Skip to main content

Wadau wakosoa kambi ya Stars

Wachezaji wa Taifa Stars wakiwa mazoezini
Wachezaji wa Taifa Stars wakiwa mazoezini kujiandaa kwa mchezo wa michuano ya awali ya Mataifa ya Afrika ya 2017 (Afcon) dhidi ya Nigeria. Mazoezi hayo yanafanyika kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam. Picha na Said Khamis 
By Oliver Albert, Mwananchi
Dar es Salaam. Uamuzi wa Shirikisho la Soka Tanzania  (TFF) kuitisha kambi ya timu ya Taifa wakati klabu zikiwa kwenye maandalizi ya msimu mpya wa ligi, umepokewa kwa hisia tofauti na wadau wa mchezo huo, baadhi wakizilaumu Yanga na Azam kwa kuzuia wachezaji wao na wengine wakiliponda shirikisho hilo kwa kutokuwa makini.
Kocha Charles Mkwassa amelazimika kuita wachezaji 10 wa ziada kujaza nafasi za wachezaji kutoka Yanga na Azam  zilizoweka kambi nje ya  Dar es Salaam. Stars inajiandaa kwa mechi ya Mataifa ya Afrika dhidi ya Nigeria.
Wakizungumza na gazeti hili, wadau hao walisema Yanga na Azam hazijafanya kitu kizuri, lakini pia wakaeleza kuwa TFF ilitakiwa kupanga ratiba za klabu kwa kuangalia tarehe za mechi za Stars.
Msemaji wa Ruvu Shooting, Masau Bwire alisema Yanga na Azam hazikupaswa kuwazuia wachezaji wao kujiunga na kambi ya Stars kwani mechi ya Ngao ya Jamii ni ya kawaida, ukilinganisha na ile dhidi ya Nigeria.
“Tumeshuhudia Ulaya ambako ndiko wenye mpira wao inapofika timu ya taifa ni suala jingine, hivyo sioni kama ni sahihi kwa Yanga na Azam kuwazuia wachezaji wao kujiunga na kambi,” alisema Bwire.
“Inapofika hali ya kugongana kwa ratiba kama hivi unaangalia umuhimu wa mechi. Wangewaachia walioitwa Stars wajiunge na kambi, hao waliobaki wangecheza hiyo mechi ya Ngao ya Jamii,” alisema Bwire.
“Ndiyo maana timu ikasajili wachezaji 30 ili kama wengine hawapo, wengine wanachukua nafasi, lakini kwa jinsi hali hii ilivyojitokeza inaonyesha kabisa Yanga na Azam ni waoga. Wanawategemea wachezaji fulani na bila wao wanaona hakuna timu jambo ambalo siyo sahihi.
“TFF wanatakiwa kubadilika, wanapopanga ratiba ya ligi waaangalie na kujiridhisha kuwa haiingiliani na mashindano mengine hasa yanayohusu timu ya Taifa.”
Meneja wa Mwadui, Khalid Adam alisema Azam na Yanga ziko sahihi kuwazuia nyota wao kujiunga na Taifa Stars kwani  hata klabu nyingine duniani zinafanya hivyo kwa masilahi ya klabu hizo.
“Kama tunafuata mfumo wa dunia ,timu ya Taifa inafanya maandalizi siku  nne hadi tano kulingana na kalenda ya Fifa (Shirikisho la Soka la Kimataifa, kuwazuia wachezaji si kwa klabu za hapa nchini kwani kuna wakati hata Barcelona  iliwahi kumzuia Lionel Messi kujiunga na timu ya Argentina, inategemea hayo mashindano ya nini na je ni muda wa kalenda ya Fifa.

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

Coastal ipo tayari kuanza ligi kuu, yashinda 3-0 ikiwa kambini Moshi.

Wachezaji wa Coastal Union wakifanya mazoezi mepesi muda mfupi kabla ya kukabiliana na Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini Moshi, anayeonekana pichani mwenye jezi namba 17 ni haruna Moshi 'Boban'. Mtokeo ya mechi hiyo ni ushindi wa 3-0 kwa Wagosi. Mazoezi yamekolea, uwanja wa Ushirika Moshi. Uhuru Suleiman amesifiwa na kocha kuwa ni kiungo mwenye kasi nyingi na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira. Mshambuliaji anayetumia mguu wa kushoto kutoka Uganda, Yayo Lutimba Kato amefunga bao lake la kwanza tangu kujiunga na Coastal Union ambayo imeweka kambi mjini Moshi tangu jana. Kato ambaye ametoka URA inayoshiriki ligi kuu nchini Uganda, alipatia timu yake bao la kuongoza dhidi ya Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini humo, bao hilo alilifunga kwa ufundi mkubwa katika kipindi cha pili baada ya kupokea pasi murua na kupiga shuti kali akiwa nje ya 18. Akitoa taarifa kutoka Moshi, mwenyekiti wa Wagosi Hemed Hilal ‘Aurora’ amesema “Katika dakika za lal...

Tuhuma nzito : Magufuli, Mwakyembe, Lukuvi kufikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge

Dk John Magufuli   Dar es Salaam.   Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imesema itawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akiwatuhumu kwa kulidanganya Bunge. Hatua hiyo ilitangazwa jana na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe baada ya kumhoji Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert Mrango kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka wa fedha 2011/2012. Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo kiasi cha Sh348,075,000,000 fedha za ndani zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililotajwa kuwa ni la mradi maalumu (Special Road Construction Project) hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni. “Ni vizuri leo uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. T...