Skip to main content

Boban ni mchezaji halali wa CUSC

 Kikosi cha maangamizi cha CUSC....

 Hiki ni kipande cha gazeti la leo Jumatano Januari 1,2014 gazeti Mtanzania kuhusu habari za Boban.



Haruna Moshi, akimiliki mpira katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha wakati akiitumikia CUSC kwenye mechi yake ya kwanza ligi kuu na Wagosi wa Kaya. Ilikuwa ni mechi dhidi ya Oljoro JKT, ambapo CUSC iliibuka na ushindi wa mabao 2-0.
 
Ndugu zangu,
WIKI hii kumekuwa na habari za upotoshaji juu ya kutimuliwa kwa kiungo mshambuliaji wa Coastal Union ‘Wagosi wa Kaya’, Haruna Moshi ‘Boban’.
Ninaziita habari za upotoshaji kwasababu hazina ukweli, na mara nyingine mtu anaweza kuenda mbali zaidi na kufikiri kuwa kuna hujuma zinafanyika dhidi ya timu yetu ili wachezaji wasicheze kwa moyo wakati wa mzunguko wa pili wa ligi kuu ya Tanzania Bara, unaotarajiwa kuanza Januari 25 mwaka huu.
Gazeti moja la michezo, jina tunalihifadhi limeripoti likimnukuu kiongozi mmoja wa Wagosi wa Kaya, jina pia tunalihifadhi kutokana na heshima yake; kuwa Coastal Union haina mpango wa kumuongezea mkataba ‘Boban’ baada ya kumalizika miezi sita ijayo kwasababu za utovu wa nidhamu.
Habari hizo hazina ukweli kwasababu hakuna kikao kilichokaliwa kujadili mustakabali wa mchezaji huyo. Ni kweli Boban, hajaripoti kambini mpaka sasa; lakini uongozi wa juu akiwemo meneja wa timu unazo taarifa za mchezaji huyo.
Kuwa na nidhamu ama kutokuwa na nidhamu, kumtimua ama kumuacha mchezaji, wanaoamua hayo ni uongozi wa juu kupitia kamati zake ndogondogo kama za mashindano, usajii na nidhamu. Na si mtu mmoja mmoja.
Hivyo kwa niaba ya Mwenyekiti wa Coastal Union, Hemed Hilal ‘Aurora’ timu inaomba radhi wanachama wa CUSC, kutokana na kuumizwa kwa namna moja ama nyingine na taarifa hizo za upotoshwaji.
Wagosi wa Kaya, bado wana mkataba wa miezi sita na Boban, kuongezewa ama kutoongezewa mkataba suala hilo litajadiliwa kati ya mchezaji na viongozi pale utakapofika ukingoni.
HAFIDH A. KIDO
MSEMAJI CUSC
JANUARI 1, 2014
DAR ES SALAAM, TANZANIA

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

Coastal ipo tayari kuanza ligi kuu, yashinda 3-0 ikiwa kambini Moshi.

Wachezaji wa Coastal Union wakifanya mazoezi mepesi muda mfupi kabla ya kukabiliana na Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini Moshi, anayeonekana pichani mwenye jezi namba 17 ni haruna Moshi 'Boban'. Mtokeo ya mechi hiyo ni ushindi wa 3-0 kwa Wagosi. Mazoezi yamekolea, uwanja wa Ushirika Moshi. Uhuru Suleiman amesifiwa na kocha kuwa ni kiungo mwenye kasi nyingi na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira. Mshambuliaji anayetumia mguu wa kushoto kutoka Uganda, Yayo Lutimba Kato amefunga bao lake la kwanza tangu kujiunga na Coastal Union ambayo imeweka kambi mjini Moshi tangu jana. Kato ambaye ametoka URA inayoshiriki ligi kuu nchini Uganda, alipatia timu yake bao la kuongoza dhidi ya Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini humo, bao hilo alilifunga kwa ufundi mkubwa katika kipindi cha pili baada ya kupokea pasi murua na kupiga shuti kali akiwa nje ya 18. Akitoa taarifa kutoka Moshi, mwenyekiti wa Wagosi Hemed Hilal ‘Aurora’ amesema “Katika dakika za lal...

Tuhuma nzito : Magufuli, Mwakyembe, Lukuvi kufikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge

Dk John Magufuli   Dar es Salaam.   Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imesema itawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akiwatuhumu kwa kulidanganya Bunge. Hatua hiyo ilitangazwa jana na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe baada ya kumhoji Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert Mrango kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka wa fedha 2011/2012. Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo kiasi cha Sh348,075,000,000 fedha za ndani zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililotajwa kuwa ni la mradi maalumu (Special Road Construction Project) hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni. “Ni vizuri leo uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. T...