Skip to main content

Wasanii wanunua stika kwa pauni ya England

Dar es Salaam. Tasnia ya sanaa imeendelea kuandamwa na changamoto nyingi ikiwamo wasanii kununua stika za kazi zao kwa pauni ya Uingereza badala ya shilingi ya Tanzania.
Mfumo huo wa ununuaji wa stika zinazobandikwa katika makasha ya kazi zinazoandaliwa na wasanii hao hutolewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA ambayo imethibitisha jambo hilo, huku ikieleza kuwa wanauza kwa pauni kwa sababu mtengenezaji wa stika hizo akaunti yake ipo mwenye pauni, siyo shilingi.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wasambazaji wa kazi hizo, wasanii na uongozi wa sanaa nchini walisema tangu kuanza rasmi kwa mfumo huoJulai 2013, kumekuwa na hali ya sintofahamu kutokana na stika hizo kuwa adimu na zinapopatikana kuuziwa kwa fedha za nje kinyume na makubaliano ya serikali na wasanii juu ya mfumo huo.
Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (Taff), Simon Mwakifamba alisema stika hizo kuuzwa kwa pauni ni changamoto mpya inayoukumba mfumo wa urasimishaji wa kazi za wasanii na kupoteza maana nzima ya zoezi hilo.
“Limekuwa ni tatizo kubwa linalowakwaza wasanii nchini hasa wasambazaji wa kazi hizo kutokana na gharama kubwa wanayotumia sambamba na kukosa stika kwa wakati mwafaka,” alisema na kuongeza;
“Mtu umeshajipanga kutoa kazi ziku mbili kabla,  ukienda  TRA unaambiwa stika zimekwisha wakati tayari  umeshachukua mkopo benki yaani unakuwa umeongeza matatizo mengine juu.”
Mwakifamba alitoa wito kwa serikali kupitia Wizara ya Viwanda na Biashara kuhakikisha inarekebisha mfumo huo uliopo sasa ambao umeonekana kuwa kero  kwa wasanii.
“Naona kutumia pauni ni kuongeza gharama kubwa ambayo isingeweza kufikiwa iwapo stika hizi zingeuzwa kwa fedha ya Tanzania.
“Kwa mujibu wa kiongozi wetu sidhani kama haya ndiyo yalikuwa makubaliano yetu. Stika moja tunanunua kwa shilingi 14, lakini unalipa kwa pauni na si shilingi ya Tanzania, hata hivyo tunauziwa kuanzia stika 100 na si chini ya hapo.”
Rais wa Shirikisho la Muziki Tanzania, Ado Novemba alisema, “Kubwa zaidi tunalolalamikia sisi kama wasambazaji na wasanii ni kuuziwa stika hizi kwa fedha isiyo yetu, kwa nini iwe hivi, pauni kila siku inabadilika mara inapanda mara inashuka.”
Novemba alisema, “Wasanii wa muziki wanalalamika kuhusu hilo hasa wa muziki wa Injili. Wasanii wa muziki wa kizazi kipya wameamua kukacha kabisa albamu kutokana na ukweli kwamba hawauzi, lakini hata waliofurahia urasimishaji bado utata unakuja kwenye stika yaani hakuna afadhali tulidhani tutapata haki, lakini sasa mambo ndivyo sivyo.”
Mkurugenzi Mtendaji wa Five Effect, kampuni inayojishughulisha na usambazaji wa kazi za wasanii, William Mtitu naye alisema, “Kuna uhaba wa stika hata hivyo tunanunua kwa pauni, wasanii tuliamua kusambaza kazi zetu wenyewe kutokana na tatizo la kutoendelea na Mhindi anatunyanyasa siyo siri akinunua kazi yako humdai tena anaitumia atakavyo.

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

Coastal ipo tayari kuanza ligi kuu, yashinda 3-0 ikiwa kambini Moshi.

Wachezaji wa Coastal Union wakifanya mazoezi mepesi muda mfupi kabla ya kukabiliana na Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini Moshi, anayeonekana pichani mwenye jezi namba 17 ni haruna Moshi 'Boban'. Mtokeo ya mechi hiyo ni ushindi wa 3-0 kwa Wagosi. Mazoezi yamekolea, uwanja wa Ushirika Moshi. Uhuru Suleiman amesifiwa na kocha kuwa ni kiungo mwenye kasi nyingi na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira. Mshambuliaji anayetumia mguu wa kushoto kutoka Uganda, Yayo Lutimba Kato amefunga bao lake la kwanza tangu kujiunga na Coastal Union ambayo imeweka kambi mjini Moshi tangu jana. Kato ambaye ametoka URA inayoshiriki ligi kuu nchini Uganda, alipatia timu yake bao la kuongoza dhidi ya Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini humo, bao hilo alilifunga kwa ufundi mkubwa katika kipindi cha pili baada ya kupokea pasi murua na kupiga shuti kali akiwa nje ya 18. Akitoa taarifa kutoka Moshi, mwenyekiti wa Wagosi Hemed Hilal ‘Aurora’ amesema “Katika dakika za lal...

Tuhuma nzito : Magufuli, Mwakyembe, Lukuvi kufikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge

Dk John Magufuli   Dar es Salaam.   Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imesema itawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akiwatuhumu kwa kulidanganya Bunge. Hatua hiyo ilitangazwa jana na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe baada ya kumhoji Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert Mrango kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka wa fedha 2011/2012. Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo kiasi cha Sh348,075,000,000 fedha za ndani zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililotajwa kuwa ni la mradi maalumu (Special Road Construction Project) hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni. “Ni vizuri leo uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. T...