Skip to main content

Rais Kikwete azuia ‘ULAJI ’ Trafiki.......Ataka Baraza la Usalama Lianzishe Mfumo wa Kulipa Faini Kwa Njia ya Benki


RAIS Jakaya Kikwete ameliagiza Baraza la Taifa la Usalama Barabarani, kuanzisha mara moja mfumo wa ulipaji faini kwa njia ya Benki na mitandao ya simu za mkononi ili kupunguza ushawishi wa vitendo vya rushwa kwa askari wa kikosi cha usalama barabarani nchini.

Pia, ameagiza kuanzishwa mfumo wa kuweka alama kwenye leseni za madereva wanaokiuka sheria na kutumia njia hiyo kuwafungia, ikiwa ni hatua mojawapo ya kudhibiti wimbi la ajali za barabarani hapa nchini.

Rais Kikwete alitoa agizo hilo jana katika viwanja vya Tangamano wakati alipokuwa akizindua Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani Kitaifa, inayofanyika mkoani Tanga, ikiwa imebeba kaulimbiu inayosema ‘Endesha Salama, Okoa Maisha’.

Alisema asilimia 56 ya ajali za barabarani, zinatokana na uzembe na ukosefu wa umakini kwa madereva na kwamba hatua hiyo inasababisha vifo, majeruhi na uharibifu wa mali na hata kuathiri ustawi wa Kaya na Uchumi wa Taifa.

“Hivi mpaka sasa Baraza na Kikosi cha usalama barabarani wanashindwaje kutumia mifumo ya kidigitali kwa nini mpaka leo hakuna kamera barabarani? Kwanza ingesaidia kudhibiti ajali na uvunjaji wa sheria, lakini hata vitendo vya rushwa ambavyo navyo vinachangia ongezeko hili la wimbi wa ajali hapa nchini,” alisema Rais Kikwete.

Alisema katika kipindi cha miaka mitano kuanzia mwaka 2010 hadi 2014, jumla ya watu 19,264 walipoteza maisha kutokana na ajali za barabarani na kwamba idadi ya ya waliokufa katika kipindi cha mwaka peke yake ni watu 3,534 sawa na idadi ya wanaopeteza maisha kutokana na ugonjwa wa malaria.

Kufuatia hatua hiyo, amelitaka baraza hilo kufanya mapendekezo ya marekebisho ya sheria za usalama barabarani hasa pale penye mapungufu ili kuweza kusaidia kudhibiti wimbi la ajali linalochangia upotevu wa nguvu kazi ya Taifa.

“Kikosi cha usalama barabarani kiongeze kasi ya kudhibiti ajali za barabarani na kuwachukulia hatua za kisheria Askari wanaojihusisha na vitendo vya rushwa….lakini lisilale katika kutoa elimu ya sheria za usalama barabarani hasa kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari,” alisisitiza Rais Kikwete.

Kwa upande Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Usalama Barabarani,Naibu Kamishna wa Jeshi la Polisi, Mohamed Mpinga alisema lengo kuu la maadhimisho ya siku hiyo ni kuhamasisha matumizi salama ya barabara pamoja na kuwakumbusha watumiaji namna rahisi ya kutumia barabara ili kupunguza ajali zisizo za lazima.

“Tunapoadhimisha siku hii tunawakumbusha watumiaji kuwa ajenda kuu ya Taifa ni mapambano dhidi ya ajali za barabarani, jambo ambalo linaweza kuadhibitiwa kwa sababu ya uzembe na uvunjaji wa Sheria za Barabarani”,alisema Kamanda Mpinga.

Hata hivyo, alisema katika maadhimisho hayo Baraza limejipanga kufanya Mkutano Mkuu wa wadau utakaoshirikisha nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, sambamba na mafunzo kwa madereva 300 wa daladala na walimu 200 wa shule za msingi kwa lengo la kujenga uelewa kuhusu sheria za usalama barabarani.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Said Magalula alisema takwimu zinaonesha katika kipindi cha mwezi Januari mpaka Juni mwaka huu, ajali za barabarani zilikuwa 52 ambapo vifo vilikuwa 59 na majeruhi 68. Magalula alisema mkoa huo kwa mwaka 2014 ulifanikiwa kuingia katika tano bora kati ya mikoa ambayo imefanikiwa kudhibiti ajali za barabarani.

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

Coastal ipo tayari kuanza ligi kuu, yashinda 3-0 ikiwa kambini Moshi.

Wachezaji wa Coastal Union wakifanya mazoezi mepesi muda mfupi kabla ya kukabiliana na Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini Moshi, anayeonekana pichani mwenye jezi namba 17 ni haruna Moshi 'Boban'. Mtokeo ya mechi hiyo ni ushindi wa 3-0 kwa Wagosi. Mazoezi yamekolea, uwanja wa Ushirika Moshi. Uhuru Suleiman amesifiwa na kocha kuwa ni kiungo mwenye kasi nyingi na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira. Mshambuliaji anayetumia mguu wa kushoto kutoka Uganda, Yayo Lutimba Kato amefunga bao lake la kwanza tangu kujiunga na Coastal Union ambayo imeweka kambi mjini Moshi tangu jana. Kato ambaye ametoka URA inayoshiriki ligi kuu nchini Uganda, alipatia timu yake bao la kuongoza dhidi ya Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini humo, bao hilo alilifunga kwa ufundi mkubwa katika kipindi cha pili baada ya kupokea pasi murua na kupiga shuti kali akiwa nje ya 18. Akitoa taarifa kutoka Moshi, mwenyekiti wa Wagosi Hemed Hilal ‘Aurora’ amesema “Katika dakika za lal...

Tuhuma nzito : Magufuli, Mwakyembe, Lukuvi kufikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge

Dk John Magufuli   Dar es Salaam.   Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imesema itawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akiwatuhumu kwa kulidanganya Bunge. Hatua hiyo ilitangazwa jana na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe baada ya kumhoji Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert Mrango kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka wa fedha 2011/2012. Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo kiasi cha Sh348,075,000,000 fedha za ndani zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililotajwa kuwa ni la mradi maalumu (Special Road Construction Project) hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni. “Ni vizuri leo uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. T...