Skip to main content

Mashine za kodi TRA ni wazo lililochelewa

Mamlaka ya Mapato Tanzania iko katika msuguano na wafanyabiashara katika maeneo mbalimbali nchini kutokana na mamlaka hiyo kuanzisha mfumo mpya wa utoaji stakabadhi za kielektroniki kwa kutumia mashine ziitwazo EFD.
Ugomvi mkubwa wa wafanyabiashara hao unatokana na bei inayodaiwa ni kubwa ya kununulia mashine hizo, inayofikia Sh800, 000 kwa kila moja. Madai mengine ni kasoro za kiufundi za mashine hizo na kitendo cha TRA kutumia mzabuni mmoja kuingiza mashine hizo.
Jana mvutano huo ulipiga hodi katika eneo maarufu kibiashara la Kariakoo jijini Dar es Salaam ambapo wafanyabiashara waligoma kufungua maduka kama ambavyo wamekwishafanya wenzao katika mikoa ya Mbeya na Morogoro.
Pamoja na ufafanuzi wa TRA kwamba baada ya majadiliano na wafanyabiashara bei za mashine za EFD zimepungua hadi Sh600, 000 kwa kila moja, bado muafaka kamili haujafikiwa.Tunaafikiana na ushauri unaotolewa na TRA kwamba mvutano huo umalizwe kwa amani kwa njia ya mazungumzo na majadiliano baina ya mamlaka hiyo na wafanyabiashara badala ya njia waliyoichagua ya migomo na maandamano.
Tunaishauri TRA iendelee kutoa majibu sahihi na kusisitiza umuhimu wa mashine hizo, huku ikitambua kwamba hakuna mfanyabiashara anayelipa kodi akicheka, hivyo iwe imara kusimamia mfumo huo mpya bila kuingiza ujanja ujanja unaoweza kuikwamisha.
Kinachojitokeza bayana hapa ni kuwapo mawasiliano hafifu baina ya TRA na wafanyabiashara. Kwa mfano, wafanyabiashara bado wanadhani ni kampuni moja tu iliyopewa tenda ya kusambaza mashine hizo, wakati ni kampuni 11 zilizopewa tenda hiyo. Hakika, tatizo ni mawasiliano na TRA lazima ikiri udhaifu huo na kuchukua hatua stahiki.
Uanzishaji wa mashine za EFD ni mkakati sahihi wa ukusanyaji na usimamizi wa kodi, hasa katika maeneo ambayo TRA haikuwa inayafikia. Ni uamuzi ambao utaliwezesha Taifa letu kupata fedha za kutosha kujenga miundombinu na kuwaletea wananchi maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Tunashawishika kuamini kuwa, hata mafanikio ambayo TRA iliyaeleza wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Mlipakodi ya kuimarika kwa ukusanyaji mapato kutoka Sh4,049.1 trilioni mwaka 2008/09 hadi Sh7,739.3 trilioni mwaka 2012/13, yamesaidiwa na mashine hizo.
Kwa muda mrefu tumekuwa tukikemea uzembe na usimamizi mbovu wa kodi uliosababisha maofisa wa TRA kuacha fedha nyingi zikilala kwa wafanyabishara wa kati, badala yake kila kukicha wakawa wanakimbilia makusanyo ya kuokota yanayotokana na mishahara ya wafanyakazi.
Kwa mfano, tumewahi kushauri kuwa vinahitajika vyanzo vipya vya mapato, kwa kuwatambua na kuwatoza wafanyabiashara wa kada ya kati katika maduka, baa, saluni, bucha za nyama, kumbi za starehe na harusi na maeneo kama hayo.
Mbali na kuongeza mapato, pia tunadhani Serikali ingefanya juhudi za kuziba matundu na mianya ya uvujaji wa mapato yake ili kuhakikisha kila kinachokusanywa kinaelekezwa katika maendeleo ya nchi na wananchi, badala ya kutafunwa na mchwa wasiojali masilahi ya umma.
Hatuna shaka kwamba TRA ikijipanga inaweza kukusanya mapato zaidi, hasa ikisimamia vizuri uamuzi wake wa kutumia EFD nchini kote na kuweka utaratibu wa kudumu wa kufuatilia kwenye maduka kuona iwapo wanatoa risiti hizo au la, maana tayari kuna madai kuwa wateja wanatakiwa kuchagua kati ya kuuziwa bidhaa kwa bei ndogo bila risiti au kwa bei kubwa na risiti za kielekroniki.

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

Coastal ipo tayari kuanza ligi kuu, yashinda 3-0 ikiwa kambini Moshi.

Wachezaji wa Coastal Union wakifanya mazoezi mepesi muda mfupi kabla ya kukabiliana na Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini Moshi, anayeonekana pichani mwenye jezi namba 17 ni haruna Moshi 'Boban'. Mtokeo ya mechi hiyo ni ushindi wa 3-0 kwa Wagosi. Mazoezi yamekolea, uwanja wa Ushirika Moshi. Uhuru Suleiman amesifiwa na kocha kuwa ni kiungo mwenye kasi nyingi na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira. Mshambuliaji anayetumia mguu wa kushoto kutoka Uganda, Yayo Lutimba Kato amefunga bao lake la kwanza tangu kujiunga na Coastal Union ambayo imeweka kambi mjini Moshi tangu jana. Kato ambaye ametoka URA inayoshiriki ligi kuu nchini Uganda, alipatia timu yake bao la kuongoza dhidi ya Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini humo, bao hilo alilifunga kwa ufundi mkubwa katika kipindi cha pili baada ya kupokea pasi murua na kupiga shuti kali akiwa nje ya 18. Akitoa taarifa kutoka Moshi, mwenyekiti wa Wagosi Hemed Hilal ‘Aurora’ amesema “Katika dakika za lal...

Tuhuma nzito : Magufuli, Mwakyembe, Lukuvi kufikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge

Dk John Magufuli   Dar es Salaam.   Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imesema itawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akiwatuhumu kwa kulidanganya Bunge. Hatua hiyo ilitangazwa jana na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe baada ya kumhoji Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert Mrango kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka wa fedha 2011/2012. Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo kiasi cha Sh348,075,000,000 fedha za ndani zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililotajwa kuwa ni la mradi maalumu (Special Road Construction Project) hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni. “Ni vizuri leo uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. T...