Skip to main content

Serikali bado inayo fursa kurekebisha kasoro za Sensa

KATIKA hali isiyotegemewa, zoezi la Sensa ya watu na Makazi iliyoanza juzi nchini kote, imekumbana na kasoro na vikwazo mbalimbali, huku tatizo kubwa likiwa ni uhaba wa vifaa na wenyeviti wa mitaa kugoma kuwaongoza makarani kuendesha zoezi hilo kwa madai ya kutolipwa posho.
 
Mbali na tatizo la baadhi ya wananchi kugoma kuhesabiwa ambalo tayari linafahamika kwa mamlaka za kiserikali, uchunguzi wa gazeti hili uliofanyika katika mikoa mbalimbali pia umegundua kwamba kasoro nyingine zinazolikabili zoezi hilo hazikutegemewa na  zilijitokeza tu mara baada ya zoezi hilo kuanza juzi. 
 
Tunaweza kusema kwamba kasoro zilizojitokeza ni za aina mbili. Moja ni kasoro zinazoweza kuwekwa katika kundi la kasoro zilizosababishwa na mamlaka za kiserikali. Pili, ni kasoro zilizosababishwa na wananchi wenyewe, wakiwamo viongozi wa mitaa ambao walishindwa kuwahamasisha wananchi katika ngazi hizo kuhusu zoezi hilo la Sensa ya Watu na Makazi.
   Pamoja na kusema kwamba mamlaka za kiserikali hazipaswi pekee kubeba lawama hizo, bado tuna kila sababu ya kusema kwamba mamlaka hizo lazima zibebe nyingi ya lawama hizo, hasa baada ya kufanya uchambuzi wa kina wa kila kasoro iliyojitokeza. Kwa maneno mengine, hata pale panapoonekana kwamba kasoro zilizojitokeza zilitokana na wananchi wenyewe, bado kuna dalili zinazoonyesha kwamba mamlaka za kiserikali zilichangia kasoro hizo kwa namna moja ama nyingine.
 
Tutatoa baadhi ya mifano. Katika baadhi ya mikoa, wenyeviti wa vitongoji na vijiji waligoma kushiriki katika  zoezi hilo baada ya Serikali kushindwa kuwatengea posho kama ilivyofanya kwa makarani na wasimamizi wa Sensa. Pamoja na kupiga filimbi ya kuanza kwa zoezi hilo, kwa maana ya kuashiria kwamba matayarisho ya zoezi hilo yamekamilika, Serikali ghafla ilijikuta ikiwa na masuala kadhaa muhimu ambayo awali ilikuwa haikuyatilia maanani.
   Baada ya Serikali kushtuka saa za ‘lala salama’ na kusema ingewalipa posho kwa ushiriki wao, ilibidi iongeze kiwango cha posho baada ya wenyeviti hao kuzikataa kwa madai kwamba zilikuwa hazitoshi. Hapa tunadhani Serikali ilifanya makosa kwa kutotambua mapema ukweli kwamba makarani wa Sensa wasingeweza kufanya kazi hiyo bila kuandamana na viongozi hao kutoka kaya moja hadi nyingine na pia kwamba viongozi hao wasingefanya kazi hiyo bila malipo.
 
Hivyo, kitendo cha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwa mkoani Katavi juzi,  kuwatangazia  wenyeviti hao wa vijiji na vitongoji kushiriki kwenye zoezi hilo na kuwaahidi kwamba wangelipwa fedha zao, kilionyesha pasipo shaka kwamba Serikali ilikuwa imejisahau kuhusu ushiriki wa viongozi hao katika zoezi hilo muhimu.  Kutokana na hali hiyo, inaonekana kwamba pengine Serikali haikuwa imetenga katika bajeti yake fedha za kuwalipa viongozi hao.
 
Tumeshangazwa pia na taarifa kwamba katika baadhi ya mikoa, makarani wa Sensa walitishia kugoma siyo tu kutokana na kutolipwa posho zao, bali pia walizilalamikia kamati za Sensa kwa kuchelewesha vifaa vya zoezi hilo katika vituo vyao, kwa maana ya vitambulisho, sare na dodoso na kusema wasingeruhusiwa kuingia katika kaya yoyote pasipo kuwa na vifaa hivyo. Katika baadhi ya mikoa, zoezi hilo lilikwamishwa na mwamko mdogo wa wananchi ambao walionekana kuendelea na shughuli zao za kilimo na ufugaji kama kawaida wakidai walikuwa hawajui kinachoendelea.
 
Tumeambiwa kwamba katika baadhi ya sehemu, kukosekana kwa wakalimani kulisababisha matatizo makubwa, hasa katika jamii za wafugaji wa jamii ya Kitaturu na Wahdzabe kutokana na kushindwa kutafsiri dodoso. Kasoro hiyo pia ilijitokeza katika mikoa ya Arusha na Mwanza ambako wananchi wengi, hasa jamii za wafugaji zinazoishi katika maeneo ya pembezoni walionyesha kutokuwa na uwezo wa kuelewa dodoso zilizokuwa katika lugha ya Kiswahili.
 
Hata hivyo, sisi tunasema Serikali bado inao uwezo na muda wa kutosha kumaliza kasoro hizo zilizojitokeza, ikiwa ni pamoja na kushawishi, badala ya kutumia nguvu, wananchi waliosusia Sensa ili washiriki katika zoezi hilo muhimu kwa taifa.

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

Coastal ipo tayari kuanza ligi kuu, yashinda 3-0 ikiwa kambini Moshi.

Wachezaji wa Coastal Union wakifanya mazoezi mepesi muda mfupi kabla ya kukabiliana na Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini Moshi, anayeonekana pichani mwenye jezi namba 17 ni haruna Moshi 'Boban'. Mtokeo ya mechi hiyo ni ushindi wa 3-0 kwa Wagosi. Mazoezi yamekolea, uwanja wa Ushirika Moshi. Uhuru Suleiman amesifiwa na kocha kuwa ni kiungo mwenye kasi nyingi na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira. Mshambuliaji anayetumia mguu wa kushoto kutoka Uganda, Yayo Lutimba Kato amefunga bao lake la kwanza tangu kujiunga na Coastal Union ambayo imeweka kambi mjini Moshi tangu jana. Kato ambaye ametoka URA inayoshiriki ligi kuu nchini Uganda, alipatia timu yake bao la kuongoza dhidi ya Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini humo, bao hilo alilifunga kwa ufundi mkubwa katika kipindi cha pili baada ya kupokea pasi murua na kupiga shuti kali akiwa nje ya 18. Akitoa taarifa kutoka Moshi, mwenyekiti wa Wagosi Hemed Hilal ‘Aurora’ amesema “Katika dakika za lal...

Tuhuma nzito : Magufuli, Mwakyembe, Lukuvi kufikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge

Dk John Magufuli   Dar es Salaam.   Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imesema itawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akiwatuhumu kwa kulidanganya Bunge. Hatua hiyo ilitangazwa jana na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe baada ya kumhoji Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert Mrango kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka wa fedha 2011/2012. Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo kiasi cha Sh348,075,000,000 fedha za ndani zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililotajwa kuwa ni la mradi maalumu (Special Road Construction Project) hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni. “Ni vizuri leo uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. T...