoezi mepesi muda mfupi kabla ya kukabiliana na Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini Moshi, anayeonekana pichani mwenye jezi namba 17 ni haruna Moshi 'Boban'. Mtokeo ya mechi hiyo ni ushindi wa 3-0 kwa Wagosi. Mazoezi yamekolea, uwanja wa Ushirika Moshi. Uhuru Suleiman amesifiwa na kocha kuwa ni kiungo mwenye kasi nyingi na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira. Mshambuliaji anayetumia mguu wa kushoto kutoka Uganda, Yayo Lutimba Kato amefunga bao lake la kwanza tangu kujiunga na Coastal Union ambayo imeweka kambi mjini Moshi tangu jana. Kato ambaye ametoka URA inayoshiriki ligi kuu nchini Uganda, alipatia timu yake bao la kuongoza dhidi ya Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini humo, bao hilo alilifunga kwa ufundi mkubwa katika kipindi cha pili baada ya kupokea pasi murua na kupiga shuti kali akiwa nje ya 18. Akitoa taarifa kutoka Moshi, mwenyekiti wa Wagosi Hemed Hilal ‘Aurora’ amesema “Katika dakika za lal...

Tuhuma nzito : Magufuli, Mwakyembe, Lukuvi kufikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge

Dk John Magufuli   Dar es Salaam.   Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imesema itawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akiwatuhumu kwa kulidanganya Bunge. Hatua hiyo ilitangazwa jana na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe baada ya kumhoji Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert Mrango kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka wa fedha 2011/2012. Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo kiasi cha Sh348,075,000,000 fedha za ndani zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililotajwa kuwa ni la mradi maalumu (Special Road Construction Project) hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni. “Ni vizuri leo uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. T...