Skip to main content

WACHEZAJI KIKAPU TANGA WAOMBA MSAADA WA KUIPELEKA TIMU MBEYA.

Mkoa wa Tanga, mabingwa watetezi wa michuano ya taifa ya kikapu (Taifa Cup) kwa mwaka jana, bado hawajathibitisha ushiriki wao katika michuano ya mwaka huu kutokana na ukata wa fedha. 

Habari zinasema mpaka sasa timu yao inafanya mazoezi bila matumaini ya kuelekea mjini Mbeya itakapofanyika michuano hiyo kwa mwaka huu mwishoni mwa mwezi wa 11.

“Michuano hii ya kikapu taifa kwa mwaka jana ilifanyika mkoani hapa (Tanga), hivyo ikawa rahisi kwetu kuweka kambi na kupata mahitaji mengine, ndiyo maana tukaibuka mabingwa, lakini mwaka huu hali katika kambi si nzuri kwani bajeti inatubana mpaka sasa hatujui mustakabali wetu,” afisa  wa timu hiyo alisema.

Kwa mujibu wa barua iliyoandikwa na Katibu Mkuu wa chama cha mpira wa kikapu mkoa wa Tanga (TRBA), Carlistus Zakaria timu hiyo inahitaji kiasi cha Sh mil 11, ili kuweza kusafiri mpaka Mbeya. Vilevile kiasi hicho cha fedha kitaweza kuhudumia kambia kwa malazi na chakula pamoja na vifaa vya michezo kwa muda wote watakaokuwa Mbeya.

“Timu yetu ina wachezaji 24 Wavulana na Wasichana pamoja na viongozi wanane hivyo kufanya idadi ya watu 32, tunahitaji kiasi cha Sh mil 3.5 za nauli kuenda na kurudi, Sh mil 5.2 za chakula kwa siku zote tutakazokuwa Mbeya pamoja na Sh mil 8.8 za vifaa vya michezo na fedha za dharura,” ilisema sehemu ya barua hiyo.

Aidha kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari ambacho kimetaka hifadhi ya jina lake mpaka sasa Mkoa wa Tanga, haujaonyesha nia ya kuwasaidia mbali ya kuwapelekea barua kutoka Shirikisho la Mpira wa Kikapu Tanzania (TBF), ambayo inaweka wazi kila kitu juu ya ushiriki wetu.

“Kinachotutia uchungu juu ya kupuuzwa huku ni kuwa, mwaka jana tulipouletea heshima Mkoa wetu kila mtu alitusifia, lakini hawakujua kama vizuri vyataka gharama.

Sasa ili tuendelee kuuletea vikombe mkoa wetu tunawaomba wadau wa mchezo huu watusaidie tufike Mbeya.

“Tumeamua hatuhitaji fedha, hata wakitokea watu wakitudhamini usafiri, wengine wakatupa vifaa na wengine wakatuhakikishia chakula hatuna matatizo.

Kikubwa tunahitaji kushiriki michuano hii kwa hali na mali, tukishindwa kushiriki itakuwa aibu kubwa kwa mkoa wetu,” kilisema chanzo hicho.

Hata hivyo, kwa mujibu wa barua ya TBF, iliyotolewa Aprili mwaka huu na kutiwa saini na Katibu Mkuu Msaidizi wa shirikisho hilo Michael Maluwe, imeweka wazi kuwa Serikali ya Mkoa inawajibika moja kwa moja kuhakikisha timu hizo zinashiriki michuano ya Taifa Cup.

“Ni wajibu wa kila mkoa kuhakikisha unawajibika katika maandalizi na kuipeleka timu ya mkoa kwenye kituo cha mashindano,” imesema sehemu ya barua hiyo na kuongeza kuwa. “Mambo muhimu ya kuzingatia ni gharama za nauli kwa timu, gharama za malazi na chakula vilevile usafiri wa ndani, posho na ada ya ushiriki ambayo ni Sh 100,000.”

Aidha timu ya kikapu ya Tanga imeweka wazi kuwa mtu binafsi, kampuni ama taasisi ambayo itaguswa na matatizo ya kambi hiyo, ambayo inapigana kuhakikisha inatetea ubingwa wake ilioupata mwaka jana wanafungua milango kupokea msaada wowote utakaowawezesha kuishi mjini Mbeya kuanzia Novemba 30 mpaka Disemba 8 mwaka huu itakapokamilika michuano hiyo.

Wamebainisha kuwa wapo tayari kutangaza biashara ya mfadhili yeyote atakayewasaidia ama mtu aliyeguswa anaweza kuwatumia fedha katika akaunti ya benki namba 4172506984 NMB Bank (badaraka Branch).

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

Coastal ipo tayari kuanza ligi kuu, yashinda 3-0 ikiwa kambini Moshi.

Wachezaji wa Coastal Union wakifanya mazoezi mepesi muda mfupi kabla ya kukabiliana na Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini Moshi, anayeonekana pichani mwenye jezi namba 17 ni haruna Moshi 'Boban'. Mtokeo ya mechi hiyo ni ushindi wa 3-0 kwa Wagosi. Mazoezi yamekolea, uwanja wa Ushirika Moshi. Uhuru Suleiman amesifiwa na kocha kuwa ni kiungo mwenye kasi nyingi na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira. Mshambuliaji anayetumia mguu wa kushoto kutoka Uganda, Yayo Lutimba Kato amefunga bao lake la kwanza tangu kujiunga na Coastal Union ambayo imeweka kambi mjini Moshi tangu jana. Kato ambaye ametoka URA inayoshiriki ligi kuu nchini Uganda, alipatia timu yake bao la kuongoza dhidi ya Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini humo, bao hilo alilifunga kwa ufundi mkubwa katika kipindi cha pili baada ya kupokea pasi murua na kupiga shuti kali akiwa nje ya 18. Akitoa taarifa kutoka Moshi, mwenyekiti wa Wagosi Hemed Hilal ‘Aurora’ amesema “Katika dakika za lal...

Tuhuma nzito : Magufuli, Mwakyembe, Lukuvi kufikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge

Dk John Magufuli   Dar es Salaam.   Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imesema itawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akiwatuhumu kwa kulidanganya Bunge. Hatua hiyo ilitangazwa jana na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe baada ya kumhoji Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert Mrango kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka wa fedha 2011/2012. Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo kiasi cha Sh348,075,000,000 fedha za ndani zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililotajwa kuwa ni la mradi maalumu (Special Road Construction Project) hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni. “Ni vizuri leo uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. T...