Skip to main content

WANANCHI KOROGWE WAUKATAA MRADI WA UMWAGILIAJI


Korogwe

WANANCHI wa Kijiji cha Mswaha Darajani Kata ya Mswaha wilayani Korogwe mkoani Tanga wamekataa kuupokea mradi wa umwagiliaji wa kijiji hicho kwa madai ya kujengwa chini ya kiwango.
 
Hatua ya wananchi hao waliiweka bayana katika mkutano wa kijiji hicho  ambao ulifanyika Novemba 7 mwaka huu katika mradi huo uligharimu zaidi ya milioni 42 kuanzia hatua za awali mpaka mwisho.
 
Kilichopelekea mradi huo kukataliwa na wananchi hao mbele ya diwani wa Kata hiyo,Aweso Omari ambaye aliambatana na Afisa Mtendaji wa Kata hiyo Paulo Mzava kilitokana na ukuta wa kukingia maji uliojengwa kumepasuka na hivyo kushindwa kutumika licha ya kugharimu fedha hizo.
 
Akizungumza katika mkutano hao mmoja ya wananchi hao ,Juma Mussa alisema wanamuomba mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kuwapelekea wataalamu ili waangalie jinsi mradi huo ulivyohujumiwa ikiwemo kuchukuliwa hatua wahusika.
 
   “Ninaamini endapo Mkurugenzi wa Halamshauri atakuja kuangalia mradi huo yatapatikana mafanikio ikiwemo kulipatia ufumbuzi suala la mradi huo “Alisema Mussa.
 
Mussa alifika mbali zaidi kwa kumuomba mkuu wa wilaya ya Korogwe,Mrisho Gambo kutembelea eneo hilo ili ajionee jinsi mradi huo ulivyoharibika na kushindwa kufanya kazi huku wananchi wakiendelea kuteseka.
 
Akizungumzia mradi huo,Diwani Aweso alisema mradi huo ulitengewa sh.milioni 35kwa ajili ya utengenezaji huo wa mradi ambao ulipagwa kutumika kwenye shughuli za umwagiliaji kwenye mbuga ya mswaha darajani.
 
  “Baada ya kuchelewa kwa mradi huo nililazimika kumtafuta diwani wa kata hiyo Aweso ambapo alinijibu kuwa mradi huo utapasuka muda wowote ule kutokana na kujengwa chini ya kiwango“Alisema Aweso wakati akizungumza na mwandishi wa gazeti hili.
 
Aweso alisema mkandarasi aliyepewa kujenga mradi huo alijenga chini ya kiwango hali ambayo ilipelekea kushindwa kufanya kazi ipasavyo badala yake kupasuka na kuendelea kuwapa tabu wananchi wa maeneo hayo.

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

Coastal ipo tayari kuanza ligi kuu, yashinda 3-0 ikiwa kambini Moshi.

Wachezaji wa Coastal Union wakifanya mazoezi mepesi muda mfupi kabla ya kukabiliana na Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini Moshi, anayeonekana pichani mwenye jezi namba 17 ni haruna Moshi 'Boban'. Mtokeo ya mechi hiyo ni ushindi wa 3-0 kwa Wagosi. Mazoezi yamekolea, uwanja wa Ushirika Moshi. Uhuru Suleiman amesifiwa na kocha kuwa ni kiungo mwenye kasi nyingi na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira. Mshambuliaji anayetumia mguu wa kushoto kutoka Uganda, Yayo Lutimba Kato amefunga bao lake la kwanza tangu kujiunga na Coastal Union ambayo imeweka kambi mjini Moshi tangu jana. Kato ambaye ametoka URA inayoshiriki ligi kuu nchini Uganda, alipatia timu yake bao la kuongoza dhidi ya Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini humo, bao hilo alilifunga kwa ufundi mkubwa katika kipindi cha pili baada ya kupokea pasi murua na kupiga shuti kali akiwa nje ya 18. Akitoa taarifa kutoka Moshi, mwenyekiti wa Wagosi Hemed Hilal ‘Aurora’ amesema “Katika dakika za lal...

Tuhuma nzito : Magufuli, Mwakyembe, Lukuvi kufikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge

Dk John Magufuli   Dar es Salaam.   Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imesema itawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akiwatuhumu kwa kulidanganya Bunge. Hatua hiyo ilitangazwa jana na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe baada ya kumhoji Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert Mrango kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka wa fedha 2011/2012. Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo kiasi cha Sh348,075,000,000 fedha za ndani zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililotajwa kuwa ni la mradi maalumu (Special Road Construction Project) hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni. “Ni vizuri leo uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. T...