Skip to main content

Wadau wakosoa kambi ya Stars

Wachezaji wa Taifa Stars wakiwa mazoezini
Wachezaji wa Taifa Stars wakiwa mazoezini kujiandaa kwa mchezo wa michuano ya awali ya Mataifa ya Afrika ya 2017 (Afcon) dhidi ya Nigeria. Mazoezi hayo yanafanyika kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam. Picha na Said Khamis 
By Oliver Albert, Mwananchi
Dar es Salaam. Uamuzi wa Shirikisho la Soka Tanzania  (TFF) kuitisha kambi ya timu ya Taifa wakati klabu zikiwa kwenye maandalizi ya msimu mpya wa ligi, umepokewa kwa hisia tofauti na wadau wa mchezo huo, baadhi wakizilaumu Yanga na Azam kwa kuzuia wachezaji wao na wengine wakiliponda shirikisho hilo kwa kutokuwa makini.
Kocha Charles Mkwassa amelazimika kuita wachezaji 10 wa ziada kujaza nafasi za wachezaji kutoka Yanga na Azam  zilizoweka kambi nje ya  Dar es Salaam. Stars inajiandaa kwa mechi ya Mataifa ya Afrika dhidi ya Nigeria.
Wakizungumza na gazeti hili, wadau hao walisema Yanga na Azam hazijafanya kitu kizuri, lakini pia wakaeleza kuwa TFF ilitakiwa kupanga ratiba za klabu kwa kuangalia tarehe za mechi za Stars.
Msemaji wa Ruvu Shooting, Masau Bwire alisema Yanga na Azam hazikupaswa kuwazuia wachezaji wao kujiunga na kambi ya Stars kwani mechi ya Ngao ya Jamii ni ya kawaida, ukilinganisha na ile dhidi ya Nigeria.
“Tumeshuhudia Ulaya ambako ndiko wenye mpira wao inapofika timu ya taifa ni suala jingine, hivyo sioni kama ni sahihi kwa Yanga na Azam kuwazuia wachezaji wao kujiunga na kambi,” alisema Bwire.
“Inapofika hali ya kugongana kwa ratiba kama hivi unaangalia umuhimu wa mechi. Wangewaachia walioitwa Stars wajiunge na kambi, hao waliobaki wangecheza hiyo mechi ya Ngao ya Jamii,” alisema Bwire.
“Ndiyo maana timu ikasajili wachezaji 30 ili kama wengine hawapo, wengine wanachukua nafasi, lakini kwa jinsi hali hii ilivyojitokeza inaonyesha kabisa Yanga na Azam ni waoga. Wanawategemea wachezaji fulani na bila wao wanaona hakuna timu jambo ambalo siyo sahihi.
“TFF wanatakiwa kubadilika, wanapopanga ratiba ya ligi waaangalie na kujiridhisha kuwa haiingiliani na mashindano mengine hasa yanayohusu timu ya Taifa.”
Meneja wa Mwadui, Khalid Adam alisema Azam na Yanga ziko sahihi kuwazuia nyota wao kujiunga na Taifa Stars kwani  hata klabu nyingine duniani zinafanya hivyo kwa masilahi ya klabu hizo.
“Kama tunafuata mfumo wa dunia ,timu ya Taifa inafanya maandalizi siku  nne hadi tano kulingana na kalenda ya Fifa (Shirikisho la Soka la Kimataifa, kuwazuia wachezaji si kwa klabu za hapa nchini kwani kuna wakati hata Barcelona  iliwahi kumzuia Lionel Messi kujiunga na timu ya Argentina, inategemea hayo mashindano ya nini na je ni muda wa kalenda ya Fifa.

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

MAJINA YA WASHIRIKI NA WA WEZESHAJI WA FILM YA HOUSE GIRL!

CAST SELEMANI MOHAMED / BUNTO ANDREW / C-O YORAM MWETA / MGANGA MWANTUMU / MKE WA C-O JOHN / MCHUNGAJI BI FURURATU / JINI WAOMBOLEZAJI SAUMU HUSENI HASHIMU BABA RASTA MAN YOHANNA TAMILWAI SAIDI MWALUBADU SEMY STIR SELEMANI MOHAMEDI  AND ANDREW C-O LOCATION ATHUMANI HAMADI MAKE UP MWASHAMBA RAMADHANI BEDUI DEREVA DAUDI SPOONSER SAIDI SHABANI AND THE FRESH2012 GLOB SOUND PRODUCER J-B LIGHT YOHANNA TAMILWAI THENK YOU THE FRESH ENERTAINMENT AND THE FRESH2012 BLOG CONTACTS 0653785027 +255714091786 ZAIDI TEMBELEA www.the-fresh.blogspot.com ADRESS Thefresh@ymail.com AU Saidshabani60@gmai.com

DOWNLOAD BERRY BLACK FT. ALI KIBA - ISHARA ZANGU