Skip to main content

BOBAN ARIPOTI COASTAL UNION TANGA.

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam 

KIUNGO mshambuliaji wa timu ya Coastal Union yenye maskani jijini Tanga, Haruna Moshi ‘Boban’, ameripoti mkoani Tanga kwa ajili ya kuanza mazoezi ya kujiandaa na mzunguuko wa pili wa ligi ya Tanzania Bara.
 
 
Haruna Moshi Boban pichani.
Kuripoti kwa Boban kunashusha presha kutoka kwa wadau wa timu hiyo wanaosema kuwa kiungo huyo amekuwa mtovu wa nidhamu kwa kuchelewa kuripoti kambini.
 
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Msemaji wa timu ya Coastal Union, Hafidh Kido, alisema kuwa Boban aliafiki kujiunga na wenzake mapema wiki hii ili kuendelea na mazoezi ya pamoja.
 
Alisema kuwa kujiunga na wenzake katika maandalizi ya michuano ya Vodacom ni sehemu ya kujiweka sawa zaidi.
 
“Baada ya kumaliza ratiba yake kama alivyotoa taarifa kwa viongozi wake, Boban amejiunga na wenzake.
 
“Tunaamini mambo yatakuwa mazuri kwa kiungo huyo ambaye uwezo wake hapana shaka unajulikana na kuheshimika sana,” alisema.
 
Boban ni miongoni mwa wachezaji wanaoheshimika katika soka hapa nchini, huku uwezo wake ukiweza kufanya makubwa awapo uwanjani.

Popular posts from this blog

NEW JOINT | dayna special nipe nafasi {Audio}

Goog music from tng jojo yatakwisha hii apa

DownLoad Na Sikiliza Joint Mpya Ya Squizer Ft Belle 9 - Mtemi Pesa