Skip to main content

Magaidi Yaitikisa Tena Morogoro


POLISI mkoani Morogoro kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama imekamata washukiwa wa ugaidi waliokuwa na mifuko mikubwa iliyokuwa na majambia na bunduki kadhaa aina ya Shot gun.
 
Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Mussa Marambo, alisema hayo jana mjini hapa na kufafanua kwamba ni washukiwa sita kati ya 50 waliotiwa mbaroni, huku msako ukiendelea kuwatafuta wengine.
 
Kwa mujibu wa Kamanda Marambo, Jumatano iliyopita Polisi iliarifiwa na raia wema kuhusu uwepo wa watu hao katika Msitu wa Njeula katika kijiji cha Njeula tarafa ya Turiani, wilayani Mvomero.
 
Kukamatwa
Baada ya taarifa hiyo, Kamanda Marambo alisema Polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama, walifika eneo la msitu huo kufuatilia nyendo zao ili kuwakamata.
 
Hata hivyo, katika harakati za kuwakamata Kamanda Marambo alisema washukiwa hao walifanikiwa kutoroka, isipokuwa mmoja ambaye alitiwa mbaroni.
 
Katika purukushani hiyo msituni, Kamanda Marambo alisema mshukiwa huyo aliyekamatwa, alijaribu kumjeruhi askari kwa kumkata na jambia mkononi, lakini umakini wa askari Polisi ulisaidia kumuepusha mwenzao asijeruhiwe na kukamata mshukiwa.
 
Msako wa watu hao uliendelea ambapo Kamanda Marambo alisema baada ya muda, washukiwa wengine watano kati ya 49 waliokuwa wametoroka, walitiwa mbaroni huku wengine 44 wakitokomea porini.
 
Walikotokea 
Uchunguzi wa awali wa Polisi, umebaini kuwa washukiwa hao wakiwa na mifuko hiyo mikubwa iliyohifadhi majambia na bunduki, walitokea wilayani Bagamoyo mkoani Pwani, kupitia Tanga huku wakitumia mabasi ya kuunganisha.
 
Kutoka Bagamoyo, Kamanda Marambo alisema washukiwa hao walizunguka kwa kwenda mpaka Segera mkoani Tanga, wakaingia Handeni ndipo wakatokea katika kijiji cha Njeula tarafa ya Turiani wilayani Mvomero.
 
Msako shirikishi 
Kwa mujibu wa Kamanda Marambo, msako mkali unaendeshwa katika msitu huo na mahali pengine ili kufanikisha kutiwa mbaroni kwa washukiwa waliobaki.
 
“Ninachoweza kusema kwa kushirikiana na wenzetu wa Tanga, bado tunaendelea na msako kwenye msitu huo uliopo mpakani lakini siwezi kujata majina yao kwa sasa wala kueleza wanatoka wapi au nia yao ni nini,” alisema.
 
Kamanda Marambo pia alikataa kutaja idadi ya majambia wala bunduki hadi watakapokamilisha uchunguzi na upelelezi wa suala hilo.
 
Hivyo aliwataka wananchi wenye mapenzi mema na Taifa lao, kuendelea kutoa ushirikiano kwa vyombo vya ulinzi na usalama ili kufichua watu wanaowatilia shaka wanapowakuta misituni na mitaani, ili hatua za haraka zichukuliwe.
 
Hii ni mara ya tatu kwa wanaoshukiwa na vitendo vya kigaidi kukamatwa mkoani Morogoro, ambapo hivi karibuni washukiwa wengine 25 walikamatwa kwa nyakati tofauti katika eneo la Kidatu wilayani Kilombero na wameshafikishwa mahakamani

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

Coastal ipo tayari kuanza ligi kuu, yashinda 3-0 ikiwa kambini Moshi.

Wachezaji wa Coastal Union wakifanya mazoezi mepesi muda mfupi kabla ya kukabiliana na Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini Moshi, anayeonekana pichani mwenye jezi namba 17 ni haruna Moshi 'Boban'. Mtokeo ya mechi hiyo ni ushindi wa 3-0 kwa Wagosi. Mazoezi yamekolea, uwanja wa Ushirika Moshi. Uhuru Suleiman amesifiwa na kocha kuwa ni kiungo mwenye kasi nyingi na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira. Mshambuliaji anayetumia mguu wa kushoto kutoka Uganda, Yayo Lutimba Kato amefunga bao lake la kwanza tangu kujiunga na Coastal Union ambayo imeweka kambi mjini Moshi tangu jana. Kato ambaye ametoka URA inayoshiriki ligi kuu nchini Uganda, alipatia timu yake bao la kuongoza dhidi ya Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini humo, bao hilo alilifunga kwa ufundi mkubwa katika kipindi cha pili baada ya kupokea pasi murua na kupiga shuti kali akiwa nje ya 18. Akitoa taarifa kutoka Moshi, mwenyekiti wa Wagosi Hemed Hilal ‘Aurora’ amesema “Katika dakika za lal...

Tuhuma nzito : Magufuli, Mwakyembe, Lukuvi kufikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge

Dk John Magufuli   Dar es Salaam.   Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imesema itawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akiwatuhumu kwa kulidanganya Bunge. Hatua hiyo ilitangazwa jana na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe baada ya kumhoji Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert Mrango kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka wa fedha 2011/2012. Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo kiasi cha Sh348,075,000,000 fedha za ndani zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililotajwa kuwa ni la mradi maalumu (Special Road Construction Project) hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni. “Ni vizuri leo uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. T...