Skip to main content

Rais Kikwete Akiri Mazingira Mabovu Magereza



RAIS Jakaya Kikwete amekiri kuwapo mazingira mabovu ya Jeshi la Magereza nchini na kulitaka jeshi hilo kubuni njia za uzalishaji wa bidhaa zao zitakazoweza kuwaletea faida na taifa kwa ujumla.
 
Aliyasema hayo jijini Dar es Salaam jana kwenye sherehe za kumaliza kozi kwa maofisa 104 wa ngazi ya juu wa Jeshi la Magereza yaliyofanyika katika Chuo cha Taaluma na Urekebishaji Ukonga.
 
Alisema mazingira mabovu yanachangiwa na wingi, msongamano wa wafungwa na watuhumiwa katika magereza hali inayofanya jamii kuwa na malalamiko ya mara kwa mara.
 
“Kila mwaka wanaotetea haki za binadamu wanapopita kwenye magereza zetu, tunakuwa tunashindwa kwenye suala la msongamano ndani ya gereza na hii inaonyesha magereza tulizonazo 126 hazitoshelezi kulingana na kasi ya ongezeko la uhalifu.
 
“Hii inajidhihirisha wazi kwani kila inapofika sikukuu za Muungano Aprili 26, tunasamehe wafungwa, lakini ikifika Desemba 9 Sikukuu ya Uhuru unakuta wameongezeka mara mbili,” alisema Rais Kikwete.
 
Alisema ili jeshi liweze kutimiza majukumu yake vizuri, ni lazima kuwe na watu, ujuzi na vitendea kazi ambavyo bado vimeonekana kuwa ni changamoto kwa jeshi hilo.
 
Pamoja na hali hiyo alilitaka Jeshi la Magereza kuwa na malengo ya kuboresha viwango bora.
 
“Jeshi linasifika kwa kuzalisha chakula na bidhaa bora, lakini kwenye uzalishaji wenu msiishie kweye mazao ya chakula, bali muangalie na mazao ya thamani pamoja na kuanzisha viwanda vikubwa na kilimo cha umwagiliaji,” alisema Rais Kikwete.
 
Aidha alilitaka jeshi hilo kuhakikisha linaharakisha mchakato wa Sera ya Taifa ya Magereza na mpango kazi wake ambao ameutaka uwasilishwe kabla hajaondoka madarakani Oktoba mwaka huu.
 
Awali Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Minja, alisema jeshi hilo linakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwamo la ongezeko la mahabusu, upungufu wa fedha kutokana na gharama kubwa ya uendeshaji, makazi ya maofisa na askari, ofisi chakavu na suala la usafirishaji.
 
“Mazingira yetu hayaridhishi sana, nyumba ni chache na zilizopo ni chakavu, pia magari kwa ajili ya usafirishaji bado ni tatizo sambamba na majengo machache ya mahakama,” alisema Kamishna Minja.

Popular posts from this blog

Matokeo ya Mtihani wa Darasa la Saba 2013 wilaya ya tanga mjini pekee!!!

ARAFAH ENG-MED PRIMARY SCHOOL - P2007029 AVICENNA ENG -MD PRIMARY SCHOOL - P2007051 AZIMIO PRIMARY SCHOOL - P2007032 BOMBO PRIMARY SCHOOL - P2007001 BURHANI ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007055 CHANGA ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007033 CHANGA PRIMARY SCHOOL - P2007002 CHUDA PRIMARY SCHOOL - P2007034 CHUMA PRIMARY SCHOOL - P2007003 CHUMBAGENI PRIMARY SCHOOL - P2007004 DARAJANI PRIMARY SCHOOL - P2007005 DAYSTAR ENG - MD PRIMARY SCHOOL - P2007053 DONGE PRIMARY SCHOOL - P2007035 EBEN EZER ENG- MD PR SCHOOL - P2007048 ECKERNFORDE ENG-MD PRIMARY SCHOOL - P2007044 GOFU-JUU PRIMARY SCHOOL - P2007006 INDIAN OCEAN ENG-MED PR SCHOOL - P2007049 JABIR BIN ZAID ENG- MED PRIMARY SCHOOL - P2007052 JUHUDI PRIMARY SCHOOL - P2007036 KANA CENTRAL ENGMED PRIMARY SCHOOL - P2007054 KANA PRIMARY SCHOOL - P2007007 KISOSORA PRIMARY SCHOOL - P2007008 KOMBEZI PRIMARY SCHOOL - P2007009 KWAKAEZA PRIMARY SCHOOL - P2007026 KWANJEKA PRIMARY SCHOOL - P2007010 MABAW...

Coastal ipo tayari kuanza ligi kuu, yashinda 3-0 ikiwa kambini Moshi.

Wachezaji wa Coastal Union wakifanya mazoezi mepesi muda mfupi kabla ya kukabiliana na Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini Moshi, anayeonekana pichani mwenye jezi namba 17 ni haruna Moshi 'Boban'. Mtokeo ya mechi hiyo ni ushindi wa 3-0 kwa Wagosi. Mazoezi yamekolea, uwanja wa Ushirika Moshi. Uhuru Suleiman amesifiwa na kocha kuwa ni kiungo mwenye kasi nyingi na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira. Mshambuliaji anayetumia mguu wa kushoto kutoka Uganda, Yayo Lutimba Kato amefunga bao lake la kwanza tangu kujiunga na Coastal Union ambayo imeweka kambi mjini Moshi tangu jana. Kato ambaye ametoka URA inayoshiriki ligi kuu nchini Uganda, alipatia timu yake bao la kuongoza dhidi ya Machava FC kwenye uwanja wa Ushirika mjini humo, bao hilo alilifunga kwa ufundi mkubwa katika kipindi cha pili baada ya kupokea pasi murua na kupiga shuti kali akiwa nje ya 18. Akitoa taarifa kutoka Moshi, mwenyekiti wa Wagosi Hemed Hilal ‘Aurora’ amesema “Katika dakika za lal...

Tuhuma nzito : Magufuli, Mwakyembe, Lukuvi kufikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge

Dk John Magufuli   Dar es Salaam.   Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imesema itawafikisha kwenye Kamati ya Maadili ya Bunge, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe akiwatuhumu kwa kulidanganya Bunge. Hatua hiyo ilitangazwa jana na Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe baada ya kumhoji Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Balozi Herbert Mrango kuhusu hati ya mashaka waliyoipata kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka wa fedha 2011/2012. Kamati hiyo ilieleza kuwa kwenye Bajeti ya mwaka huo kiasi cha Sh348,075,000,000 fedha za ndani zilizokuwa zimetengwa chini ya fungu lililotajwa kuwa ni la mradi maalumu (Special Road Construction Project) hazikutumiwa kwa malengo yaliyoelezwa bungeni. “Ni vizuri leo uiambie kamati fedha hizi ziliombwa kwa kitu gani na zilitumika kwa jambo gani. T...